OMBI KWA TCU: Angalieni upya cut off Ponts kwa kozi za afya

mbingunikwetu

JF-Expert Member
Feb 17, 2015
13,663
18,037
TCU ilipandisha cut off points kwa ajili ya kujiunga na kozi za afya kwa digrii na kuwa 8 yaani C, C na D badala ya D, D na S. Kwa maoni yangu sioni ulazima wa kutaka MTU apate D ya physics kama kigezo cha kusoma kozi ya afya. Masomo ya msingi kwa kozi za afya ni chemistry na biology. Kwa hiyo wangerudisha kigezo cha awali kuhusu physics cha kuhitajika kupata angalau S ya physics. Kwa hiyo kigezo kiwe C, C na S point 6.5. Madaktari bingwa tulionao Leo wengi walipata S ya physics na hilo halikuwa kikwazo kwao kusomea udaktari au pharmacy. Hiki kigezo cha sasa kinaharibu sana ndoto za watu na baadhi ya vyuo vinaweza kuwa vinakosa wanafunzi!!! Chonde chonde tazameni upya vigezo hivi. Watoto ndo mwezi ujao wanaanza mitihani yao! Ni vizuri kuweka vigezo kabla hawajafanya mitihani ya kidato cha sita.
 
Chuo gani kimekosa wanafunzi..mind you course za afya zina ushindani kuliko kawaida na pia mbona watu wanapataga hadi two ya kumi kwa miaka hii na bado hawapati kirahisi...kada ya afya sio lelemama,kwa hiyo sioni haya ya point kushushwa
 
TCU ilipandisha cut off points kwa ajili ya kujiunga na kozi za afya kwa digrii na kuwa 8 yaani C, C na D badala ya D, D na S. Kwa maoni yangu sioni ulazima wa kutaka MTU apate D ya physics kama kigezo cha kusoma kozi ya afya. Masomo ya msingi kwa kozi za afya ni chemistry na biology. Kwa hiyo wangerudisha kigezo cha awali kuhusu physics cha kuhitajika kupata angalau S ya physics. Kwa hiyo kigezo kiwe C, C na S point 6.5. Madaktari bingwa tulionao Leo wengi walipata S ya physics na hilo halikuwa kikwazo kwao kusomea udaktari au pharmacy. Hiki kigezo cha sasa kinaharibu sana ndoto za watu na baadhi ya vyuo vinaweza kuwa vinakosa wanafunzi!!! Chonde chonde tazameni upya vigezo hivi. Watoto ndo mwezi ujao wanaanza mitihani yao! Ni vizuri kuweka vigezo kabla hawajafanya mitihani ya kidato cha sita.
Chief,uhitaji unatofautiana sana zamani na sasa.
Kama vijana wengi wanafaulu na mpaka wanakosa chuo kuna ulazima gani wa TCU kushusha vigezo? Na hao ambao hawakupata kozi za afya,ulazima upo wapi wa wao kuchukua kozi za afya?!
 
Chuo gani kimekosa wanafunzi..mind you course za afya zina ushindani kuliko kawaida na pia mbona watu wanapataga hadi two ya kumi kwa miaka hii na bado hawapati kirahisi...kada ya afya sio lelemama,kwa hiyo sioni haya ya point kushushwa
Vyuo vya private vinabaki na nafasi. Ushindani upo vyuo vya serikali lakini vyuo ksma Kariuki, st Joseph havina ushindani kwa ajili ya kuwa na ada ndefu! Sioni sababu ya mwanafunzi mwenye C C S au hata C C E asiruhusiwe kudahiliwa. Uwezo anao mkubwa tu wa kumudu kozi hizo. Akose kwa ushindani na si kusema hana sifa.
 
Vyuo vya private vinabaki na nafasi. Ushindani upo vyuo vya serikali lakini vyuo ksma Kariuki, st Joseph havina ushindani kwa ajili ya kuwa na ada ndefu! Sioni sababu ya mwanafunzi mwenye C C S au hata C C E asiruhusiwe kudahiliwa. Uwezo anao mkubwa tu wa kumudu kozi hizo. Akose kwa ushindani na si kusema hana sifa.
Una uhakika kati ya hvyo vyuo kuna nafasi zimebaki? Unafamu waliwekewa idadi ya wanafunzi wa kudahili na TCU na baadhi ya hivyo vyuo wamevuka hiyo idadi.
Usilazimishe mambo mkuu,unaweza anza CO au Pharm Technician halafu uje utoboe na hyo MD au BPharm
 
Vyuo vya private vinabaki na nafasi. Ushindani upo vyuo vya serikali lakini vyuo ksma Kariuki, st Joseph havina ushindani kwa ajili ya kuwa na ada ndefu! Sioni sababu ya mwanafunzi mwenye C C S au hata C C E asiruhusiwe kudahiliwa. Uwezo anao mkubwa tu wa kumudu kozi hizo. Akose kwa ushindani na si kusema hana sifa.
Wewe bipa shaka ni kidato cha sita hivi kwwli una sema vyuo kama Kairuki na St Joseph havina ushindani hebu jaribu kuapply mwaka huu ukimaliza shule uone joto ya Jiwe iliyomo ngoma ikipigwa ingia ucheze

Ukiona chuo CHOCHOTE cha AFYA narudia teana chuo CHOCHOTE cha AFYA kumbuka maneno yanhu kina COMPETITION tena kubwa na ya ajab HUTAAMIN endelea kujipa moyo kua havina ushindani waliopo kwenye vyuo hivo vyote wanaelewa nazungumza nini
 
Wewe bipa shaka ni kidato cha sita hivi kwwli una sema vyuo kama Kairuki na St Joseph havina ushindani hebu jaribu kuapply mwaka huu ukimaliza shule uone joto ya Jiwe iliyomo ngoma ikipigwa ingia ucheze

Ukiona chuo CHOCHOTE cha AFYA narudia teana chuo CHOCHOTE cha AFYA kumbuka maneno yanhu kina COMPETITION tena kubwa na ya ajab HUTAAMIN endelea kujipa moyo kua havina ushindani waliopo kwenye vyuo hivo vyote wanaelewa nazungumza nini
Huyu jamaa mi nimemshangaa sana..mwaka juzi kuna dogo aliomba kiu roundi ya pili na alikuwa na 11 na alitemwa..
 
TCU ilipandisha cut off points kwa ajili ya kujiunga na kozi za afya kwa digrii na kuwa 8 yaani C, C na D badala ya D, D na S. Kwa maoni yangu sioni ulazima wa kutaka MTU apate D ya physics kama kigezo cha kusoma kozi ya afya. Masomo ya msingi kwa kozi za afya ni chemistry na biology. Kwa hiyo wangerudisha kigezo cha awali kuhusu physics cha kuhitajika kupata angalau S ya physics. Kwa hiyo kigezo kiwe C, C na S point 6.5. Madaktari bingwa tulionao Leo wengi walipata S ya physics na hilo halikuwa kikwazo kwao kusomea udaktari au pharmacy. Hiki kigezo cha sasa kinaharibu sana ndoto za watu na baadhi ya vyuo vinaweza kuwa vinakosa wanafunzi!!! Chonde chonde tazameni upya vigezo hivi. Watoto ndo mwezi ujao wanaanza mitihani yao! Ni vizuri kuweka vigezo kabla hawajafanya mitihani ya kidato cha sita.

Hapana sikubaliani nawe tena nadhani hata hiyo alama C wamewapendelea sana na badala yake wanatakiwa wachukuwe wenye alama B au A tu. Utanisamehe Mkuu nadhani kama kuna Kozi ambazo zinatakiwa zipatikane Watu Vipanga / Werevu kabisa basi ni hiyo ya Udaktari na masuala mazima ya Afya kwa Mwanadamu. Naungana na nakubaliana na TCU 100%.
 
Huyu jamaa mi nimemshangaa sana..mwaka juzi kuna dogo aliomba kiu roundi ya pili na alikuwa na 11 na alitemwa..
Atakua ni form six tena anataja Kairuki haina COMPETION NIMECHEKA SANA

Achilia mbali vyuo vya Dar es Salaam mpaka AJUCO ni tabu tu bonge la competition Hataamin

Hii iwaendee PCB wote wanaodhani watapata vyuo sijui Kampala au St Joseph hata kama kwenu pesa ipo ya kutosha jiandae kisaikolojia kuna competition ya kutosha sana, hata hivyo vyuo mnaviona sijui vibaya VINAFURIKA HUTAAMIN
 
Atakua ni form six tena anataja Kairuki haina COMPETION NIMECHEKA SANA

Achilia mbali vyuo vya Dar es Salaam mpaka AJUCO ni tabu tu bonge la competition Hataamin

Hii iwaendee PCB wote wanaodhani watapata vyuo sijui Kampala au St Joseph hata kama kwenu pesa ipo ya kutosha jiandae kisaikolojia kuna competition ya kutosha sana, hata hivyo vyuo mnaviona sijui vibaya VINAFURIKA HUTAAMIN
ushindani upo vyuo vya umma lakini kwa vyuo vya binafsi hakuna ushindani kivile.....cha msingi uwe na vigezo vya kusoma hiyo kozi hata kama ni division two ya 10
 
Ukweli ni uwa tuna vyuo vichache vya Medicine na bahati mbaya kwa ajili ya QC (quality control) vingi mwaka jana havikuruhusiwa kudahili. Kwa upande mwingine wengi wanaochukua PCB wanataka kusomea MD, Pharmacy etc. Hii husababisha competition kuwa kubwa kupita kiasi na vijana wengi kukosa nafasi. Sijui mwaka huu mambo yatakuwa vipi.

Kitu ambacho sina hakika ni wale wenye diploma wakitaka kwenda kuchukua MD etc, je GPA ya 3.5 inawatendea haki? Sina data kwa mfano ni asilimia ngapi ya wanao dahiliwa ni watu wa diploma?
 
Ukweli ni uwa tuna vyuo vichache vya Medicine na bahati mbaya kwa ajili ya QC (quality control) vingi mwaka jana havikuruhusiwa kudahili. Kwa upande mwingine wengi wanaochukua PCB wanataka kusomea MD, Pharmacy etc. Hii husababisha competition kuwa kubwa kupita kiasi na vijana wengi kukosa nafasi. Sijui mwaka huu mambo yatakuwa vipi.

Kitu ambacho sina hakika ni wale wenye diploma wakitaka kwenda kuchukua MD etc, je GPA ya 3.5 inawatendea haki? Sina data kwa mfano ni asilimia ngapi ya wanao dahiliwa ni watu wa diploma?
Wengi sanaaa kuliko Hawa wa advance
 
ushindani upo vyuo vya umma lakini kwa vyuo vya binafsi hakuna ushindani kivile.....cha msingi uwe na vigezo vya kusoma hiyo kozi hata kama ni division two ya 10
Tunachoomba kigezo cha mpaka uwe na D ya physics kirekebishwe. Hii ni kuweka kikwazo kisicho cha lazima! Kigezo cha physics kirudi kuwa S au hata E basi! MTU hawezi kushindwa kozi ya udaktari eti kwa sababu alikuwa na E ya physics! Vinginevyo madaktari wote walio kazini waliokuwa na E au S ya physics waondolewe kwenye ajira!!! Maprofesa wengi wanaofundisha MD walipata S au D ya A-level!!! Agizo la kuwaondoa likitoka utaona vumbi litakavyotimka! Sema hatuwezi kutaja majina hapa lakini wapo wengi tu! Kwa nini TCU imeamua kuwabania watoto! Acha MTOTO akose chuo kwa kushindwa ushindani na siyo kwa kumwekea vikwazo visivyo na mantiki!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Chief,uhitaji unatofautiana sana zamani na sasa.
Kama vijana wengi wanafaulu na mpaka wanakosa chuo kuna ulazima gani wa TCU kushusha vigezo? Na hao ambao hawakupata kozi za afya,ulazima upo wapi wa wao kuchukua kozi za afya?!
Usichoelewa ni kuwa hata mtu akapata nafasi nje ambako watamkubali kusoma MD pamoja na kuwa na E ya Physics, ili maadamu ana C za bios na kemia lakini cheti chake hakitatambulika nchini kwetu maana watadai hakuwa na sifa ya kusoma MD. Kumbuka vyeti vyote vya nje lazima vipate baraka ya TCU ili vikubalike nchini! Tunaposema washushe hatuangalii kusoma TZ peke yake!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Usichoelewa ni kuwa hata mtu akapata nafasi nje ambako watamkubali kusoma MD pamoja na kuwa na E ya Physics, ili maadamu ana C za bios na kemia lakini cheti chake hakitatambulika nchini kwetu maana watadai hakuwa na sifa ya kusoma MD. Kumbuka vyeti vyote vya nje lazima vipate baraka ya TCU ili vikubalike nchini! Tunaposema washushe hatuangalii kusoma TZ peke yake!

Sent using Jamii Forums mobile app
Asante sana kwa kusaidia ufafanuzi!
 
Usichoelewa ni kuwa hata mtu akapata nafasi nje ambako watamkubali kusoma MD pamoja na kuwa na E ya Physics, ili maadamu ana C za bios na kemia lakini cheti chake hakitatambulika nchini kwetu maana watadai hakuwa na sifa ya kusoma MD. Kumbuka vyeti vyote vya nje lazima vipate baraka ya TCU ili vikubalike nchini! Tunaposema washushe hatuangalii kusoma TZ peke yake!

Sent using Jamii Forums mobile app

Sijawasikia TCU wakiliongelea hili. Watu watakuja kushikana mashati hapa (LoL). Walitakiwa waliweke wazi kama ni hivyo ili kila mhusika alijue.
 
Back
Top Bottom