Ole Sendeka aeleza siri ya ukimya wake bungeni

tang'ana

JF-Expert Member
Apr 3, 2015
11,809
15,055
Mirerani. Mbunge wa Jimbo la Simanjiro Mkoani Manyara, Christopher Ole Sendeka amesema kwa sasa hazungumzi sana Bungeni kutokana na utendaji kazi mzuri wa Serikali ya awamu ya sita ya Rais Samia Suluhu Hassan.

Ole Sendeka akizungumza na wadau wa madini ya Tanzanite, mji mdogo wa Mirerani, amesema amekuwa kimya Bungeni kwani hivi sasa viongozi wa serikali wanaofanyia kazi changamoto za wananchi.

Amesema kipindi chake cha miaka 10 ya ubunge wake alikuwa anazungumza mara nyingi Bungeni kwa sababu baadhi ya mambo hayakuwa sawa.

Amesema kila changamoto ya wapiga kura wake inapojitokeza viongozi wa serikali wanaifanyia kazi hivyo anakosa sababu ya kuzungumza.

"Wadau wa madini walipokuwa wanapekuliwa bila staha nilifikisha kilio hicho Serikali na sasa hivi wanapekuliwa kwa staha," amesema Ole Sendeka.

Amesema akiwa na jambo mkuu wa mkoa wa Manyara, Charles Makongoro Nyerere anatatua, likihusu Simanjiro, mkuu wa wilaya hiyo Dk Suleiman Serera anafanyia kazi hivyo hana sababu ya kulalamika.
 
Hakika Mh.Ole Sendeka ni mzalendo na shuhuda wa ukweli...😍

Unapokuwa na serikali SIKIVU basi tarajia matokeo hayo ya ukimya wa mh.Ole Sendeka.....

#AwamuYaSitaNaMuendelezoWaKazikuntu

#SiempreJMT
#NchiKwanza
 
Kabisa Mkuu ndiyo sababu hawa wahuni wanahaha sasa na huyo Simbachawene anatafuta namna ya kudhibiti Twitter Space na hasa ya Maria ambayo kwa nyakati mbali mbali imevuta wasikilizaji hadi karibu 7,000 kwa siku moja.

Hakuna jinsi ya kuzuia hii kitu ila nina wasiwasi mkubwa na usalama wa Maria hasa ukitilia maanani wasiojulikana wamemaliza likizo zao na wamerudi rasmi kazini.

Bunge la Space ni bora mara 100 kuliko hili la wahuni
 
Wewe ongea tu kwa sauti Kikwete anakusikia au hujui ndo kashika usukani? enzi zake mlijipatia umaarufu kupinga ufisadi.
 
6 Reactions
Reply
Back
Top Bottom