Inside10
JF-Expert Member
- May 20, 2011
- 33,783
- 40,565
Emmanuel Arnold Okwi hii leo ametangaza kustaafu kuitumikia timu ya Taifa ya Uganda akiwa na umri wa miaka 32 baada ya kuhudumu kwa miaka 16 na 'The Cranes'.
Nyota huyo wa zamani wa Simba na Yanga ambaye kwa sasa anaitumikia Kiyovu SC ya Rwanda, ameitumikia The Cranes tangu 2009 akiifungia magoli 28 kwenye mechi 95 huku akihudumu nafasi ya unahodha kuanzia mwaka 2021 akichukua kitambaa hicho kutoka kwa Golikipa Denis Onyango.
Pia soma Okwi atimiza miaka 32, ni mmoja ya wachezaji bora wa kigeni kuwahi kucheza ligi kuu nchini
Kupitia taarifa yake rasmi aliyoipakia kwenye mitandao ya kijamii, Okwi amesema “Kuiwakilisha nchi yangu kwenye jukwaa la kimataifa imekuwa ndoto yangu ambayo imetimia kila mara iliacha hisia maalum, na kuwa nahodha wa timu yetu ilikuwa fursa na heshima kubwa.”
Je, una mkumbuka Okwi kwa tukio gani Timu ya Taifa?
source east africa tv