Oktoba tunatiki!!

Setfree

JF-Expert Member
Joined
Dec 25, 2024
Posts
5,527
Reaction score
7,121
Marko 12:17
"...Mpeni Kaisari yaliyo ya Kaisari, na yaliyo ya Mungu mpeni Mungu."

Mimi hata kabla ya Oktoba, yaliyo ya Mungu ninayatiki ✅
  1. Yesu Kristo ni Mwokozi wa ulimwengu ✅
  2. Damu ya Yesu inasafisha dhambi zote ✅
  3. Wokovu haupatikani kwa matendo, bali kwa neema ✅
  4. Biblia ni Neno la Mungu, ni tamu kuliko asali ✅
  5. Msalaba ni msingi wa upatanisho kati yetu na Mungu ✅
  6. Roho Mtakatifu ni Msaidizi na Mwalimu wetu ✅
  7. Kanisa ni mwili wa Kristo duniani ✅
  8. Jina la Yesu lina nguvu ya kufukuza mapepo ✅
  9. Yesu atakuja tena kwa utukufu ✅
  10. Wanaomwamini Yesu wataurithi uzima wa milele ✅
 
Kuwa makini na kila unachoposti, hasa kuhusianisha Yesu na siasa za hawa wezi na waporaji wa mali za umma na hususani kipindi hiki ambacho kuna fukuto kubwa sana la watu kutaka mabadiliko. Mwombe Roho Mtakatifu akujalie hekima na busara. Lengo linaweza kuwa zuri lakini uwasilishaji wake ndio ukawa na kasoro.
 
Wewe ni Low minded sana.
 
Kuwa makini ni kutiki kwamba
Yesu Kristo ni Mwokozi wa ulimwengu ✅

Uwe makini na comments zako, Ibilisi asikutumie kuzuia Injili
 
Kwa waliokua wanakupenda kwasababu ya neno la Mungu Leo umewafukuza rasmi Kwa kuonyesha upande wako
Kama watanikimbia kwa sababu niko upande wa Mungu, hakuna shida, mimi ntaendelea tu kutiki
Yesu Kristo ni Mwokozi wa ulimwengu ✅
 
Kabisa hii ni vita ya HAKI.
 
Kuwa makini ni kutiki kwamba
Yesu Kristo ni Mwokozi wa ulimwengu ✅

Uwe makini na comments zako, Ibiisi asikutumie kuzuia Injili
Sijawahi kutumiwa na Ibilisi kuzuia Injili. Kichwa cha habari ulichotumia kina ukakasi ndugu. Hadi hapo bado hujagundua kasoro hiyo? Pamoja na kuhubiri Injili, tumia busara na hekima juu ya maneno unayotumia.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…