Ofisi ya rais yatumika kupora mali za wananchi

Ofisi ya rais yatumika kupora mali za wananchi

BASIASI

JF-Expert Member
Joined
Sep 20, 2010
Posts
9,732
Reaction score
5,010
ofisi ya rais Kikwete yatumika kupora kiwanja:

Nimeiweka kwa uchungu jamani kuona sasa wenye pesa bila aibu wanaenda kupora mali za wazee hata wenye miaka 88 bila aibu shame on them

Kiufupi wizara ya ardhi ilihalilisha kiwanja no 170a cha Mwanaidi Alawi wa Kipawa Dar es salaam kwa bwn Abdul Khan mfanyabiashara wa kiasia...baadae ilipotoka magazetini wizara hiyo hiyo ikaona aibu chini ya katibu wake alieshurutishwa kustaafu Patrick Rutabanzibwa wakaondoa kibali cha Khan na kurudishwa umiliki wake kwa mh rais.

Wakati zoezi likiendelea wahusika wakaiongozwa na bi Mwanaiidi wakafungua kesi mahakamani wakashinda .Waliposhinda akarudishiwa uhalali wa kiwanja bibi Mwanaidi,baadae Khan mfanyabiashara akaenda wizara ya ardhi kulalamika kikarudishwa kwa ofisi ya rais ambae mmiliki wake ni rais wetu Kikwete.

Sasa basi ilipoenda mh. Chilligati wakati huo waziri akaondoa uhalalisho kwa rais na kumrudishia bi Mwanaidi haki yake ya umiliki kama ilivoyelezwa na Machi 25,2011 na msajili wa hati na kutolewa gazeti la serikali toleo 12 namba 38101.

Vichekesho vya wizara ya ardhi vs ofisi ya rais

31july mwaka huu bibie akienda kulipia kodi ya kiwanja akakuta kiwanja chake kimerejeshwa kwa ofisi ya rais tangu Apr 2013
bila ya yeye kuambiwa

Kwa mliosoma unachoona hapa kuna kamchezo kachafu kanataka kufanyika kumdhulumu bibi huyu kati ya ofisi ya rais na wizara ya ardhi ikiongozwa na mama Tibaijuka....

Hata hivyo taarifa zilizotufikia zinasema bibie Mwanaidi akiwa na wakili wake waliekea ofisi ya rais kutaka kujua mmiliki wa kiwanja ni nani na yeye kama rais anarudishiwa kumiliki kiwanja kama nani??Ikasema rais wetu kipenzi Jakaya Mrisho Kikwete ajawahi kusaini kufuta umiliki wa bi Mwanaidi hata siku moja.

wito:
Najua hii sio tu kwa Mwanaidi na ndugu zako wengi wamepigwa kule ardhi wakiongozwa na katibu asiyehamishika mpaka maombi ya Mungu kuamua kumng'oa mwenywe.

Ndugu zanguni lazima tuwe wazi haki yako usiiachie hata maramoja,kuna uchafu mwingi ardhi..

Nilijua mh. Tibaijuka utakuwa mwisho wa matatizo lakini inavyoonekana mtandao wao ni hatari kuliko wa madawa yakulevya kama uamini stay tune.

Mh Tibaijuka tunaitaji maneno yako kwa huyu bibi.
 
Mengine tutamuonea Mh. Rais maana jinsi ninavyoliona hili JK hangefanya kabisa ni aibu mno kukaba hata penati. Hapa ni kwamba wasaidizi ambao ni too corrupt wamafanya upumbavu huo. (Samahani Mod kwa lugha hiyo kali, limeniuma sana) Kumdhulumu nadhani huyu ni Mjane, ni dhambi kubwa sana kwani hata katika dini maandiko yanasema "...dini ya kweli ni kuwafariji wajane, watoto yatima ..." Sasa inapotokea dhuluma juu yao kwa kweli nisamehewe kwa kauli iliyopo ndani ya mabano. Ni mategemeo ya wengi kwamba Mh. Rais JK jinsi ninavyomfahamu kwa hili ataingilia kati na kuwawajibisha wale walioendesha "mahakama zao binafsi"
 
Msiichague CCM, CCm si chama cha kutetea wanyonge, CCM ipo kwa ajili ya kutetea maslah ya wafanyabiashara wakubwa wasio lipa kodi na wanaovuna wasipopanda.
CCM ni adui namba moja wa MTANZANIA.
CCM kuwepo madarakani ni kifo kwa mlala hoi
 
Ni wengi tulidhulimiwa,hata sisi tuna shamba letu lilipimwa viwanja lakini hatukupata viwanja vya kutufidia.Nimehangaika sana bila msaada wowote.
 
Mama Tibaijuka ana taarifa kweli maana huwa namuamini angalau kwenye viongozi wachache wa CCM waliobakia
 
Tanzania Daima ni gazeti la UDAKU...
Kwani magazeti ya udaku hayaandiki ukweli? Kwa mtazamo wangu huu ni uonevu mkubwa sana. Huyu katibu mkuu si ndiyo hivi majuzi waziri mmoja ameiambia kamati ya kina Lembeli kuwa kamuwekea dhamana mhalifu aliyevunja sheria kwa kujenga nyumba kinyume na taratibu?
 
Mama nae siasa nyingi, mimi nina hati za viwanja pale block 22 kibada kuanzia muda cha kushangaza kunajamaa mwingine amepewa hati palepale plot 100/101 na wizara. mama anajua lakini nae hakuna kitu... usalama wa taifa na ofisi ya mkaguzi mkuu wa serikali fanyieni kazi swala hili watu wanashindwa kuendeleza kwa migogoro isiyo na tija miaka!

Mungu ibariki Tanzania.
 
mama nae siasa nyingi, mimi nina hati za viwanja pale block 22 kibada kuanzia muda cha kushangaza kunajamaa mwingine amepewa hati palepale plot 100/101 na wizara. Mama anajua lakini nae hakuna kitu... Usalama wa taifa na ofisi ya mkaguzi mkuu wa serikali fanyieni kazi swala hili watu wanashindwa kuendeleza kwa migogoro isiyo na tija miaka!

Mungu ibariki tanzania.

mkuu mama tiba kawekwa pale kwa ajili ya uchaguzi subiri mwakani baadhi ya viwanja utasikia vimerudishwa kwa wenyewe nahis hata huyu bibi wanataka ajikalie mpaka mwakani waproove kama atakuwa tayari kuipigia ccm ama la wamrudishie lakini hili la kusema kiwanja kimepelekwa kwa ofisi ya raisi ofisi ya rais inamilikije kiwanja??sawa na kama mzee wangu jk akusaini nani ameshikilia hiko kiwanja kwa muda huu naamini anaisoma hii mada na ajaenda zimbabwe basi amsaidie huyu bibi kabla mungu ajampenda zaidi akuna kitu mbaya kama kufa unauchungu ....
 
Mengine tutamuonea Mh. Rais maana jinsi ninavyoliona hili JK hangefanya kabisa ni aibu mno kukaba hata penati. Hapa ni kwamba wasaidizi ambao ni too corrupt wamafanya upumbavu huo. (Samahani Mod kwa lugha hiyo kali, limeniuma sana) Kumdhulumu nadhani huyu ni Mjane, ni dhambi kubwa sana kwani hata katika dini maandiko yanasema "...dini ya kweli ni kuwafariji wajane, watoto yatima ..." Sasa inapotokea dhuluma juu yao kwa kweli nisamehewe kwa kauli iliyopo ndani ya mabano. Ni mategemeo ya wengi kwamba Mh. Rais JK jinsi ninavyomfahamu kwa hili ataingilia kati na kuwawajibisha wale walioendesha "mahakama zao binafsi"

Bubu Msemahovyo, Kutokana na ulemavu wako wa ububu,sidhani kama umekosea kusema baadhi ya wasaidizi wa mheshimiwa rais Kikwete ni corrupt na kwa hiyo wanafanya upumbavu kwa kutotenda haki panapostahili kufanya hivyo!

Rushwa ni adui wa haki. Wanaohusika wampe haki yake bibi Mwanaidi. Wale wote walioshirikiana na Abdul Khan katika mpango wa kumpora bibi Mwanaidi kiwanja chake kwa kutumia jina na ofisi ya mheshimiwa rais wachukuliwe hatua kali kwa kitendo cha kumdhalilisha mheshimiwa rais!
 
Niulize swali la kizushi, huyo bibi hicho kiwanja alimilikishwa lini? Na je ameishakiendeleza hicho kiwanja tangia alipomilikishwa? Mimi si mwanasheria lakini nafahamu kwamba ukimilikishwa kiwanja na usikiendeleze, basi unaweza kufutiwa umiliki. Kabla sijachangia zaidi, naomba mleta mada ajibu maswali yangu.

Tiba
 
Back
Top Bottom