Ofisi ya Rais itoe tamko juu ya Mawaziri ambao Ubunge wao umekwisha na wanaendelea na Uwaziri

aligawee

JF-Expert Member
Jan 3, 2015
507
105
Kwenu wanajamvi naomba kufahamishwa kama ni sahihi baada ya Bunge kuvunjwa rasmi Mawaziri wanaweza kuendelea na Uwaziri. Ninavyofahamu kwa kuwa Uwaziri wa sasa ni mpaka uwe Mbunge na tayari Bunge limevunjwa hivyo hakuna Mbunge tena, vivyo hivyo hakuna Mawaziri tena.

Lakini tunachoshuhudia ni Mawaziri kutekeleza Uwaziri kinyume na Katiba ambayo naamini inamtaja Katibu mkuu wa Wizara katika kipindi hiki kuelekea uchaguzi. Kama wanaendelea na kama wamepata ridhaa ya Rais basi Rais amevunja Katiba na nadhani wanataaluma wa sheria nchini wataliangalia hili kwani kwa kiasi fulani kutekeleza kwao uwaziri kunawapa fursa ya kukipigia kampeni chama chao.
 
kwenu wanajamvi naomba kufahamishwa kama ni sahihi baada ya bunge kuvunjwa rasmi mawaziri wanaweza kuendelea na uwaziri. Ninavyofahamu kwa kuwa uwaziri wa sasa ni mpaka uwe mbunge na tayari bunge limevunjwa hivyo hakuna mbunge tena, vivyo hivyo hakuna mawaziri tena.

Lakini tunachoshuhudia ni mawaziri kutekeleza uwaziri kinyume na katiba ambayo naamini inamtaja katibu mkuu wa wizara katika kipindi hiki kuelekea uchaguzi. Kama wanaendelea na kama wamepata ridhaa ya rais basi rais amevunja katiba na nadhani wanataaluma wa sheria nchini wataliangalia hili kwani kwa kiasi fulani kutekeleza kwao uwaziri kunawapa fursa ya kukipigia kampeni chama chao.

wewe utakuwa ukawa tu maana asilimia 90 huwa hawafikiri. Nani alikwambia serikali imevunjwa?
 
wewe utakuwa ukawa tu maana asilimia 90 huwa hawafikiri. Nani alikwambia serikali imevunjwa?

hapana kuna logic hapa kwenye hoja yake.mawaziri hawana tena legitimacy sababu kilichowapeleka uwaziri(ubunge)hawana tena.
 
Tafuta katiba ya Jamhuri ya Muungano kifungu cha ukomo wa Mawaziri kitakupa majibu. Kwa kukusaidia kinasema Waziri hukoma nafasi yake akifa au akiapishwa mwingine.
 
uko sahihi kabisa mimi niko ukawa. lakini august 15 gazeti la serikali lilitangaza kuvunjwa rasmi kwa bunge.
wewe utakuwa ukawa tu maana asilimia 90 huwa hawafikiri. Nani alikwambia serikali imevunjwa?
 
Tanzania tunaongoza kwa kujadili vitu ambavyo vimeshaandikwa.Nakushauri ukasome kama ulivyoelekezwa.
 
Back
Top Bottom