Ofisi ya CCM yachomwa moto Mafia

Ofisi ya CCM yachomwa moto Mafia

real G

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2013
Posts
5,227
Reaction score
5,302
Watu wasiojulikana wameichoma moto ofisi ya Chama cha Mapinduzi tawi la Mshonzini iliyopo wilayani Mafia mkoani Pwani na kuteketeza mali mbalimbali za chama hicho.

Akithibitisha tukio hilo, Katibu wa CCM wilayani Mafia Mohammed Dhikiri amesema tukio hilo limetokea usiku wa kuamkia leo Alhamisi Julai 13.

Dhikiri amesema moto huo umeteketeza kabisa ofisi hiyo pamoja na samani za ndani.

Amesema bado haijajulikana sababu za ofisi hiyo kuchomwa moto kwa kuwa wakati tukio linatokea hakukuwepo na viashiria vyovyote vya vurugu miongoni mwa wanachama.

Amesema bado halijafahamika ni nani aliyehusika na tukio hilo na kueleza kuwa wameliachia Jeshi la Polisi kuendelea na uchunguzi zaidi dhidi ya tukio hilo.


Chanzo: Mwananchi
 
Watu wasiojulikana wameichoma moto ofisi ya Chama cha Mapinduzi tawi la Mshonzini iliyopo wilayani Mafia mkoani Pwani na kuteketeza mali mbalimbali za chama hicho.

Akithibitisha tukio hilo, Katibu wa CCM wilayani Mafia Mohammed Dhikiri amesema tukio hilo limetokea usiku wa kuamkia leo Alhamisi Julai 13.

Dhikiri amesema moto huo umeteketeza kabisa ofisi hiyo pamoja na samani za ndani.

Amesema bado haijajulikana sababu za ofisi hiyo kuchomwa moto kwa kuwa wakati tukio linatokea hakukuwepo na viashiria vyovyote vya vurugu miongoni mwa wanachama.

Amesema bado halijafahamika ni nani aliyehusika na tukio hilo na kueleza kuwa wameliachia Jeshi la Polisi kuendelea na uchunguzi zaidi dhidi ya tukio hilo.


Chanzo: Mwananchi
Haya yanaelekea ni yale yale ya Kibiti na Mkuranga!Ngoja tusubiri cinema.
 
Again...ni gazeti la Mwananchi ndiye wa kwanza kuripoti!
 
Nani amechoma akamatwe awekwe ndani

Mkuu wa wilaya amesemaje mpaka sasa
 
Ni vile tu AK47 hazipo mtaani vinginevyo kwa chuki Na dhuluma ya kisiasa hii kingewaka mapema

Sent from my VF685 using JamiiForums mobile app
 
Jamani kunani huko wangekua wanaonekana tungewa omba radhi

Sent from my TECNO-L8 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom