Mpaka siku Rubani feki aangushe ndege ndo tutaelewa ukubwa wa hili tatizo Tanzania.
Kova ni msanii, anakimbia kwenye media anasema vitu vya ajabu ajabu tu , mara ngapi watu wanalalama hawa watu wanaojiita Usalama wako wengi sana hakuna hatua leo huu ugomvi wa mtu binafsi wanauleta na kuupa coverage kuuubwaa..
Huyu kaka alishAkuwa dereva tume ya kurekebisha sheria au nimemfananisha?
jamb toka jana yupo uraian..
Hii age kati ya 40 na 42 ukifuatilia matukio mengi ya kushangaza utakuta wenye umri huo walianza vituko muda mrefu sasa mf.Mwaka 1990 kuna kijana mmoja akiwa kidato cha pili alichukua fomu za kuwania urais kupitia CCM(enzi hizo chama kimoja tu cha siasa)ambaye sasa kama yupo atakuwa na miaka 42.
Mwaka 1988 kuna vijana kutoka Zanzibar waliteka ndege ingawa hawakufanikiwa kutimiza lengo lao la kupelekwa Uingereza ambapo walijitoa ati wakafungwe huko then baadae waendelee na maisha yao!Hivi sasa mmoja wao ana umri wa miaka 42!Kuna jamaa mmoja namfahamu kwa jina moja Kolimba(alijipachika tu jina hili) kama yupo hai sasa atakuwa na miaka 42 aliwahi kwenda kuripoti shule moja Misungwi kama mwl mkuu muda mfupi tu baada ya kuacha masomo Bwiru boys akiwa kidato cha pili(jamaa alikuwa genius kwani alikuwa akifanya vyema sana masomo)Jamaa alipokelewa ila kabla hawajamshitukia akawapora akatoroka.
Huyu nae umri 43!Sijui vipi yule trafiki feki?unaweza kuna ni umri ni kati ya hiyo niliyotaja!
Sent from my BlackBerry 9220 using JamiiForums
Tunao wengi sana hapa Dar wanaojita ni TISS, huwa nawacheka sana nikikutana nao vilingeni!Duh hapa ni research inahitajika.Hizi dondoo ni hints!!!
Kova ni msanii, anakimbia kwenye media anasema vitu vya ajabu ajabu tu , mara ngapi watu wanalalama hawa watu wanaojiita Usalama wako wengi sana hakuna hatua leo huu ugomvi wa mtu binafsi wanauleta na kuupa coverage kuuubwaa..
Chanzo cha yote Haya inasemekana ni mgogoro wa kiwanja Huku Ukonga ambao ulipelekea kuibua Songombingo hatimae likatinga polisi na kuibua yote Haya tunayoyasikia sasa
Mkuu... hebu dadavua kidogo. Ugomvi wa mtu binafsi kivipi??
- Mtuhumiwa ana ugomvi na Kova??
- Mtuhumiwa ana ugomvi na Wanausalama???
- Ama mtuhumiwa ana ugomvi na nani???
Watu wanaojiita Usalama ni wengi sana na hilo ni kosa, idara yenyewe ya Usalama imeshindwa kudhibiti hii hali, manake kweli kujiita usalama ni kosa kisheria lakini la pili ni kwamba unajiita ili iweje, sasa hilo kosa la pili manake sasa ukijiita usalama unatapeli au unajipatia favour flani, nachojua huu ulikua ugomvi wa kiwanja na ndio sababu huyu jamaa akakamatwa sasa kusema ni au sio usalama ni kazi ya polisi kudhibitisha, je kama amekua usalama kwann wao hawakumjua siku zote mpaka juzi kiwanja kilipoleta gogoro na kwamba hicho kiwanja kinahusisha ndugu wa mkuu wa polisi ilala, kumbe walikua wanajua ila sasa ni mchezo wa kutegeshana ukiingia anga zao wanakuliza wakati hujaingia anga wanajua ww ni mharfu ila wanakaa kimya maajabu ya Tanganyika hii!!
Katika hali isiyo ya kawaida,watu waliojipachika vyeo vya maafisa usalama wa taifa na wengine kutumia majina ya viongozi wa serikali wameunda mtandao hatari ambao hutumia majina na vyeo hivyo kutapali watu kwa kuwaingiza katika viunga vya Ikulu na baadae kuwatekeleza baada ya kuwaahadaa kuwa watapata ajira Ikulu.
Mtu mmoja aliejitambulusha kama Baraka Tiabaijuka na kudai kuwa ni mtoto wa waziri Tibaijuka ndie aliehusika na moja ya matukio hayo.Imeelezwa katika utapeli hup wa kuwapatia ajira Ikulu,watu wanaoathirika zaidi ni kina mama na wanafunzi wa vyuo vikuu.Wanafunzi wsliotapeliwa ambao walichangishwa kiasi cha sh 450,000-500,0000 ni kutoka vyuo vya CBE,IFM ,chuo kikuu cha Mlimani na Tumain.
Kinachofanywa na matapeli hao ni kuwaingiza katika viunga vya Ikulu na kisha kuwatelekeza sehemu ya mapokezi huku wakiwa teyari wameshalipa viwango hivyo vya fedha kwa ahadi ya kupatiwia kazi Ikulu.
Hata hivyo,waziri Tibaikuka amekana kumfahamu mtu anaejiita Baraka Tibaijuka.
CHANZO:MTANZANIA JUMAPILI
Picha ya mtuhumiwa aliyejifanya Afisa usalama.
JESHI la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, limemkamata Alquine Claud (42) mkazi wa Yombo Buza wilayani Temeke kwa tuhuma za kujifanya ofisa Usalama wa Taifa.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Kamanda wa Kanda hiyo, Kamishna Suleiman Kova alisema kuwa baada ya mtuhumiwa kuhojiwa alikiri kuwa hakuwa mfanyakazi wa Idara ya Usalama wa Taifa.
Kova alisema kuwa siku ya tukio mtuhumiwa alikamatwa na vielelezo mbalimbali ikiwemo bastola aina browning yenye namba A.956188-CZ83 ikiwa na risasi 12 ndani ya magazine.
Kwamba alipopekuliwa nyumbani kwake alikutwa na bastola nyingine aina ya Maknov yenye namba BA4799 ikiwa na risasi 19 pamoja na kitabu cha mmiliki silaha hiyo chenye namba CAR 0007168 na jina la P.1827 LT COL Mohamedi Ambari, kitambulisho cha JWTZ No.7001-E. 1075.
Mbali na vielelezo hivyo, mtuhumiwa alikutwa na nyaraka mbalimbali zikiwemo za Ikulu pamoja na mihuri ya Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP) na vyeti bandia vya shule.
Tanzania Daima
Kova ni msanii, anakimbia kwenye media anasema vitu vya ajabu ajabu tu , mara ngapi watu wanalalama hawa watu wanaojiita Usalama wako wengi sana hakuna hatua leo huu ugomvi wa mtu binafsi wanauleta na kuupa coverage kuuubwaa..
Huyu kaka (Masubo) anajulikana kila sehemu hapa mjini!pia ana vitu kibao havieleweki kabisa!!alishawahi kuwa jeshini kama daktari miaka ya zamani!alishakuwa dereva wa mama Salmini Zbar!leo ni dereva huko serikalini!kuna vitu havieleweki hapa!sina hakika kama ameshapanda kizimbani!jamaa yuko kitaaa!!Kova msanii!amezidiwa kete!