kailakarama
Member
- Aug 30, 2014
- 73
- 30
Chama cha demokrasia na maendeleo(chadema),kimetuhumiwakusuka mkakati wa kukuvutia chama cha ACT-Tanzania kwa kutumia baadhi ya wanachama wa chama hicho.
Taarifa ambazo zimelifikia gazeti hili Dar-es-salaam jana,mmoja wa viongozi wa chama hicho,alisema kuwa wanahisi chadema wanacheza mchezo mchafu wa kuhakikisha ACT-Tanzania inaingia kwenye mgogoro.
Chanzo hicho (jina tunalo),kilisema kwa hali ilivyo kuna kila dalili ya Chadema kuhusika ikiwa ni pamoja na kuandaa mkutano uliofanywa juzi na baadhi ya wanachama wa ACT-Tanzania ambao wanajitambulisha kwenye vyombo vya habari kama waasisi wa chama hicho.
Taarifa zaidi zilieleza kuwa taarifa waliyonayo ni kwamba mmoja wa maofisa wa habari wa chadema,ndiyo alihusika kutoa taarifa kwa vyombo vya habari kwa vinatakiwa kwenda kwenye mkutano huo wakiamini baada ya habari kutoka watakuwa wamefanikiwa kutimiza malengo yao.
Hata hivyo,chanzo hicho hakikuwa tayari kutaji jina la ofisa anayetuhumiwa kuhusika katika mkakati wa kuichafua ACT-Tanzania.
Alipotafutwa kwa njia ya simu, ofisa habari wa chadema, Tumaini Makene ili kuzungumzia tuhuma hizo, alisema hawezi kuzizungumzia maana yupo mkoani ambapo alitaka kufahamu ni nani alitoa madai hayo.
Chanzo: Gazeti la Jambo Leo tarehe 13/11/2014.
Taarifa ambazo zimelifikia gazeti hili Dar-es-salaam jana,mmoja wa viongozi wa chama hicho,alisema kuwa wanahisi chadema wanacheza mchezo mchafu wa kuhakikisha ACT-Tanzania inaingia kwenye mgogoro.
Chanzo hicho (jina tunalo),kilisema kwa hali ilivyo kuna kila dalili ya Chadema kuhusika ikiwa ni pamoja na kuandaa mkutano uliofanywa juzi na baadhi ya wanachama wa ACT-Tanzania ambao wanajitambulisha kwenye vyombo vya habari kama waasisi wa chama hicho.
Taarifa zaidi zilieleza kuwa taarifa waliyonayo ni kwamba mmoja wa maofisa wa habari wa chadema,ndiyo alihusika kutoa taarifa kwa vyombo vya habari kwa vinatakiwa kwenda kwenye mkutano huo wakiamini baada ya habari kutoka watakuwa wamefanikiwa kutimiza malengo yao.
Hata hivyo,chanzo hicho hakikuwa tayari kutaji jina la ofisa anayetuhumiwa kuhusika katika mkakati wa kuichafua ACT-Tanzania.
Alipotafutwa kwa njia ya simu, ofisa habari wa chadema, Tumaini Makene ili kuzungumzia tuhuma hizo, alisema hawezi kuzizungumzia maana yupo mkoani ambapo alitaka kufahamu ni nani alitoa madai hayo.
Chanzo: Gazeti la Jambo Leo tarehe 13/11/2014.