Official: Dirisha la usajili lafunguliwa rasmi England

brave one

JF-Expert Member
Feb 5, 2013
4,876
7,366
Rasmi Sasa Leo tarehe 16 May dirisha ya usajili limefunguliwa kwa ajili ya msimu ujao.Dirisha litafungwa rasmi tarehe 8 mwezi wa 8 wiki moja kabla ya Ligi kuanza.
England wamebadilisha utaratibu was usajili kupishana na ule wa Ulaya unaonza July 1 mpaka September 31. England wamebadilisha ili kuondoa mkanganyiko wa usajili kufanyika wakati ligi ikiwa imeanza.
Inst-image-4.jpeg
 
Eintracht Frankfurt striker Luka Jovic has completed a £52.4m (€60m) move to Real Madrid.

- Sky Sports
 
Ole Mr nice guy,

Ole yeye asema nani kama Young..?
Nani kama Jones..?
Nani kama Smalling?
Olle Gunnar uwanja wako baba chukua vifaa msimu ujao tubebe kila kitu ili turudishe heshima
Hiyo miamba mitatu itamvusha mbele.
 
=L'Equipe

-Klabu ya Paris Saint-Germain inajiandaa kumpa mkataba mpya wa muda mrefu mshambuliaji Kylian Mbappe anayehusishwa na Real Madrid.

-Klabu ya Arsenal imeweka mezani ofa ya Pauni Milioni 10.5 kwa ajili ya kuinasa saini ya Beki wa kati ya Gremio Walter Kannemann.

>Hata hivyo Beki huyo wa Kiargentina mwenye umri wa miaka 28 ameripotiwa kuwindwa vikali ya baadhi ya timu za Italia ikiwepo Inter Milan pamoja na Sampdoria.

=Daily Mirror

-Klabu ya Manchester United imetuma maombi ya kutaka kuinasa saini ya Mshambuliaji wa Bayern Munchen Robert Lewandowski.

-Klabu ya Atletico Madrid inaangalia uwezekano wa kumsajili mshambuliaji wa Arsenal Alexandre Lacazette kwa ajili ya kuchukua mahala pale Antoine Griezmann.

-Klabu ya Manchester United inajiandaa kuweka mezani ofa ya Pauni Milioni 40 kwa ajili ya kuinasa saini ya mshambuliaji wa Lyon Moussa Dembele.

=Daily Mail

-Liverpool, Tottenham pamoja na West Ham United wanapigana vikumbo kuwania saini ya Mshambuliaji wa Celta Vigo Maxi Gomez mwenye umri wa miaka 22.

>Katika mkataba wa Maxi Gomez kuna kifungu kinachomruhu kuondoka klabu hapo endapo klabu inayomtaka itaweka mezani ofa ya Pauni Milioni 43 (release clause).

=The Independent

-Philippe Coutinho pamoja na Ivan Rakitic ni miongoni mwa wachezaji 10 wanaotarajiwa kuuza na klabu ya Barcelona kwa ajili ya kupata fedha za kutosha ili kuwasaini Antoine Griezmann pamoja na Matthijs de Ligt.

=The Times

-Klabu ya Paris Saint-Germain imeonesha nia ya kutaka kumsajili Mshambuliaji wa Liverpool na Brazil Roberto Firmino.

=The Sun

-Klabu ya Manchester United inakaribia kumsajili winga wa Swansea City Daniel James mwenye umri wa miaka 21 kwa kiasi cha Pauni Milioni 10.

=Daily Telegraph

-Klabu ya Juventus inakabiriwa na ushindani kutoka Inter Milan katika mbio za kutaka kuinasa saini ya Mshambuliaji wa Manchester United Alexis Sanches.

=Daily Star

-Klabu ya Real Madrid imejitosa katika mbio za kuwania saini ya winga wa Lille Nicolas Pepe ambaye anawindwa vikali na Manchester United.
 
Back
Top Bottom