October to remember

October to remember

Mshana Jr

Platinum Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
360,082
Reaction score
828,874
Ni wangapi waliiangalia sinema ya Sometimes in April? Tuombe sana Mungu na sisi tusije tukaja kutengeneza sinema ya October to remember ..! Na kama ikitokea hivyo basi iwe kwa heri na si kwa kumbukumbu za kutisha na kutia simanzi.

Leo ni tarehe moja mwezi wa kumi.. Mwezi uliongia kwenye historia za mataifa ya Tanganyika na Zanzibar kwa kuondokewa na mmoja wa waasisi wa Taifa la Tanzania. Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere Mchonga meno hapo mnamo tar 14.10.

October hii inaweza kuwa tofauti kabisa na October nyingine zote na siku ya tar 14 ya kumbukizi ya kifo cha Mwalimu Nyerere inaweza kutumiwa na wananchi kufanya jambo kubwa sana.

Maono mbalimbali, tabiri, mijadala mbalimbali na hali halisi vinaonesha kwamba kuna mwamko mkubwa sana wa kutaka mabadiliko chanya ya kisiasa kati ya wananchi wa mataifa yote mawili ya Tanganyika na Zanzibar.

Mwamko huu pamoja na mengine yote ni hitaji la nyakati..! Mojawapo ya vitu ambavyo huwa havizuiliki basi ni mahitaji ya nyakati.. Wakati ukitimia lililopangwa kuwa HUWA!

Mahitaji ya nyakati ni sawa na maji yanayosafiri hasa baada ya mvua kubwa kunya! Kamwe usijaribu kuyazuia haya maji kwakuwa
Mosi hutaweza.. I mean hutafanikiwa!
Pili kama utaweza kuyazuia basi ni kwa muda tuu.

Tatu yatakuletea madhara makubwa sana utakapojaribu kuyazuia yasipite yatakapo ama yaingie mahali na yakose pa kutokea
Ndani ya mwaka kuna miezi 12 lakini kiroho kila mwezi una tafsiri yake! Kwa miezi inayoishia na na ember hiyo ni miezi ya mabadiliko ama pando la mabadiliko!

September iliyoishia jana tuliiona wote ilivyokuwa imepanda na kuchochea mbegu ya mabadiliko.. Hiyo mbegu itamea October na November unaweza kuja kuwa mwezi mpya utakaobeba mengi mapya yawe mazuri ama mabaya.

All in all hatuombei tuje kutengeneza sinema ya Sometimes in November!

Bado tuna muda wa kutafakari, kutengeneza na kubadili maamuzi kwa amani kwa maelewano na kwa ushirikiano! Bado tuna nafasi ya kujifunza historia na kwa waliotutangulia.. Hatuhitaji kuwa na haraka kwakuwa hata hizo haraka tulizozitumia huko nyuma hapo awali hazikutufikisha popote!

Tukiamua kuwa na tafakuri kuu Tukaacha kiburi
Tukaacha ego
Tukaacha craving
Tukaacha kujiona sisi ni bora kuliko wao
Tukaacha yote mabaya yanayouseta uumbaji wa Mwenyezi Mungu, Oktober hii itapita salama nasi tutaondoka kwa heshima na historia itatuweka mahali pazuri pa kukumbukwa vema!
1759004011342.jpg
 
Nilishangaa sana Jana nilipokaa na watu wakijijini Hadi na wale wenye baiskeli wakisema hawamtaki huyu mama.
Tena usukumani wanasema ni dharau kubwa sana Nchi kuongozwa na mwanamke!!

Wanasema hawawezi kumpigia kura mwanamke hivyo Bora washinde wanacheza bao!!

Hii ni kijijini ndanindani huko
 
Nilishangaa sana Jana nilipokaa na watu wakijijini Hadi na wale wenye baiskeli wakisema hawamtaki huyu mama.
Tena usukumani wanasema ni dharau kubwa sana Nchi kuongozwa na mwanamke!!

Wanasema hawawezi kumpigia kura mwanamke hivyo Bora washinde wanacheza bao!!

Hii ni kijijini ndanindani huko
Ndiye amiri jeshi mkubwa
1759003984418.jpg
 
Ally Bongo wa Gabon alitangazwa kuwa mshindi wa kura za uchaguzi wa mizengwe.
Wazalendo wa nchi yao wakakataa upuuzi huo!

Sasa hapa kwetu Tanzania; nchi hii kweli imekosa kabisa wazalendo wa kukomesha ujambazi huu?
 
Ni wangapi waliingalia sinema ya Sometimes in April? Tuombe sana Mungu na sisi tusije tukaja kutengeneza sinema ya October to remember ..! Na kama ikitokea hivyo basi iwe kwa heri na si kwa kumbukumbu za kutisha na kutia simanzi

Leo ni tarehe moja mwezi wa kumi.. Mwezi uliongia kwenye historia za mataifa ya Tanganyika na Zanzibar kwa kuondokewa na mmoja wa waasisi wa Taifa la Tanzania. Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere Mchonga meno hapo mnamo tar 14.10.

October hii inaweza kuwa tofauti kabisa na october nyingine zote na siku ya tar 14 ya kumbukizi ya kifo cha Mwalimu Nyerere inaweza kutumiwa na wananchi kufanya jambo kubwa sana

Maono mbalimbali, tabiri, mijadala mbalimbali na hali halisi vinaonesha kwamba kuna mwamko mkubwa sana wa kutaka mabadiliko chanya ya kisiasa kati ya wananchi wa mataifa yote mawili ya Tanganyika na Zanzibar

Mwamko huu pamoja na mengine yote ni hitaji la nyakati..! Mojawapo ya vitu ambavyo huwa havizuiliki basi ni mahitaji ya nyakati.. Wakati ukitimia lililopangwa kuwa HUWA!

Mahitaji ya nyakati ni sawa na maji yanayosafiri hasa baada ya mvua kubwa kunya! Kamwe usijaribu kuyazuia haya maji kwakuwa
Mosi hutaweza.. I mean hutafanikiwa!
Pili kama utaweza kuyazuia basi ni kwa muda tuu
Tatu yatakuletea madhara makubwa sana utakapojaribu kuyazuia yasipite yatakapo ama yaingie mahali na yakose pa kutokea
Ndani ya mwaka kuna miezi 12 lakini kiroho kila mwezi una tafsiri yake! Kwa miezi inayoishia na na ember hiyo ni miezi ya mabadiliko ama pando la mabadiliko!
September iliyoishia jana tuliiona wote ilivyokuwa imepanda na kuchochea mbegu ya mabadiliko.. Hiyo mbegu itamea October na November unaweza kuja kuwa mwezi mpya utakaobeba mengi mapya yawe mazuri ama mabaya
All in all hatuombei tuje kutengeneza sinema ya Sometimes in November!

Bado tuna muda wa kutafakari, kutengeneza na kubadili maamuzi kwa amani kwa maelewano na kwa ushirikiano! Bado tuna nafasi ya kujifunza historia na kwa waliotutangulia.. Hatuhitaji kuwa na haraka kwakuwa hata hizo haraka tulizozitumia huko nyuma hapo awali hazikutufikisha popote!

Tukiamua kuwa na tafakuri kuu Tukaacha kiburi
Tukaacha ego
Tukaacha craving
Tukaacha kujiona sisi ni bora kuliko wao
Tukaacha yote mabaya yanayouseta uumbaji wa Mwenyezi Mungu, Oktober hii itapita salama nasi tutaondoka kwa heshima na historia itatuweka mahali pazuri pa kukumbukwa vema!View attachment 3481546
Hakuna kitu, hizo ni hisia zako tu
 
Huu ndo Mwezi unaenda kubadilisha siasa za Tanzania.
Nitaisikitikia sana nchi yetu hii kama haya yataachwa yaendelee kama yalivyo pangwa na waovu hawa!

Ni vigumu sana kuamini kuwa kweli hii ni Tanzania kunakofanyika upuuzi wa ajabu sana huu.

Mwanamke asiye kuwa na sifa zozote za uongozi; akili kichwani kiduchi kabisa; tena toka nchi jirani, ambaye hata asili yake haijulikani vizuri; anaamua kulazimisha kuwatawala watu zaidi ya milioni 60!

Katika utawala wa miaka minne, kila uchafu umeonekana; tena anafanya kama hakuna anayeweza kuhoji chochote; na watu wakihoji, anajiita chura kiziwi asisikie kelele za waTanzania wakililia raslimali zao zinazosombwa.

Huyu mtu sasa analazimisha kwa nguvu abaki madarakani ili afanye uharibifu mkubwa zaidi!
Nchi nzima hii, hakuna wa kumzuia?

Hapana. Mimi namtabilia mwisho wake. na asipokuwa mwangalifu atapoteza kila kitu hadi uhai wake.
 
Maono mbalimbali, tabiri, mijadala mbalimbali na hali halisi vinaonesha kwamba kuna mwamko mkubwa sana wa kutaka mabadiliko chanya ya kisiasa kati ya wananchi wa mataifa yote mawili ya Tanganyika na Zanzibar
"---mabadiliko chanya ya kisiasa kati ya wananchi wa mataifa yote mawwili ya Tanganyika na Zanzibar"?

Mstari huu mwandishi hakuutendea haki hata kidogo, na kwa kufanya hivyo, andiko lake limekosa umakini stahiki.

Hata swala la Oktoba 14 nalo mwandishi katumia hisia tu; na matokeo yake yanaweza kuwachanganya wananchi ambao wamejiandaa kufanya kazi nzuri Oktoba 29.

Tuamue moja, Oktoba 14, au Oktoba 29? Tusiwachanganye waTanzania.
 
Kwa dalili zilizopo huku mtaani,hiyo October wananchi wengi watalala Tu nyumbani,hawaendi kuandamana wala kupiga Kura!
Usitegemee hata siku moja kuwapeleka waTanzania wote barabarani.
Lakini wakibaki nyumbani bila kwenda vituoni, watakuwa wametoa mchango muhimu sana katika kuzuia uchaguzi.

Watakaojitokeza kuandamana, hata wakiwa milioni tano nchi nzima, hilo ni tukio kubwa sana katika nchi yoyote ile.

Ni wachache huleta mabadiliko; hasa yanayohitaji kujitoa mhanga kupigania haki.

Hata kwenye vita, kuna wapiganaji, na kuna raia wanaoshirikiana na askari wapambanaji.
 
Back
Top Bottom