OBD Diagnosis 101

Styvo254

JF-Expert Member
Aug 5, 2015
246
226
Hamjambo Wote WanaJamii,
Kama wengi wenu mjuavyo, magari na mitambo ya kisasa ina husisha mfumo wa diagnosis katika sehemu mbali mbali. Wamiliki wa magari na madereva bila shaka sio wageni na taa ya Check Engine au MIL (Malfunction Indicator Lamp). Lakini, swali muhimu ni wangapi wanaelewa mfumo wa OBD una maana gani kwenye chombo?
Engine na mifumo mbali mbali ya kisasa ina husisha umeme wa digital au elektroniki katika uangalizi(monitor), udhibiti(control) na utekelezi(actuate) wa utenda kazi wake. Hii ni kwa usalama, ubora na wepesi wa gari au mtambo. Mtandao huu wa umeme pia umewezesha mawasiliano kati ya ECU au 'bongo' za mifumo tofauti kwenye chombo kw mfn breki (ABS) na engine na transmission. Mawasiliano haya yanawezesha usawazishaji wa tukio mara moja bila dereva kuhusika kama vile gari linapoteleza kwa barbara telezi, breki uhusika kupunguza na kusawazisha mwendo wa kila gurudumu ili kudhibiti mwendo NA mwelekeo wa chombo, wakati huo huo gear pia inashushwa ili kuyapa magurudumu uzito kwenye barabara.
Sijasahau mada wapendwa, ila ni kuieleza poa zaidi.
Mfumo wa On Board Diagnosis ni aina ya mtandao, rekodi na mawasiliano maalum ya kiufundi kwa zile bongo za mifumo ya chombo. Hii yahusisha kusoma matatizo(faults) yaliopo kwenye mfumo, kuangalia(monitor) utendakazi wa mfumo na pia kulazimisha utendakazi kwa ajili ya ukaguzi(test) na utekelezi(actuation); hii ya mwisho ni kwa vifaa kwenye mfumo ambazo uhusika na usalama, udhibiti maalum au utendaji kazi unaohitaji taarifa(data) maalum kwenye mfumo na kwa hivyo ni lazima iwekwe au inukuuiwe na mfumo wa kiufundi.
Kutoka na hayo maelezo hadi sasa waweza kuona kua mfumo wa OBD una nukuu matatizo yanapotokea, lakini sio rahisi hivyo! Lazima bongo lihesabu ni mara ngapi tatizo linatokea kw kila chombo kitumiwavyo (Key Cycle). Na pia kama tatizo linahusika na utumizi au mazingira ya mda huo. Ni kwamba sio kila tatizo litawasha MIL, kusema kutowaka kwa MIL sio kutokua na tatizo.
Watengenezaji vyombo hivi walikusudia tukio la Service litahusisha Diagnosis ya chombo ili kukagua hali ya mfumo kwa wakati mzuri - kabla ya kuharibika! Na pia gari linapotoa taarifa tata likaguliwe kwa kina katika mazingira take ya kazi na matumizi; hii ni wazi kwa engine za electronic injection diesel kama vile D4D(Toyota) na DI(Mitsubishi).
Kinacho nishinda hadi sasa ni mafundi wenzangu wameshachukia teknolojia hii ya kurahisisha kazi na kuiogopa wakidai ni kuwapotezea ajira, Upumbafu Mtupu! Ukichelewa usidai umetengwa - ni lazima fundi ajiongeze kitaaluma kwa kua ulimwengu unajoingeza kila kuchao.
Shukran sana na Karibuni sana!
 
Hamjambo Wote WanaJamii,
Kama wengi wenu mjuavyo, magari na mitambo ya kisasa ina husisha mfumo wa diagnosis katika sehemu mbali mbali. Wamiliki wa magari na madereva bila shaka sio wageni na taa ya Check Engine au MIL (Malfunction Indicator Lamp). Lakini, swali muhimu ni wangapi wanaelewa mfumo wa OBD una maana gani kwenye chombo?
Engine na mifumo mbali mbali ya kisasa ina husisha umeme wa digital au elektroniki katika uangalizi(monitor), udhibiti(control) na utekelezi(actuate) wa utenda kazi wake. Hii ni kwa usalama, ubora na wepesi wa gari au mtambo. Mtandao huu wa umeme pia umewezesha mawasiliano kati ya ECU au 'bongo' za mifumo tofauti kwenye chombo kw mfn breki (ABS) na engine na transmission. Mawasiliano haya yanawezesha usawazishaji wa tukio mara moja bila dereva kuhusika kama vile gari linapoteleza kwa barbara telezi, breki uhusika kupunguza na kusawazisha mwendo wa kila gurudumu ili kudhibiti mwendo NA mwelekeo wa chombo, wakati huo huo gear pia inashushwa ili kuyapa magurudumu uzito kwenye barabara.
Sijasahau mada wapendwa, ila ni kuieleza poa zaidi.
Mfumo wa On Board Diagnosis ni aina ya mtandao, rekodi na mawasiliano maalum ya kiufundi kwa zile bongo za mifumo ya chombo. Hii yahusisha kusoma matatizo(faults) yaliopo kwenye mfumo, kuangalia(monitor) utendakazi wa mfumo na pia kulazimisha utendakazi kwa ajili ya ukaguzi(test) na utekelezi(actuation); hii ya mwisho ni kwa vifaa kwenye mfumo ambazo uhusika na usalama, udhibiti maalum au utendaji kazi unaohitaji taarifa(data) maalum kwenye mfumo na kwa hivyo ni lazima iwekwe au inukuuiwe na mfumo wa kiufundi.
Kutoka na hayo maelezo hadi sasa waweza kuona kua mfumo wa OBD una nukuu matatizo yanapotokea, lakini sio rahisi hivyo! Lazima bongo lihesabu ni mara ngapi tatizo linatokea kw kila chombo kitumiwavyo (Key Cycle). Na pia kama tatizo linahusika na utumizi au mazingira ya mda huo. Ni kwamba sio kila tatizo litawasha MIL, kusema kutowaka kwa MIL sio kutokua na tatizo.
Watengenezaji vyombo hivi walikusudia tukio la Service litahusisha Diagnosis ya chombo ili kukagua hali ya mfumo kwa wakati mzuri - kabla ya kuharibika! Na pia gari linapotoa taarifa tata likaguliwe kwa kina katika mazingira take ya kazi na matumizi; hii ni wazi kwa engine za electronic injection diesel kama vile D4D(Toyota) na DI(Mitsubishi).
Kinacho nishinda hadi sasa ni mafundi wenzangu wameshachukia teknolojia hii ya kurahisisha kazi na kuiogopa wakidai ni kuwapotezea ajira, Upumbafu Mtupu! Ukichelewa usidai umetengwa - ni lazima fundi ajiongeze kitaaluma kwa kua ulimwengu unajoingeza kila kuchao.
Shukran sana na Karibuni sana!
Hivyo vifaa vipo vya aina ngapi na bei zake zikoje

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Asante kw swali lako SQ100,
Vifaa/mitambo/mashine za diagnosis ziko aina nyingi. Pengine njia rahisi ya kuhoji hili swali ni kupanga/orodhesha mashine hivi:
1. OEM
Safu hii inajumlisha mashine zilizobuniwa, zinazotumika au zilizotambuliwa na watengeneza chombo (Original Equipment Manufacturer). Kw. mfn. Nissan hutumia mfumo uitwao CONSULT ambao sasa uko kwenye muundo(version) ya tatu, na labda ya nne tayari imetoka tunavyojadili hapa; Toyota uwa na mfumo wake uitwao TECHSTREAM; VW/Audi wako na VAG COM na wengine pia wana mifumo yao maalum.
Katika safu hii tunapata mashine na mifumo inayotumika na mawakala na kwa hivyo hua na uwezo mkubwa wa kuwasiliana na mitambo kw chombo.

2. Diagnostic Interface
Hii ni safu ya mifumo ambayo inatumia vifaa maalum kuwezesha tarakilishi kutumika katika shughuli hii ya diagnosis. Hii mifumo hutumia software ambayo imebuniwa na watengeneza vyombo au yenye nguvu mama vile. Mawasiliano huwa ya hali ya juu.

3. SCANNER/CODE READER
Hii ni mifumo yenye uwezo mdogo wa mawasiliano na hutumika sana sana kusoma matatizo kwenye mfumo yaani kusoma kodi zilizoko kwenye mfumo.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Naomba kuuliza je nikitaka kununua hicho kifaa ni aina gani nzuri kupita nyengine?
 
Naomba kuuliza je nikitaka kununua hicho kifaa ni aina gani nzuri kupita nyengine?
Itategemea na gari unazolenga kuunda au ulio na uzoefu nazo. Kama ni Toyota kuna Techstream software na cable yake. Hii inakuwezesha kuwasiliana na Toyota, Lexus na Scion.
 
Kama nataka kununua ya kusoma gari za aina nyingi ipi ni nzuri
Pesa yako ndio itakupa kitu bora zaidi mkuu.

Kuna mshine za mpaka milioni 30 na ushee huko..

Hizi za milion 5 kushuka chini huwa haziwezi fanya kazi zote kwa ubora ule ule .

Harafu kuna aina ya magonjwa au tatizo hutatuliwa na mashine maalum tuu.

Mfano range rover kuna aina ya shida ni lazima uwr na T4 tuu ndio itaweza kutatua ,au benz ni lazima uwe na mb star.

Hivyo hapo ni mtihani kidogo
 
Pesa yako ndio itakupa kitu bora zaidi mkuu.

Kuna mshine za mpaka milioni 30 na ushee huko..

Hizi za milion 5 kushuka chini huwa haziwezi fanya kazi zote kwa ubora ule ule .

Harafu kuna aina ya magonjwa au tatizo hutatuliwa na mashine maalum tuu.

Mfano range rover kuna aina ya shida ni lazima uwr na T4 tuu ndio itaweza kutatua ,au benz ni lazima uwe na mb star.

Hivyo hapo ni mtihani kidogo
Sasa wewe waanzia uzi kisha wautoroka ukishigunduliwa kua tapeli sasa wa mwenyewe ndio waingilia. Hata haya huna we Lege.
 
Back
Top Bottom