Nyumba ina mauzauza

Nyumba ina mauzauza

Habari wakuu
Poleni kwa kazi la kulisongesha mbele taifa na natumaini ni wazima wa afya.

Tatizo langu ni hivi,tuna nyumba yetu maeneo ya mwananyamala ambayo hua tunapangisha.Mwaka 2013 mwezi wa kumi tulipata mpangaji singasinga(wale wahindi wanaovaa vilemba) ambaye alipanga.Sasa mwezi wa nane huu mwishoni alihama na kutuachia nyumba pia alichimba kisima kwaiyo alituachia masimtank pamoja na pump ya maji,sasa mzee wangu alipanga airekebishe nyumba ndo apangishe tena kwaiyo akaniambia mimi niwe nakaa kwenye nyumba hii mpaka hapo atakapotengeneza.

Sasa siku ya kwanza kukaa nilirudi mida kama ya saa 7 usiku,ile nafungua mlango naingia ndani nakutana na baridi la ajabu wakati nilizima kila kitu na hamna ac wala fridge yaani baridi kama kuna ac kuliko nje nilipotoka,nikakausha nikajua handaz tu sasa mimi hua navuta sigara nilikaa sitting room yaani hamna upepo lakini nawasha sigara na njiti haiwaki yaani haiwaki kabisaaaa nikatoka nje ndo ikawaka mi nilipata waswas ila kwakua nilikua nipo high(handaz)nikachukulia poa nikarudi kwa akili yangu niliweka godoro chini pale pale sebuleni ili nilale,usiku ule nalala nkawa naota ndoto za ajabu ajabu,nkawa naota kuna mzee mmoja hapa mtaani(ni mlinzi wa mduka duka ya hapa)et anataka kunif**ra yaani naota mzee anataka kunila tigo,asubuhi nakumbuka niliamka saa 3 nkawa bado nipo kitandani nachezea simu nkasikia jikoni kama kuna mama anaongea huku akipika tena mpaka kelele za vyombo naziskia basi nkaenda jikoni kuangalia nkakuta hamna kitu yaani nkashangaa basi ile kurudi sebuleni nikakuta yule mzee singasinga pamoja na mwenzake simjui wamekaa kene makochi(sijui yalitokea wapi) wanaongea aisee niliishiwa nguvu hata kukimbia nilishindwa naona sababu ya uzito wa kujinyea nikaanza kupiga kelele huku naelekea mlangoni kufika milango nilifunga nkaanza kusoma madua yaani sala zote niliomba na kutoa shahada mpaka kuna jirani akaja na kuniuliza kunani ndo akili ikarudi sawa..

Tukaja sebuleni kuangalia hakuna kitu,nilichoka ndo nikaondoka hapo kumwambia mzee na yeye akanijibu atalishughulikia,wadau mi mpaka sasa iv ile picha ya yule singasinga inanijia nikiwaza yaani sina raha na sijui nifanye nini?

Usiombee yakutokee wadau unaweza ukajua haya mambo hayapo ila yapo nimeamini..

Kuna mtu anaitwa mshanajr ni wakala wa mambo hayo mtafute utapata msaada
 
Last edited by a moderator:
Mshanajr njoo huku utoe msaada tafadhali
 
Kwani huyo singasinga hayo matanki ya maji aliwapa au mlipora bila idhini yake? Asije akawa anawatesa kwa hivyo vitu vyake, maana wenye nyumba mnavisa. Vipi lakini sigara kubwa inapanda? usije ukawa umeitandika inakuletea mawenge. ..
 
Kwani huyo singasinga hayo matanki ya maji aliwapa au mlipora bila idhini yake? Asije akawa anawatesa kwa hivyo vitu vyake, maana wenye nyumba mnavisa. Vipi lakini sigara kubwa inapanda? usije ukawa umeitandika inakuletea mawenge. ..

Alituachia na sigara kubwa haipandi mkuu hata hivo hilo tukio lilitokea asubuhi nipo sober
 
Uoga wako tu mkuu. Kama unataka kuamini chukua vijana wa mabange wakavute usiku kucha humo. Huyo singasinga atalewa moshi na harudi tena.
 
Kwamaelezo yako inawezekana singa singa aliweka makafara mengi sana hapo. Hii story inanikumbusha baba wa rafiki zangu alikuwa meneja wa mashamba ya chai miaka ya 70. Walipewa zile nyumba walizokuwa wanaishi wazungu, basi tukiwa shule alikuwa anahadithia vituko kwenye nyumba, watu wote wanaweza kuwa sittingroom, unakwenda kuoga unasikia mtu anapiga mluzi, au unakuta taulo ambalo ni geni kabisa bafuni.
 
Hahaaa Jf raha lol,mkuu hizi stories za kuliwa kiboga zitakua moja ya Vitu unavyoviogopa,ndio maana vinakujia ukiwa subconscious, na pia kinadharia unaogopa uchawi, both combination imekuwa ukiogofya ndio maana unaota ,hamna lolote mkuu...

Ila umenichekesha handazz lol,Ngoja na mie niende handazz lol,nikajionee mambo, sitaki kusimuliwa hahaaa
 
Hayo ni madhara ya bangi handaz unazovuta mpaka saa saba usiku huku unatamani pesa na makochi ya Singasinga, na huku akili iko kwenye wanakonyea, hayo ndo utakayoendelea kuyaona ukiendelea kutumia handaz
Samahani, Handaz ni nini?
 
Hayo mambo yapo sana mkuu, inafikia hatua unayazoea tu, nakumbuka kipindi cha kwanza Kuhamia kwenye Nyumba yetu mama yangu aliniambia niende peke yangu siku ya kwanza, ila usiku ilikuwa balaa mchanga ulikuwa unamwaga kama mvua, na nimekutana na majanga ya namna hiyo sehemu nyingi tu, inafikia hatua unazoea tu.
Habari wakuu
Poleni kwa kazi la kulisongesha mbele taifa na natumaini ni wazima wa afya.

Tatizo langu ni hivi,tuna nyumba yetu maeneo ya mwananyamala ambayo hua tunapangisha.Mwaka 2013 mwezi wa kumi tulipata mpangaji singasinga(wale wahindi wanaovaa vilemba) ambaye alipanga.Sasa mwezi wa nane huu mwishoni alihama na kutuachia nyumba pia alichimba kisima kwaiyo alituachia masimtank pamoja na pump ya maji,sasa mzee wangu alipanga airekebishe nyumba ndo apangishe tena kwaiyo akaniambia mimi niwe nakaa kwenye nyumba hii mpaka hapo atakapotengeneza.

Sasa siku ya kwanza kukaa nilirudi mida kama ya saa 7 usiku,ile nafungua mlango naingia ndani nakutana na baridi la ajabu wakati nilizima kila kitu na hamna ac wala fridge yaani baridi kama kuna ac kuliko nje nilipotoka,nikakausha nikajua handaz tu sasa mimi hua navuta sigara nilikaa sitting room yaani hamna upepo lakini nawasha sigara na njiti haiwaki yaani haiwaki kabisaaaa nikatoka nje ndo ikawaka mi nilipata waswas ila kwakua nilikua nipo high(handaz)nikachukulia poa nikarudi kwa akili yangu niliweka godoro chini pale pale sebuleni ili nilale,usiku ule nalala nkawa naota ndoto za ajabu ajabu,nkawa naota kuna mzee mmoja hapa mtaani(ni mlinzi wa mduka duka ya hapa)et anataka kunif**ra yaani naota mzee anataka kunila tigo,asubuhi nakumbuka niliamka saa 3 nkawa bado nipo kitandani nachezea simu nkasikia jikoni kama kuna mama anaongea huku akipika tena mpaka kelele za vyombo naziskia basi nkaenda jikoni kuangalia nkakuta hamna kitu yaani nkashangaa basi ile kurudi sebuleni nikakuta yule mzee singasinga pamoja na mwenzake simjui wamekaa kene makochi(sijui yalitokea wapi) wanaongea aisee niliishiwa nguvu hata kukimbia nilishindwa naona sababu ya uzito wa kujinyea nikaanza kupiga kelele huku naelekea mlangoni kufika milango nilifunga nkaanza kusoma madua yaani sala zote niliomba na kutoa shahada mpaka kuna jirani akaja na kuniuliza kunani ndo akili ikarudi sawa..

Tukaja sebuleni kuangalia hakuna kitu,nilichoka ndo nikaondoka hapo kumwambia mzee na yeye akanijibu atalishughulikia,wadau mi mpaka sasa iv ile picha ya yule singasinga inanijia nikiwaza yaani sina raha na sijui nifanye nini?

Usiombee yakutokee wadau unaweza ukajua haya mambo hayapo ila yapo nimeamini..
 
Back
Top Bottom