Ziroseventytwo
JF-Expert Member
- Mar 27, 2011
- 7,976
- 13,626
Tarehe 8/8/ mwaka huu,niliudhuria mkutano mkubwa wa kuzindua vuguvugu la mabadiliko, almaarufu M4C hapa ifakara. Mkutano uliohutubiwa na viongozi wakuu wa chama, mwenyekiti mh Freeman Mbowe, katibu mkuu Dr Wilbrod Slaa na baadhi ya wabunge wa cdm, mmjawapo ni dogo janja, Joshua Nassari. Katika mkutano ule pamoja na mambo mengine, tuliuziwa kadi, pamoja na cd yenye nyimbo za kuhamasisha. Hapa ndo penye hoja. Nilinunua cd si kwa 7bu nazipenda hizo nyimbo,bali kuongeza mapato ya chama. Ukisikiliza nyimbo zote zinamahadhi ya zile za ccm zilizoimbwa na "dubwana" komba wa TOT. Kuanzi ile ya People's power, Slaa kiboko ya mafisadi na nyingine zote mwimbaji ana sauti ya komba. CHADEMA kama chama makini kinatakiwa kutengeneza nyimbo zenye tenzi za kimapinduzi, zinazohamasisha, zitakazn tengeneza chuki dhidi ya utawala mbovu wa ccm. Tumechoka kusikia ladha zilezile za ki-ccm, tuwe macreator na c macopister!