unao uhuru wa kusema utakacho, ninao uhuru wa kufikiri na kuandika nitakacho, na ni tabia yetu wabongo kutopenda kuthamini vya kwetu hivyo siwezi kukushangaa hata kidogo, leo hii Magufuli anasifiwa na waandishi wa habari wa kimataifa lakini hapa hapa nyumbani watu wanakwambia hajafanya kitu! hivyo siwezi kukushangaa unapojaribu kujenga hoja kuwa nyerere hakufanya kitu, ni maoni na ni upeo wako unaokupa jeuri ya kuandika chochote utakacho, kwangu mwalimu nyerere atabakia kuwa mmoja wa viongozi halisi wenye vision waliowahi kutokea barani Afrika. Mataifa mengine yamezama kwenye udini, ukabila na majungu ya ukanda, nyerere alipiga vita uhayawani huo tangu miaka ya 60 mwanzoni, wewe unajaribu kuniambia kuwa hajafanya lolote la maana, jaribu uwe na shukrani japo inaweza isitoke moyoni.