Nyerere alivyoiua timu ya PanAfrican

GT has a point ambayo labda kuieleza inakuwa shida. Nadhani anachojaribu kueleza ni madhara kwa mpira wa Tanzania yaliyotokana na Serikali kuingilia uongozi wa vilabu miaka ya 70-80.Wadau mnakumbuka jinsi Kambarage alivyowafurumua Tambwe Leya (Yanga) na Nabi Camarra(Simba) kwa PI? kwa nini alifanya hivyo wakati hao walimu walikuwa ni wazuri sana waliotengeneza timu nzuri? Mnaukumbuka mtanange mkali wa Yanga(chini ya Tambwe) vs Kwara United na Simba(chini ya Camarra) vs Hearts of Oak?Hizo ndo zilikuwa Simba na Yanga bwana! Nakubaliana na GT ilikuwepo namna,wataalam wa historia tupeni analysis,hivi vilabu havikuporomoka bure ati!!!!!!!!
1.Kuporomoka kwa Simba na Yanga ni kwa sababu zimeshindwa kubadilika kutokana na kubadilika kwa nyakati.Investment zilizofanyika wakati ule kama ni zile ghorofa za msimbazi na ile ya Jangwani almost ni zilezile.No more investments.Na hata hizo zilizopo vilabu vinashindwa kuzitumia na kusubiri fadhila ya kina Dewji na Manji respectively.

2.La Pan Afrika kusambaratishwa kwa sabau za kisiaisa ni debatable.

3.Kuhusu maendeleo ya soka kwa ujumla wake, tunakumbuka ni wakati huo, kama sera ya taifa ya michezo,kila shirika la umma lilikuwa na timu ya soka.

Tunakumbuka Tumbaku,Pamba,Sigara,Pilsner ya Arusha(NDOVU),Pilsner ya DSM,Mwadui Shinyanga,RTC Kigoma,RTC Mwanza,RTC Kagera kuzitaja chache.

Sera ile ilipanuka mpaka kwenye mashule.Michezo mashuleni ilitiliwa mkazo.Tumepata kuwa na wachezaji wazuri ambao wametoka kwenye mashule.

Michezo ilikuwa kila mahala.

Kama si michezo, wewe unapenda dansi, basi kulikuwa na bendi mfano polisi,bima n.k

Nyerere alifanya sehemu yake ambayo mpaka kesho aliyofanya yanaonekana hata kama mtajaribu kuyafuta.

Tatizo ni kwamba hamwezi kufuta aliyofanya kwasababu ALIYAANDIKA KWA WINO siyo penseli.ZAIDI MTACHAFUA KARATASI.

Msihangaike kufuta hizo kurasa za Mwalimu, tatizo karatasi zetu kama taifa ni chache mno,tunaweza kukosa pa kuandika.

MNACHAFUA DAFTARI LA TAIFA,SIO LENU HILO watoto wenu watasoma nini?
 
Pan Africa Walikuwa Mabingwa 1982 sio 1983 Rekebisha Hapo Na kwa Kuongezea Wao ndio mabingwa wa awali wa iliokuwa LIGI KUU YA MUUNGANO, msimu huo wakiitwa mataji mawili Ubingwa wa bara na wa Muungano Wakisaaidiwa saana na uongozi Chini ya Marehemu Alhaji Mangara Tabu Mangara,Shiraz Shariff wacahezaji Mahiri adolph Rishard,Peter Tino(aliewaua Yanga)Abdalah Burhan,Ali Katolila,John Faya,Gordian Mapango,Jaffar Abdulrahman,Salum Carlos mwinyimkuu,Idd Msaka(Ali Yusuph)Ibrahim Kiswabi,Jellah Mtagwa,Leodigar Tenga,Mohammed Yahya Tastao,Doto Ruta Mokilli,Mkweche,Ngulungu nk.

Mkuu umenukumbusha mbali sana.
 
Pan Africa Walikuwa Mabingwa 1982 sio 1983 Rekebisha Hapo Na kwa Kuongezea Wao ndio mabingwa wa awali wa iliokuwa LIGI KUU YA MUUNGANO, msimu huo wakiitwa mataji mawili Ubingwa wa bara na wa Muungano Wakisaaidiwa saana na uongozi Chini ya Marehemu Alhaji Mangara Tabu Mangara,Shiraz Shariff wacahezaji Mahiri adolph Rishard,Peter Tino(aliewaua Yanga)Abdalah Burhan,Ali Katolila,John Faya,Gordian Mapango,Jaffar Abdulrahman,Salum Carlos mwinyimkuu,Idd Msaka(Ali Yusuph)Ibrahim Kiswabi,Jellah Mtagwa,Leodigar Tenga,Mohammed Yahya Tastao,Doto Ruta Mokilli,Mkweche,Ngulungu nk.

Katika wote humu wewe ndio unaijua chini juu Pan African na Pan African iliharibika baada hao watu kupumzika na ikarudi tena juu baada ya watu wanaohusiana na kama hao uliowataja kurudi tena 91 mpaka 94 wakati wa kina Thomas Mashalla kina Abubakar Malima kina Akida makuda then akatokea kiongozi mmoja kutoka Yanga akawatoa viongozi wote ambao walikuwa Pale Pan African miaka ya 91 mpaka 94 kama watu wa Mtaa wa Swahili na wengi walikuwa wazee wa Dar-es-salaam ndio akaja kuiharibu Pan African kwa Uongo wake wa itakuwa timu kama Kampuni ndio timu ya Kwanza kutaka kufanya hivyo Tanzania alivyotua huyo kiongozi ndio mida ile Yanga ipo kwenye mgogoro Mata kufika yeye Pan African walikuwa Viongozi washamleta Shaban Nonda na Kalokola baada kutua tu mjini Dar-es-salaam yule jamaa na viongozi wa Yanga wakaenda kuwachukua kule Pan African hilo wengi hawalijui mkitafuta viongozi wa Pan African ushahidi upo kuhusu Shaban Nonda na Kalokola kama nimepatia huyo Goal kipa jina lake. Kuhusu Nyerere tena hapo imekaa vibaya haileweki ila pia nakumbuka Mzee mangara alikuwa akimsema sana Vibaya Nyerere kwake Ilala kuhusu Yanga sikumsikia kuhusu Pan African. ila tukumbuke sio yote Nyerere kafanya mabaya na sio yote Nyerere kafanya mazuri ni Binadamu.
 
...bila kumsahau Juma Pondamali "Mensah" golini!

Huyo Sasa Ndio Pan African mie nimekuwa Pan African ya 91-94 Bw Mdogo naona viongozi wanavyokwenda mbio mpaka timu inataka kuvunjika kina Mogella kina Nemeth na Iddi Pazi anapisha njia wanaanza kuja Pan African sasa kutoka kwenye Migogoro ile ilioigonga kwa pamoja Simba na Yanga ila Yanga na Pan African ni timu za Waswahili za wenyewe Asilia kuliko Simba Sports Club japo mie ni Mshabiki mkubwa wa Simba Sports Club then ndio hiyo Pan African.
 
Naikumbuka Pan Afrika na Vita ya Zaire ile mechi ilikuwa balaa wengi wenu mlikuwa bado hamjazaliwa.Nakumbuka Sunday Manara aliingia uwanjani wakati timu zinasalimu watazamaji Muhaji Mukki akampisha Sunday Manara dakika za mwanzoni Vita wakapiga goli kupitia mshambuliaji wake hatari Lofombo pasi ilitoka kwa Mayanga.

Sunday Manara akaokota mpira akaanzisha akawapiga chenga akatoa pasi nzuri kwa mdogo wake Kassim Manara akaswazisha mchezo ulimazika Pan 2 Vita 1.

Kuna mechi nyingine naikumbuka Pan na Ibadan ya Nigeria kama sikosei hii mechi Jellah Mtagwa aliumia goti ndiyo ukawa mwanzo mwisho wa kucheza mpira nakumbuka daktari wa Pan alikuwa bonge la mtu mnene,mrefu mweusi alimnyayua Jellah uwanja kama mtoto mdogo sio siku hizi mnaingiza vigari uwanjani.

Mechi zote hizo zilikuwa zikichezwa Arusha.
 
1.Kuporomoka kwa Simba na Yanga ni kwa sababu zimeshindwa kubadilika kutokana na kubadilika kwa nyakati.Investment zilizofanyika wakati ule kama ni zile ghorofa za msimbazi na ile ya Jangwani almost ni zilezile.No more investments.Na hata hizo zilizopo vilabu vinashindwa kuzitumia na kusubiri fadhila ya kina Dewji na Manji respectively.

2.La Pan Afrika kusambaratishwa kwa sabau za kisiaisa ni debatable.

3.Kuhusu maendeleo ya soka kwa ujumla wake, tunakumbuka ni wakati huo, kama sera ya taifa ya michezo,kila shirika la umma lilikuwa na timu ya soka.

Tunakumbuka Tumbaku,Pamba,Sigara,Pilsner ya Arusha(NDOVU),Pilsner ya DSM,Mwadui Shinyanga,RTC Kigoma,RTC Mwanza,RTC Kagera kuzitaja chache.

Sera ile ilipanuka mpaka kwenye mashule.Michezo mashuleni ilitiliwa mkazo.Tumepata kuwa na wachezaji wazuri ambao wametoka kwenye mashule.

Michezo ilikuwa kila mahala.

Kama si michezo, wewe unapenda dansi, basi kulikuwa na bendi mfano polisi,bima n.k

Nyerere alifanya sehemu yake ambayo mpaka kesho aliyofanya yanaonekana hata kama mtajaribu kuyafuta.

Tatizo ni kwamba hamwezi kufuta aliyofanya kwasababu ALIYAANDIKA KWA WINO siyo penseli.ZAIDI MTACHAFUA KARATASI.

Msihangaike kufuta hizo kurasa za Mwalimu, tatizo karatasi zetu kama taifa ni chache mno,tunaweza kukosa pa kuandika.

MNACHAFUA DAFTARI LA TAIFA,SIO LENU HILO watoto wenu watasoma nini?

Respect Bonnie1974....So straight and true..
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom