Nyerere alimlaza Kenyatta baharini!

Nyerere alimlaza Kenyatta baharini!

Salary Slip

Platinum Member
Joined
Apr 3, 2012
Posts
52,209
Reaction score
162,780
Aliekuwa Raisi wa Kenya,hayati mzee Jommo Kenyatta alikuwa akilala baharini ili kumuombea Nyerere atawale Tanganyika.Maelezo hayo yametolewa na mzee Idd Nhende wa Sinza Dar-es-salaam katika mahojiano na gazeti la Tanzania Daima.

Mzee huyo amedai Mzee Kenyatta alikuwa akilala bahari siku tatu kabla ya kutangazwa kwa uhuru wa Tanganyika.Mzee Kenyatta alikuwa anaenda kulaka ufwekeni mbele ya Ikulu na walinzi wake huku wakiwa na soda na kuwaagiza walinzi wake wampige teke ikifika saa sita usiku ili amke na kujitosa baharini.

Kwa maelezo ya mzee huyo wa miaka 81 ni kuwa ilikuwa ikifika saa 2 usiku wote walikuwa wakiekekea ufukweni karibu na lango la Ikulu huku wakiwa wamebeba soda mikeka.Mzee huyo(mlinzi) ameeleza zaidi kuwa alietaka kunywa soda alikunywa na walikuwa wakilala kwenye mikeka hiyo na mzee Kenyatta alikuwa akilala katikati ambapo kulia na kushoto walilala wajukuu zake.Mzee huyu anasema Kenyatta alimwagiza kuwa ikifika saa 6 ampige teke kwenye unyayo ili amke.Baada ya kuamka wote huingia kwenye maji usawa wa magoti na mzee Kenyatta akawa anawamagia maji kwa kutumia usinga wake katika kumuombea Nyerere atawale vizuri Tanganyika.

UFAFANUZI:
Hii habari ni ndefu na katika ukurasa wa 14 haya yalifanyika hapa Tanzania na Kenyatta alikuwa mgeni wa Nyerere wakati huo mzee Kenyatta akiwa kiongozi wa KANU.Mzee Idd Nhende aliteuliwa na Nyerere kuwa mlinzi wa mzee Jomo Kenyatta alipokuwa hapa nchini.

Kwa maelezo zaidi soma gazeti husika online au subiri ununue gazeti hilo kesho.

CHANZO:TANZANIA DAIMA ONLINE

MY TAKE:
Hii habari ni ya ajabu sana na ngumu kuiamini!
 
hapo kwenye red sielewi kabisa. tanganyika ilipata uhuru 1961 wakati kenya mwaka 1963, kwa maelezo yako kenyatta kwa wakati huo alikua kiongozi tena mwenye kulindwa na walinzi tena maeneo ya ikulu(inaonesha tayari alikua anaishi ikulu), nina mashaka na maelezo yako. toa ufafanuzi wa wasiwasi wangu ili nielewe(doubt is a source of knowledge)




Aliekuwa Raisi wa Kenya,hayati mzee Jommo Kenyatta alikuwa akilala baharini ili kumuombea Nyerere atawale Tanganyika.Maelezo hayo yametolewa na mzee Idd Nhende wa Sinza Dar-es-salaam katika mahojiano na gazeti la Tanzania Daima.

Mzee huyo amedai Mzee Kenyatta alikuwa akilala bahari siku tatu kabla ya kutangazwa kwa uhuru wa Tanganyika.Mzee Kenyatta alikuwa anaenda kulaka ufwekeni mbele ya Ikulu na walinzi wake huku wakiwa na soda na kuwaagiza walinzi wake wampige teke ikifika saa sita usiku ili amke na kujitosa baharini.
 
Mkuu, ikulu ipo Nairobi, sasa Kenyata yupo baharini usiku mbele ya ikulu ya wapi tena?

Simulizi feki ! Kenyatta alikuwa ananyea debe lupango ya mwingereza wakati huo, pia tuliwatangulia wakenya kupata uhuru, Sasa wapi na wapi eti alale ikulu ? Kwanza Kenyatta alimdharau sana Mwl,
 
Uongo bila ya Uhariri , ili upate Coverage tengeneza Uongo wowote wa kumsifia Nyerere,Haya basi wengine Waseme Mwanademokrasia wa Kweli japo ndo alifuta Vyama vingi vya siasa 1965, Sheria kandamizi ya Magazeti 1976
 
hapo kwenye red sielewi kabisa. tanganyika ilipata uhuru 1961 wakati kenya mwaka 1963, kwa maelezo yako kenyatta kwa wakati huo alikua kiongozi tena mwenye kulindwa na walinzi tena maeneo ya ikulu(inaonesha tayari alikua anaishi ikulu), nina mashaka na maelezo yako. toa ufafanuzi wa wasiwasi wangu ili nielewe(doubt is a source of knowledge)

Mkuu hii habari ndio hivyo ilivyoripotiwa na hilo gazeti.

Gazeti linapatikana online muda huu au subiri kesho ununue na maelezo ya habari hiyo kwa kirefu ni katika ukurasa wa 14.

Hata hivyo,mods wanaweza wakato hiyo habari nzima kwani iko online katika gazeti(Copy and paste).
 
Simulizi feki ! Kenyatta alikuwa ananyea debe lupango ya mwingereza wakati huo, pia tuliwatangulia wakenya kupata uhuru, Sasa wapi na wapi eti alale ikulu ? Kwanza Kenyatta alimdharau sana Mwl,

Ni mwendelezo wa habari za UDAKU za gazeti la Tanzania Daima...
 
Tanzania Daima wameshindwa kufahamu kuwa Nairobi hakuna bahari.

Mkuu,

Uongo ukizidi inakuwa kama ugonjwa.

Hawa ndio waliandika Rais kaagiza ndege impleke China kutatua kesi ya madawa ya kulevya!!! Uongo wa kitoto kabisa, lakini kuna watu wanalaghaika nao!!!
 
Historia nzuri ya uhuru wa Tangayika. Angalau hii inaminika kuliko official version.
 
Mkuu,

Uongo ukizidi inakuwa kama ugonjwa.

Hawa ndio waliandika Rais kaagiza ndege impleke China kutatua kesi ya madawa ya kulevya!!! Uongo wa kitoto kabisa, lakini kuna watu wanalaghaika nao!!!

Hivi kumbe ile ya China ilikuwa uongo........?......wewe ndio unaniambia leo.......khaaaaa!!!
 
Mkuu,

Uongo ukizidi inakuwa kama ugonjwa.

Hawa ndio waliandika Rais kaagiza ndege impleke China kutatua kesi ya madawa ya kulevya!!! Uongo wa kitoto kabisa, lakini kuna watu wanalaghaika nao!!!

Nina wasiwasi na hii ID kama sio Ridhiwan basi ni njaa kali mmoja....!_
 
Back
Top Bottom