Nyarandu kumuondoa Dr Nzuki?

Nakubaliana na wewe! Mifumo ndio inayotuangusha...

Kwa muda mrefu watendaji wa serikali wamekuwa wakilalamikia mifumo mibovu katika sekta wanazoziongoza, hata wanasiasa (hasa mawaziri) nao wanalalamikia sera mbovu zinazokabili wizara zao ktk kutekeleza wajibu wao. Lakini tujiulize ni nani kaweka na ni nani mwenye jukumu la kubadili hizi mifumo mibovu?

Mkurugenzi mkuu kama mtendaji mkuu hapaswi kulalamikia mfumo mbovu katika Taasisi anayoingoza badala yake kama anaona mfumo ulipo unamkwamisha katika utendaji kazi ni lazima awasilishe mapendekezo yake kwa bodi ya wakurugenzi ili hatimaye mwenyekiti wa bodi awasiliane na waziri husika kuona namna ya kuboresha mfumo wa Taasisi husika. Maboresho mengine yatahitaji kurekebisha sera na sheria husika na hii idhini hutolewa na waziri wa wizara husika. Ni ajabu mtendaji mkuu wa Taasisi au wizara kulalamikia mfumo wakati yeye ndiyo mwenye jukumu la kurekebisha.

Ukiwa mtendaji mkuu hupaswi kulalamika badala yake ni lazima uweke mazingira mazuri ya kutekeleza wajibu wako ikiwa ni pamoja na kuwa mifumo rafiki. Tatizo lilipo Tanzania ni kwamba watendaji wengi pamoja na kuwa na vyeti lukuki lakini kichwani hakuna lolote, wanafanya maamuzi kwa namna ileile ambapo yangefanywa na mtu ambaye hakwenda shule kabisaaaaaa! Tubadilike. Kuwa CEO si kufurahia mafao manono na cheo bali delivery is more important.
 
kutoka twitter page ya Mh. Nyalandu
"Tanzania Tourist Board's CEO, Aloyce Nzuki is relieved of his this duties following the Board's decision today. Search for new CEO underway".

Hizi twiraa....kiboko. Hala hala tusije siku tukasoma kutoka kwa wakuu zaidi...nimevunja baraza la mawaziri....
 
kuna wakati ttb iliongozwa na somebody Senyagwa naye alitoka usa nikajua sasa mambo yatakuwa mswano, sijui jamaa aliishia wapi na huku Alliance air na mkataba na SA md Gideon Kaunda lakini kilichotokea ni maumivi. watendaji wazuri bongo wana haribiwa na wana siasa, yaani unatakiwa kuwa na tentacles kila sehemu kulinda position yako, uwe kama pweza, Polisi una mtu, uwt una mtu, ikulu una mtu, bungeni una watu, kwenye board una mtu , s'wanga au bwagamoyo una mtu (transformer au pete likubwaa) ktk dini yako una mtu
 
Nyalandu ana kampuni ya utalii yeye na mkewe,isije ikawa anatumia fursa ya uwaziri kulipiza kisasi kwa watu walioko wizarani na idara ya utalii kwa ujumla
 
...............Mkuu unayoyazungumzia yana mashiko lakini........ni vema ukatambua...utalii ...ni mpana saana....na kwa Tanzania ..Mungu katujalia si kidogo.....KWA TANZANIA Urban Tourism.....utalii wa kutembelea miji..kuona historia...majengo ya zamani....haujaendelezwa hata kidogo ....na kwa mji kama DSM..majengo yote ya kale wameshawauzia wahindi na waarabu....hizo garden ni maswala ya muda tu na zenyewe zitauzwa......beach tourism...na yenyewe haijaendelezwa kihivyo...ila unazungumzia beach za baadhi ya maeneo ya DSM...na hiyo sio focus kwa sasa....beach tourism zungumzia Zanzibar.....bagamoyo.,.....mafia....Pemba....kwa hayo maeneo niliyoyataja beach zao ni safi na bado zina mvuto kwa wageni wengi..............SWALA LA BEI ZA PACKAGE ZA TANZANIA... hii kwa kiasi kikubwa inachangiwa na NCHI..TAIFA kukosa STRONG NATIONAL CARRIER.....mfano TTB WAKIENDA CHINA kutangaza utalii wa Tanzania hata siku moja hawataweza shindana na KENYA....kwani kuna direct flight zinatoka CHINA TO NAIROBI....how about Tanzania......kama utakuwa unaelewa utajua bei ya package za Tanzania lazima ziwe GALI.....swala la wafanyakazi kilipwa mshahara kidogo..hii ni mfumo wa nchi....tuna sharia amabzo ni butu.....Serena walinunua Muvinpick.....nadhani kama ni mfuatiliaji wa mambo unajua kilichotokea ...na wafanyakazi waliuziwa SERANA kinyume na sharia hakuna aliyezungumza.........kumbuka na elimu ya utalii......tangu mwaka 1967 kulikuwa na chuo cha utalii FORODHANI kwa sasa kinaitwa national college of tourism (NCT)...tangu miaka hiyo kwenye kada ya hotel ni mwaka jana ndio wameanza kutoa diploma ya hotel ( tambua ktk hotel kuna front office, house keeping and laundry...food production...achilia kada nyingine kama kukata ticket....kuongoza watalii ambazo bado wanatoa cheti...sasa kwa hapo unategemea nini......KENYA UTALII COLLEGE ....kipo tangu miaka ya 70 wamebobea kutoa wapishi ma. Manager wa hotel sasa SISI TULIOLALA TUTASHINDANA NAO........hotel nyingi Tanzania mamanager ni WAKENYA KWANI WANAELIMU NA UZOEFU..................tambua TTB kama yenyewe haitaweza kutangaza utalii wa TANGANYIKA KAMA....HAWANA BUDGET YA KUTOSHA.....WAFANYAKAZI WENYE ELIMU NA UZOEFU WA KUTOSHA.......KAMA HATUNA SHIRIKA LA NDELE LA TAIFA......NA ILE POLITICAL WILL .....TUSIMLAUMU Dr. Nzuki tuilaumu system ya nchi na wanasiasa ndio wanaotuangusha
 
..................MKUU mfumo ndio tatizo...na wanasiasa..ndio waharibifu wakubwa .....huyubwana kilichomkwamisha alingilia interest za wakubwa.........alitaka TTB IWE KAMA TCRA..EWURA....namaanisha nini hotel zote ziwe zinasajiliwa na TTB....tour companies....pamoja na travel agencies......tanbua huu ni mradi mkuwa saana ndani ya wizara....walipoliona hilo ndio zengwe zikaanza.... kipindi cha kagasheki....kila kitu kiliandaliwa...n asheria ilikuw aipelekwe bungeni..wizara ndio ilimkwamisha....................TAMBUA HUMSIKII PROF MKOMA WA TCRA ANALALAMIKA KWA SABABAU ANAVYANZO VYAKE VYA MAPATO....AMBAVYO SEREKALI KUU...HAZINA HAWAMUINGILII...Dr.Nzuki alishindwa kwani yeye kama budget yake kwa mwezi ni milioni 50 alikuwa anapewa milioni 5 hapo unategemea nini???????KUMBUKA NI NZUKI HUYU HUYU AIASISI MAONYESHO YA UTALII KAMA YA ........INDABA....... NA YALIKUWA YAANZE MWAKA HUU HAPA DSM BAHATI MBAYA WIZARA HAIKUMPA PESA.....NYALANDU I AM SURE ANAAAAAAYAKE YA SIRI NA GENGE LAKE
 
........hilo sio suluhisho la uozo wa kuto-perform kwa utalii Tanzania......ni incompetence tu.......hii mambo ya kufikiri kwa ku-cut & paste si mambo ya kukumbatiwa sana.......
.................UNGEIJUA TTB Ya Mwenguo........sidhani kama ungeyaongea haya.....kama sio mvivu wa kutafuta habari tafuta performance ya TTB during MWENGUO ERA.....then ulinganishe na ya sasa ukishafanya hivyo ndio u..conclude......kama organisation hukujiuliza hata alikuwa amezungukwa na akina nani???wanaelimu gani.... nana aliwaleta TTB.....walikuwa na influence gani??????......ni bora tuwe tunajipa muda wa kutafaaakari mambo kabla ya kukurupuka
 

Na yeye ajiandae kunyolewa kwani mwosha huoshwa.
 
Nyalandu ana kampuni ya utalii yeye na mkewe,isije ikawa anatumia fursa ya uwaziri kulipiza kisasi kwa watu walioko wizarani na idara ya utalii kwa ujumla

I think this is a very good fact, Lazaro ana conflict of interest ya aina yake na naskia alishawahi kuharrass watu kuipa hiyo kampuni favors in UK

Lakini tukirudi kwenye mada, i think Dr. Nzuki ni wale walioshindwa kupenya kwenye mfumo vizuri na kupigwa panga... even his appointment faced a lot of challenges
 

Nimekusoma mkuu. Nyalandu naye anamakapuni yake ya tours, sijui inajiendeshaji tokea alipokuwa naibu waziri na sasa waziri kamili katika wizara hii.

Sasa inaonekama mifumo katika idara nyingi za serikali ina walakin, ni mbinu gani itumike kutatua tatizo hilo? Je kuna uwezekano wa kuwa na jukwaa la watalaam (professionals) ambalo litakuwa na jukumu ya kutetea professionals wanaokuwa victimised kwa maslahi ya wachache serikalini? Hiyo forum inaweza kuundwa kisheria? Nasema hivi kwa sababu wanasiasa wamekuwa tatizo la kukwamisha utendaji wa wataalamu ktk sekta mbalimbali nchini na umaskini hapa Tanzania kwa kiasi kikubwa unachangiwa na wanasiasa wetu.
 

leave alone akina Peter Mwenguo....kama wewe ni competent....na unatambua hivyo....na kwamba hubembelezi nafasi......ukiona yale unayotaka hayatekelezwi....unajiuzulu......kama unadai Nzuki alizungukwa na watu labda wenye elimu ndogo....au sijui waliletwa na nani au sijui walikuwa na influence gani.....bado hiyo sio sababu ya Nzuki kuto-kuperform......kuna njia nyingi za kushughulikia matatizo kama hayo.........mifano ipo......

Kama Nzuki alikuwa na ajenda na mikakati mizuri ya kuinua Utalii nchini na akakutana na vikwazo......si angeachia ngazi ili kulinda heshima yake? ......... jibu nililolipata baada ya kuona madudu yanaendelea i.e. business as usual......what do you think a common person would say?......"jamaa naye keshakuwa fisadi...au anashirikiana nao!"......na mtu kama mimi nitasema ni incompetence!

....Engineer/Architect wa Wilaya..... kuruhusu mambo kuenda kiholela business as usual matokeo yake tumeyaona....i.e. watu kupoteza maisha......kwa sababu Nzuki ameendeleza business as usual....madudu mengi kwneye Utalii nchini tumeyashuhudia......na kama madudu yale yalifanyika under his watch......na kwamba yalikuw ana nguvu kubwa behind them....then mtu smart unajiuzulu.....
...Ninalisemea hili jambo kwa sababu nina experience nalo..........
 
hii pangua pangua ya wakurugenzi ni vyema ikaleta matunda mazuri kwenye sekta ya utalii
 
.................MKUU sija question uelewa wako wa haya mambo hata kidogo......ninachokizungumzia mie......NIUHALISIA WA MAMBO.............KWA MUJIBU WA SHERIA KAZI ZA TTB NA (ZTC)..KWA ZANZIBAR ni kutangaza utalii wa Tanzania ndani na nje ya Tanzania.......TAMBUA kama ni bidhaa kazi za hawa mabwana ni kutangaza ....already manufactured products.....NA KWA UTALII............NI PACKAGE......INAMAANISHA NINI????????ACCOMODATION...TRANSPORTAION....NA ATTRACTION-kutembelea mbuga....beach...kupanda milima...kuwinda nk),,,,......KAZI TA TTB NI NINBI???? ni kutangaza ni kutangaza bidhaa(package) zilizotengenezwa na TANAPA(kwa Mbuga zao ambazo ni 16)Ngorongoro...na Zanzibar.....wakishazalisha hizi bidhaa wanawapa TTB ndio wakatangaze ndani na nje ya Tanzania.......TTB waanahitaji pesa...taifa linatakiwa liwe na national carrier (Shirika la ndege la taifaa mfano... KQ,,,( KENYA)ET(ETHIOPIA) SA( AFRIKA YA KUSINI......nk).......,,,,,,KWA KUWA NA HIYO MIUONDOMBINU INGEKUWA RAHISI KWA TTB KUTANGAZAUTALII WA TANZANIA KWANI PACKAGE ZA TANGANYHIKA ZISINGEKUWA GALI.........KIKWETE ALITAMBUA KWAMBA......MHESHIMIWA SAAAAAAAAAANA MATAKA MKAPA ALIMFUKUZA PF KUTOKANA NA KUKOSA UADILIFU YEYE AKAMUONA MUADILIFU...NA LULU ,.....AKAMPA AIR TANZANIA SHIRIKA LIKO WAPI,,,,,,,,,,WATANGANYIKA TUKUBALIANE NA UKWELI..........HBUWEZI UKATANGAZA UTALIII KAMA HUNA NATIONAL CARRIER........WATAALAUM,,,,,,,MFUMO MZURI... OTHER WISE utakuwa ubabaishaji tu......n ahakuna jipya
 
.......................MKUU kuwanna jukwaa linawezekana tana kabisa......ila kwa TANGANYIKA NI GUMU SAANA.......kwanini......mifumo yote wamehodhi wanasiasa...........jiuliza mtu kasomwa kilimo...uchumi...sharia.....akilala umeamka kapewa wizara ya UTALIIII.....AMBAYO hajui lolote........kwakuwa... ni waziri anaanza fanya aaanayoyajua mwenyewe.......waduu mna paa kupumulia??????????wanaotungangusha ni wanasiasa...mfano nyalandu anakampuni ya utaliii........aliokaribu nae watamshauri wanayooona hyanafaaa........akikubaliana nao ataayatekeleza.....wafuasi wake watamfuata......ambao maamuzi yamewaumiza wataguna... unaanza mgfogoro chini kwachini......akiondoka waliokuw ahawakubaliani naaanza kufanya michachako...mwisho wasiku.........wizara inakuwa ni ya majungu....kujuana....kulaumiaana,,,,na hakuna kitakachofanyika.........ni kulaumiana tu...hakuna maendeleo..........tunachokilalamikia........TANGANYIKA ni mfumo.......TANGANYIKA MAWAZIRI WASIWE WANASIASA( WAWE WATAALAUM.....KAMA NI MTAALUM AWA UTALIII AONGOZE WIZARA UTALIII AFYA NK......OTHERWISE TUTABAKIA LALAMIKA FOR DA NEXT 50 YRS TO COME
 
Wewe ni mchambuzi mzuri sana! I wish wangekuelewa vizuri!


 
Nilimuona DEVOTA katika usahili wa hii post,na chini chini ni kuwa NYARANDU anataka kumpa office awe MD
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…