Nusu ya bidhaa sokoni 'feki'

Majighu2015

JF-Expert Member
Jul 11, 2015
2,936
3,959
bidhaa+pic.jpg

Imeelezwa kuwa nusu ya bidhaa mbalimbali zinazotumika nchini, zikiwamo dawa za binadamu na vifaa vya umeme, ni bandia.

Profesa Honest Ngowi wa Chuo Kikuu cha Mzumbe amesema hayo yamebainika katika utafiti alioufanya kuhusu tatizo la bidhaa feki nchini.

Akitoa matokeo ya awali ya utafiti huo uliodhaminiwa na Shirikisho la Wenye Viwanda Tanzania (CTI), Profesa Ngowi amesema kutokana na utafiti huo hali ilivyo mbaya kwa maisha ya binadamu.

Katika utafiti huo, aliwahoji watumiaji 250 wa bidhaa mbalimbali na waendeshaji wa kampuni 47 zinazotengeneza bidhaa mbalimbali nchini.

Source:Mwananchi.

Hii nchi kwa kweli ina hali mbaya..Almost kila kitu ni feki tu. Bidhaa feki,wabunge feki,viongozi feki,vyuo feki n.k Tunahitaji maombi mbadala.
 
Huo ndio ukweli,na Tanzania ndio nchi yenye maulana za ovyo sana kuweka Duniani,tbs na mamlaka ya chakula na dawa,zinafanya kazi kwa matukio bila kuwa na mfumo
 
Back
Top Bottom