Mohamed Said
JF-Expert Member
- Nov 2, 2008
- 23,283
- 33,881
Msanii,Nimeona kuna mahala wafuasi wa Chadema wanatumia ile salamu ya Kinazi.
Mungu atusaidie kwa kweli
Hansrashid,Asante kwa kutukumbusha kuhusu historia hiyo. Ila ina mapemgo kidogo. Si Marekani na Uingereza pekee walioianzisha mahakama ya Nuremberg. Tangu uvamizi wa POland ilikuwa dhahiri kwamba serikali ya Ujerumani ililenga makundi mbalimbali ya watu kwa shabaha ya kuwaangamiza (mwanzoni kabisa Wasomi Wapoland waliokamatwa, wengi kuuawa tu). Tangu 1941 (uvamizi wa Urusi) taarifa zilifika kwamba vikosi maalum ya Kijerumani vilianza kuua Wayahudi kwa malakhi. Hadi 1942 taarifa za kwanza zilifika nje kuhusu makambi ya mauti.
"In November 1943, the Soviet Union, the United Kingdom, and the United States published their "Declaration on German Atrocities in Occupied Europe", which gave a "full warning" that, when the Nazis were defeated, the Allies would "pursue them to the uttermost ends of the earth ... so that justice may be done. ... The above declaration is without prejudice to the case of the major war criminals whose offenses have no particular geographical location and who will be punished by a joint decision of the Government of the Allies."[5] This intention by the Allies to dispense justice was reiterated at the Yalta Conference and at Potsdam in 1945.[6] "
Hawakulenga kuua Manazi wote lakini walitafuta wale waliokuwa na wajibu na uongozi.
" In late 1943, during the Dinner Meeting at the Tehran Conference, the Soviet leader, Joseph Stalin, proposed executing 50,000–100,000 German staff officers. US President Franklin D. Roosevelt joked that perhaps 49,000 would do. British Prime Minister Churchill, believing them to be serious, denounced the idea of "the cold-blooded execution of soldiers who fought for their country" and that he would rather be "taken out in the courtyard and shot" himself than partake in any such action.[8] "
Nuremberg penyewe ni 12 tu waliohukumiwa kunyongwa, 7 walitupwa jela, 3 waliachishwa.
Wajerumani wachache waliokamatwa penginepo walihukumiwa pale Poland, Urusi na Chekoslovakia na kunyongwa pale.
Machar,Nini kilimkuta Rudolf Hess aka deputy fuhrer?
Naona chanzo kabisa kilitokea tayari 13 Januari 1942; wawakilishi wa nchi zilizovamiwa na Ujerumani walikutana London (hapa ofisi za serikali za ugenini exile governments ambako wasiasa wachache au viongozi wengine waliokuwa nje ya nchi zao zilizotekwa tayari na Ujerumani) walikutana na kudai kesi ziendeshwe dhidi ya viogozi Wajerumani waliowajibika katika jinai.Hansrashid,
Ahsante sana ndugu yangu kwa kujazia taarifa.
Kuna chuki ya muda mrefu ilienezwa dhidi yao ,hapo kale walidai walikuwa wanasambaza magonjwa na kuwatilia sumu wenzao,tatizo likakuwa baada ya kuenea habari kwamba walimuua Yesu na kule kujitenga kwao huku wakiwa na mafanikio kuliko wenyeji.Ikazalia sera ya anti-Semitism na hata Hitler alipoenda kule Vienna akajifunza mambo hayo na kuibuka baada ya vita ya Kwanza ya dunia kwamba Ujeruman haikushindwa bali wayahudi waliisaliti.Kuna ka ukweli fulani kwa kuwa wayahudi walipigana alongside majeshi ya washirika na hata Urthur Balifour waziri wa makoloni awapa ahadi ya kuwapa nchi Palestina na ikumbukwe kwamba wayahudi walikuwa matajiri na wakimiliki hisa katika makampuni mbalimbali duniani hivyo kulinda maslahi yao Kuna uwezekano wa lolote.Hitler aliwapokonya uraia wa Ujeruman na maeneo aliyoyateka ndo yakafuta ya Auschawitz ,Sobibor na nk.Kwa nini wayahudi walikuwa wana uwawa?
Haiwezekani waiwawe tu bila sababu za msingi?
Kosa lao lilikuwa ni lipi?
Kwa nini mpaka sasa wayahudi hawapendwi huko mashariki ya kati na sehemu zingine duniani? Tatizo lao ni nini?
Asili ya wayahudi ni ubinafsiKwa nini wayahudi walikuwa wana uwawa?
Haiwezekani waiwawe tu bila sababu za msingi?
Kosa lao lilikuwa ni lipi?
Kwa nini mpaka sasa wayahudi hawapendwi huko mashariki ya kati na sehemu zingine duniani? Tatizo lao ni nini?
Swali lako ni zuri, kimsingi linafanana na swali: Je Watutsi (pamoja na watoto wadogo) waliouawa Rwanda mwaka 1994 waliuawa kwa nini??? Haiwezekani wauawe tu bila sababu za msingi?Kwa nini wayahudi walikuwa wana uwawa?
Haiwezekani waiwawe tu bila sababu za msingi?
Kosa lao lilikuwa ni lipi?
Kwa nini mpaka sasa wayahudi hawapendwi huko mashariki ya kati na sehemu zingine duniani? Tatizo lao ni nini?
Bila ya shaka mauaji ya kimbari ya Zanzibar 1964Swali lako ni zuri, kimsingi linafanana na swali: Je Watutsi (pamoja na watoto wadogo) waliouawa Rwanda mwaka 1994 waliuawa kwa nini??? Haiwezekani wauawe tu bila sababu za msingi?
Chuki ya kijamii, na ubaguzi, na matumizi ya chuki katika siasa, huleta matokeo ya kuhuzunisha , pamoja na kutajwa kwa maelezo mengi ya uwongo, na kutoa jibu sahihi ni changamoto.
Nijaribu kwa kifupi kuorodhesha:
1. kwa karne nyingi Wayahudi walibaguliwa katika Ulaya kwa sababu za tofauti ya dini. Hii iliacha mawazo mabaya juu yao na wakati mwingine chuki katika sehemu za raia wakristo.
2. Hadi mwanzo wa karne ya 19 Wayahudi hawakuwa na haki za kiraia waliruhusiwa kuishi tu katika mitaa michache ya miji na wilaya chache. Hawakuruhusiwa kufanya kazi nyingi, wala ukulima wala ufundi, wala biashara nyingi, isipokuwa biashara ya machinga na biashara ya kukopesha fedha. Wengi walikuwa maskini sana, wachache matajiri. Kwa jumla walikuwa tabaka duni.
3. Harakati ya demokrasia iliwapa watu wote haki zaidi pamoja na Wayahudi waliweza kuingia katika kazi nyingi na kuhamia walipopenda, pia kusoma vyuo. Hapa walijitokeza matabibu na wanasheria Wayahudi, wengine walifungua maduka. Asilimia yao kwenye vyuo ilipanda haraka kushinda asilimia yao ndogo kati ya wananchi.
4. Kadri wayahudi walivyoondoka katika "ghetto" zao (mitaa ya Kiyahudi walipobanana mno) na kupata nafasi nzuri, walionewa na watu wengine.
5. Katika karne 19 ilitokea pia mafundisho mapya ya ubaguzi wa kimbari (racism). Mfaransa Gobineau na Mwingereza H.S. Chamberlain walifundisha kuwa mbari wa Kiarya (Aryan race) ni kilele cha ubinadamu, Waasia wako chini yao kiuwezo na Weusi chini kabisa; Chamberlain aliona Wayahudi kama sehemu ya pekee ya Waasia aliwaona ni hatari akiamini wanataka kutawala dunia kwa njama za kisiri. Hakuwaona kama dini bali aliwaona kibiolojia kama mbari (race).
6. Hitler alikuwa mwanafunzi wa Chamberlain. Alichukua mafundisho ya kipaumbele cha mbari ya Waarya na hatari ya Wayahudi. Pia aliona katika Ujerumani aliweza kupata wafuasi akihubiri eti Wayahudi ni sababu kwamba Ujerumani ilishindwa Vita Kuu ya Kwanza.
7. Baada ya kushika serikali alianza mara moja kuwabagua Wayahudi, aliwafukuza walimu, maprofesa, maafisa wa serikali wote kazini kama walikuwa na asili ya Kiyahudi, aliwalazimisha Wajerumani wote kupata "Hati ya Arya" ambako walipaswa kuonyesha hawakuwa na Myahudi kwenye familia katika vizazi 3, aliondoa Uraia wao, alianza kutwaa mali yao. Wakati wa Vita Kuu ya Pili jeshi la Ujerumani lilivamia maeneo ya Poland na Urusi penye Wayahudi wengi. Hapo walianza kuwaua kwa kupiga risasi; baada ya kuona wanajeshi wanachoka waliendelea kwa gesi ya sumu katika makambi ya mauti.
8. Ukiuliza sababu? Ujinga na chuki. Jitahadhari na mwanasiasa yeyote anayeanza kuhubiria "maadui". Hofu ya "maadui" ni mbinu tu kuunganisha wafuasi. mara umeanza inaweza keundelea vibaya.
Kama Mauaji ya Rwanda.
Kwa nini wayahudi walikuwa wana uwawa?
Haiwezekani waiwawe tu bila sababu za msingi?
Kosa lao lilikuwa ni lipi?
Kwa nini mpaka sasa wayahudi hawapendwi huko mashariki ya kati na sehemu zingine duniani? Tatizo lao ni nini?