Nukuu: Wanaume wanamaumivu pia

Nukuu: Wanaume wanamaumivu pia

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
4,809
Reaction score
15,032
Mwanamke mmoja amewahi kunambia kwamba ilimchukua muda mrefu kufahamu kwamba wanaume nao hulia.

Akanisimulia kwamba siku moja weekend alitoka nyumbani kuelekea mahali Fulani huku akiwa amemuacha mumewe nyumbani. Baada ya kufika mbali kidogo amesahau kitu nyumbani, hivyo akarudi kuchukua.

Alipofika kabla hajaingia ndani alimsikia mumewe akisononeka kwa kuongea peke yake huku akimuomba Mungu amuinue kiuchumi ili aweze kutunza familia yake kwani anahali mbaya ya kiuchumi.

Akaniambia kwamba mumewe hajawai kumuambia kama ana matatizo ya kiuchumi, anasema hali hiyo ilimfanya hata yeye kuangusha machozi kwa kutambua kuwa mumewe anapitia kipindi kigumu mno!
--------------------------------------------------------------------------
Binti Fulani ambaye ameolewa alienda kwa mama yake kilalamika kwamba mumewe hamnunulii vitu ambavyo anaviitaji.

Mama akamuuliza "Je kati ya hivyo unavyomuomba akununulie, wewe umeshawai kununua kipi??"

Binti alikaa kimya kisha akasema, "Mama lakini yeye ni mume wangu"

Mama akamjibu "Je wewe umeshawai kujua ni vitu gani mume wako anahitaji na ukamnunulia??"

Wanaume siku siku zote hificha maumivu yao.
-------------------------------------------------------------------------
Mwanamke alialikwa kutoa hotuba katika mkutano wa wanawake. Katikati mwa hotuba yake akawataka wanawake wote wanaojishughulisha na kazi mbali mbali wasimame.

Baada ya kusimama akawauliza ni wangapi hukumbuka hata kuwanunulia waume zao walau shati ama kitu chochote kile???

Wachache hufanya hivyo. Hufikiri kwamba wanaume hawana uhitaji wa kununuliwa vitu wapendavyo!!
--------------------------------------------------------------------------
Wanaume wengi wameoa lakini wanaishi maisha ya kipweke. Muda mwingine jitahidi hata kumtoa Out mume wako, wanaume hawako busy kila siku kama unavyofikiri!!

Inatakiwa ufahamu kwamba wanaume nao wanamaumivu na mahitaji yao pia. Usimjaji kwa vitu ambavyo hata wewe umeshindwa kujinunulia. Muda mwingine hana uwezo."
 
If your friend, partner, coworker, neighbor au hata mwenzi wa ndoa seems to be irresponsible ama is doing something you wish it would have been done differently, and uko so quiet unalalamikia tuuuuuuuu ndani kwa ndani au kwa marafiki au ndugu wengine, humwambii, you are only to be blamed. Relationships zinajengwa kwa communication ambayo ni healthy; hakuna anayezaliwa akiwa na full access ya ufunguo ama ujiniasi wa mahusiano. Sote tunajifunza kila kukicha. Talk, talk, talk positively. Unangoja mambo ziende mrama ndipo useme!???
 
wanawake ni wabinafsi ingawa sio wote.
kuna siku nilimuomba dem wng kiutani anitoe out akakubali tulitumia kama elf70 hivi asee alinuna wiki nzima ikabidi nimrudishie tuuu.maana sio kwa kulalamika hivyo!
Huyo nae wa ajabu, si angekukatalia tu kwamba hayuko vizuri kwa wakati huo? Ama angesubiri few days later akupe invoice ili hela yake irudi.
 
Huyo nae wa ajabu, si angekukatalia tu kwamba hayuko vizuri kwa wakati huo? Ama angesubiri few days later akupe invoice ili hela yake irudi.
Yaani angeirudisha kwa mfumo wa "baby, kuna nzuri nimeiona halafu sina hela kwa sasa, plizzzz..."
Jamaa angeikumbuka ile outing yaani ni dakika sifuri hela yote ingerudi na riba juu...
 
Nilichojifunza kwenye maisha husipolalamika utalalamikiwa. Nilikuwa najifanya kidume silalamika hata hali ikiwa ngumu, walichonifanya ndugu zangu sasa hivi ni mwendo wa kulalamika njaa tu,ukinipigia simu nalalamika njaa uchumi wa kati umebana.

Una matatizo ya kiuchumi mke wako hajui unategemea nini hapo.
 
Mwanamke mmoja amewahi kunambia kwamba ilimchukua muda mrefu kufahamu kwamba wanaume nao hulia.

Akanisimulia kwamba siku moja weekend alitoka nyumbani kuelekea mahali Fulani huku akiwa amemuacha mumewe nyumbani. Baada ya kufika mbali kidogo amesahau kitu nyumbani, hivyo akarudi kuchukua.

Alipofika kabla hajaingia ndani alimsikia mumewe akisononeka kwa kuongea peke yake huku akimuomba Mungu amuinue kiuchumi ili aweze kutunza familia yake kwani anahali mbaya ya kiuchumi.

Akaniambia kwamba mumewe hajawai kumuambia kama ana matatizo ya kiuchumi, anasema hali hiyo ilimfanya hata yeye kuangusha machozi kwa kutambua kuwa mumewe anapitia kipindi kigumu mno!
--------------------------------------------------------------------------
Binti Fulani ambaye ameolewa alienda kwa mama yake kilalamika kwamba mumewe hamnunulii vitu ambavyo anaviitaji.

Mama akamuuliza "Je kati ya hivyo unavyomuomba akununulie, wewe umeshawai kununua kipi??"

Binti alikaa kimya kisha akasema, "Mama lakini yeye ni mume wangu"

Mama akamjibu "Je wewe umeshawai kujua ni vitu gani mume wako anahitaji na ukamnunulia??"

Wanaume siku siku zote hificha maumivu yao.
-------------------------------------------------------------------------
Mwanamke alialikwa kutoa hotuba katika mkutano wa wanawake. Katikati mwa hotuba yake akawataka wanawake wote wanaojishughulisha na kazi mbali mbali wasimame.

Baada ya kusimama akawauliza ni wangapi hukumbuka hata kuwanunulia waume zao walau shati ama kitu chochote kile???

Wachache hufanya hivyo. Hufikiri kwamba wanaume hawana uhitaji wa kununuliwa vitu wapendavyo!!
--------------------------------------------------------------------------
Wanaume wengi wameoa lakini wanaishi maisha ya kipweke. Muda mwingine jitahidi hata kumtoa Out mume wako, wanaume hawako busy kila siku kama unavyofikiri!!

Inatakiwa ufahamu kwamba wanaume nao wanamaumivu na mahitaji yao pia. Usimjaji kwa vitu ambavyo hata wewe umeshindwa kujinunulia. Muda mwingine hana uwezo."
Dah!... ukweli mtupu huu.

Ila ni vizuri kuongea kuliko kuugulia maumivu kimya kimya, utakuwa unajitesa mwenyewe.
 
Mwanamke mmoja amewahi kunambia kwamba ilimchukua muda mrefu kufahamu kwamba wanaume nao hulia.

Akanisimulia kwamba siku moja weekend alitoka nyumbani kuelekea mahali Fulani huku akiwa amemuacha mumewe nyumbani. Baada ya kufika mbali kidogo amesahau kitu nyumbani, hivyo akarudi kuchukua.

Alipofika kabla hajaingia ndani alimsikia mumewe akisononeka kwa kuongea peke yake huku akimuomba Mungu amuinue kiuchumi ili aweze kutunza familia yake kwani anahali mbaya ya kiuchumi.

Akaniambia kwamba mumewe hajawai kumuambia kama ana matatizo ya kiuchumi, anasema hali hiyo ilimfanya hata yeye kuangusha machozi kwa kutambua kuwa mumewe anapitia kipindi kigumu mno!
--------------------------------------------------------------------------
Binti Fulani ambaye ameolewa alienda kwa mama yake kilalamika kwamba mumewe hamnunulii vitu ambavyo anaviitaji.

Mama akamuuliza "Je kati ya hivyo unavyomuomba akununulie, wewe umeshawai kununua kipi??"

Binti alikaa kimya kisha akasema, "Mama lakini yeye ni mume wangu"

Mama akamjibu "Je wewe umeshawai kujua ni vitu gani mume wako anahitaji na ukamnunulia??"

Wanaume siku siku zote hificha maumivu yao.
-------------------------------------------------------------------------
Mwanamke alialikwa kutoa hotuba katika mkutano wa wanawake. Katikati mwa hotuba yake akawataka wanawake wote wanaojishughulisha na kazi mbali mbali wasimame.

Baada ya kusimama akawauliza ni wangapi hukumbuka hata kuwanunulia waume zao walau shati ama kitu chochote kile???

Wachache hufanya hivyo. Hufikiri kwamba wanaume hawana uhitaji wa kununuliwa vitu wapendavyo!!
--------------------------------------------------------------------------
Wanaume wengi wameoa lakini wanaishi maisha ya kipweke. Muda mwingine jitahidi hata kumtoa Out mume wako, wanaume hawako busy kila siku kama unavyofikiri!!

Inatakiwa ufahamu kwamba wanaume nao wanamaumivu na mahitaji yao pia. Usimjaji kwa vitu ambavyo hata wewe umeshindwa kujinunulia. Muda mwingine hana uwezo."
Wanawake wakijitahidi sana leso,soksi labda na boxer basi.

Ila hela ya mwanamke chungu na mara nyingi huambatana na malalamiko,ndio maana sometimes wanaume tunaamua kukaa na yetu moyoni.
 
Nilichojifunza kwenye maisha husipolalamika utalalamikiwa. Nilikuwa najifanya kidume silalamika hata hali ikiwa ngumu, walichonifanya ndugu zangu sasa hivi ni mwendo wa kulalamika njaa tu,ukinipigia simu nalalamika njaa uchumi wa kati umebana.

Una matatizo ya kiuchumi mke wako hajui unategemea nini hapo.
Walalamishi matatizo hayawaishi
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom