PreGE2025 Ntobi asema yeye bado ni mwanachama wa CHADEMA na hana nia ya kujiondoa

PreGE2025 Ntobi asema yeye bado ni mwanachama wa CHADEMA na hana nia ya kujiondoa

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla)

Wont be the same

JF-Expert Member
Joined
Aug 15, 2024
Posts
1,564
Reaction score
2,483
Kupitia ukurasa wake wa X, Emmanuel Ntobi ameeleza kuwa amesikia msimamo wa waliojiondoa lakini yeye hana nia ya kujiondoa.

Ikumbukwe kuwa Ntobi alikuwa team Mbowe wakati wa kampeni, na alitoa maneno makali kwa Lissu hata kupelekea kuvuliwa uongozi aliokuwa nao.

===

"Nimesikia taarifa zinazohusu baadhi ya waliokuwa wajumbe wa Sekretarieti ya CHADEMA Taifa zamani kujiondoa kwenye Chama.

Napenda kuchukua fursa hii kuwajulisha rasmi kwamba mimi, Emmanuel Ntobi, bado ni mwanachama halali wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), na sijawahi wala sina nia ya kujiondoa katika Chama hiki.

Naendelea kuwa mwanachama mtiifu, nikiwa na imani na misingi, itikadi, na malengo ya CHADEMA kama Chama kinachopigania haki, usawa na maendeleo ya kweli kwa Watanzania wote.

Naahidi kuendelea kushirikiana na viongozi wenzangu, wanachama na wapenzi wa CHADEMA katika kuendeleza mapambano ya kuleta mabadiliko ya kweli nchini.

Chief NtobiMei 7, 2025." Emmanuel Ntobi
1746611687622.png


Somapia:

 
Kama hujafundishwa kuayaandika haya basi huu ndio utu uzima. Just remain silent viongozi watakuona.
 
Back
Top Bottom