NSSF wazinduka, wawataka waajiri zaidi ya 3,000 kuwasilisha michango ya wafanyakazi wao

Informer

JF-Expert Member
Jul 29, 2006
1,599
6,670
Shirika la Hifadhi ya Jamii, NSSF limetoa miezi miwili kwa waajiri zaidi ya 3,000 jijini Dar es Salaam, kuiwasilisha michango ya wafanyakazi wao mara moja, na watakaokiuka watafikishwa mahakamani.

Kaimu Mkurugenzi wa shirika hilo, James Oigo ameeleza kuwa katika jiji la Dar es Salaam pekee, hadi kipindi cha mwezi Machi, waajiri 3,234 hawajawasilisha michango ya wafanyakazi wao yenye jumla ya shilingi Bilioni 21.4 kinyume cha sheria.

Amebainisha kuwa tayari shirika hilo limewasiliana na Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP), Vyombo vya Ulinzi na Usalama pamoja na Mahakama kwa ajili ya kuwachukulia hatua kali za kisheria waajiri hao.

Kwa mujibu wa sheria, ni kosa la jinai kwa mwajiri anaposhindwa kuwasilisha michango ya wafanyakazi wake, kwani adhabu yake ni kifungo kisichopungua miaka miwili.
 
Kuna hoja za CAG kuhusu uozo wa shirika wanataka michango ili wakaendelee kufisidi?
 
Shirika la Hifadhi ya Jamii, NSSF limetoa miezi miwili kwa waajiri zaidi ya 3,000 jijini Dar es Salaam, kuiwasilisha michango ya wafanyakazi wao mara moja, na watakaokiuka watafikishwa mahakamani.

Kaimu Mkurugenzi wa shirika hilo, James Oigo ameeleza kuwa katika jiji la Dar es Salaam pekee, hadi kipindi cha mwezi Machi, waajiri 3,234 hawajawasilisha michango ya wafanyakazi wao yenye jumla ya shilingi Bilioni 21.4 kinyume cha sheria.

Amebainisha kuwa tayari shirika hilo limewasiliana na Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP), Vyombo vya Ulinzi na Usalama pamoja na Mahakama kwa ajili ya kuwachukulia hatua kali za kisheria waajiri hao.

Kwa mujibu wa sheria, ni kosa la jinai kwa mwajiri anaposhindwa kuwasilisha michango ya wafanyakazi wake, kwani adhabu yake ni kifungo kisichopungua miaka miwili.

Zoezi liende na mikoani kote; waajiri wengi walizoea kutafuna michango ya wafanyakazi kwa muda mrefu sana! Watumbuliwe tu!
 
Shirika la Hifadhi ya Jamii, NSSF limetoa miezi miwili kwa waajiri zaidi ya 3,000 jijini Dar es Salaam, kuiwasilisha michango ya wafanyakazi wao mara moja, na watakaokiuka watafikishwa mahakamani.

Kaimu Mkurugenzi wa shirika hilo, James Oigo ameeleza kuwa katika jiji la Dar es Salaam pekee, hadi kipindi cha mwezi Machi, waajiri 3,234 hawajawasilisha michango ya wafanyakazi wao yenye jumla ya shilingi Bilioni 21.4 kinyume cha sheria.

Amebainisha kuwa tayari shirika hilo limewasiliana na Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP), Vyombo vya Ulinzi na Usalama pamoja na Mahakama kwa ajili ya kuwachukulia hatua kali za kisheria waajiri hao.

Kwa mujibu wa sheria, ni kosa la jinai kwa mwajiri anaposhindwa kuwasilisha michango ya wafanyakazi wake, kwani adhabu yake ni kifungo kisichopungua miaka miwili.

Mkuu informer. Mimi ni mmoja wa wahanga wa tatizo hilo. Michango yangu ya miaka 3 haijawakirisha kwenye Shirika kutoka kwa Mwajiri wangu. ( Yaani Makato kutoka kwenye Mshahara wangu hayapelekwi NSSF) wakati makato kutoka Kwa Mwajiri mkuu (Serikali - Wizara ya fedha yanapelekwa). Nilienda kuangalia balance nikakuta hizo discrepancies. Nilipohoji kwa nini inakuwa hivyo eti mama mmoja akasema chukuwa form upeleke kwa Mwajiri akujazie. Nikamuuliza hivi kweli Wafanyakazi wa NSSF mnajua Majukumu yenu? Make sheria ya Mifuko ya Hifadhi iko wazi kabisa kuhusu waajiri wasiopeleka Michango ya wanachama ambao ni waajiriwa wao. Nikamuuliza nini majukumu ya Compliance Officer wa NSSF? Akabaki kuniangalia tu. Ilibidi niwaandikie barua kali sana kama Mwanachama, copy nikampa Regulator wao (SSRA). Nadhani kwa kasi hii ya Mzee wa Majipu inabidi wachangamke.
Ndugu zetu wastaafu wamepoteza maisha wengine ni wagonjwa wa stroke kwa sababu ya upuuzi kama huu wa shirika kutofuatilia michango ya wanachama kutoka kwa waajiri. Imagine ndo umestaafu utumish wa umma au popote ulipokuwa unafanya kazi, Kufuatilia michango yako unakuta kuna michango ya miaka 5 wakati ulitumikia taifa miak 30. si utakufa kwa pressure
 
hiyo michango ya wafanyakazi inahitajika ili serikali ya CCM waendelee kukopa kama kawaida yao..
 
NO NO WENGI WANAHAMISHA MICHANGO MIFUKO MINGINE...
HAWA WAMEJENGA MADARAJA NA ECO VILLAGE ZA WAKUBWA AMBAZO NI UBADHIRIFU MKUUU KWANI HAUNA TIJA KWA WANACHAMA..KWANZA WALIPE MADAI YA WANACHAMA
 
em mwenye ujuzi anijuze ni namna gani naweza kummanage mwajiri asopeleka michango? na inaonekana kuna mchezo kati ya mwajiri na hawa wenye mifuko ya hifadhi ya jamii
 
NSSF ni wazembe sana ....mimi binafsi nimeshiriki kuongea na baadhi ya maafisa wakuu kuhusu waajiri ambao ni zaidi ya miaka 3 hawajawahi kupeleka michango ....wakaishia kutoa ahadi ya kufatilia hadi kesho ....nilipowatisha kwa uzembe huu wakaishia kwenda kuomba payroll then hawakurudi tena .....NSSF ni wazembe bora TRA ....makampuni yapo humu mjini tena makubwa hawadai michango wala kuuliza chochote ....kwa ufupi kupeleka michango ni hiari tu ingawa wamepewa meno kisheria kuchukua hatua ....
 
em mwenye ujuzi anijuze ni namna gani naweza kummanage mwajiri asopeleka michango? na inaonekana kuna mchezo kati ya mwajiri na hawa wenye mifuko ya hifadhi ya jamii
Waajiri hawabanwi kupeleka michango while wanakata wafanyakazi ....wizi wa mchana huu ....itolewe notice ya mwezi mmoja kampuni zote zilipe otherwise ni mahakamani kwa hatua za kisheria ....wakifanya kosa la kuruhusu walipe kwa awamu itakula kwao ....
 
  • Thanks
Reactions: MTK
Inawezekana tatizo la staff wa NSSF kushindwa kuwachukulia hatua waajiri hawa wakorofi ni tatizo la management nzima ya NSSF inayofanya staff wawe waoga ....Naunga mkono hii operation kamata wezi ....hawa ni wezi ....NSSF wekeni list ya hayo makampuni ili watie adabu ....makampuni mengine ni ya matajiri wakubwa nchi hii ...
 
Hizi ndio topic zenye maslahi yetu direct ....


Mkuu mimi ni muhanga wa hili. Nilifanya kazi miaka miwili michango yangu haipelekwi NSSF. Nilienda NSSF wakaishia kulipa fomu ya kurekebisha michango, sasa hiyo fomu ikawa ndio kimbembe yani mwajiri ananizungusha kunijazia na NSSF hawanipi msaada wowote na nimepata kazi nyingine so ilinisumbua mpaka nikaamua kuacha na mwajiri a kuonyesha ata kuogopa.


Kama kweli ili litashughulikiwa basi Mungu aibariki sana hii serikali at last sasa wananchi wa kawaida tuna sehemu ya kukimbilia.
 
Nilipohoji kwa nini inakuwa hivyo eti mama mmoja akasema chukuwa form upeleke kwa Mwajiri akujazie. Nikamuuliza hivi kweli Wafanyakazi wa NSSF mnajua Majukumu yenu? Make sheria ya Mifuko ya Hifadhi iko wazi kabisa kuhusu waajiri wasiopeleka Michango ya wanachama ambao ni waajiriwa wao. Nikamuuliza nini majukumu ya Compliance Officer wa NSSF? Akabaki kuniangalia tu. Ilibidi niwaandikie barua kali sana kama Mwanachama, copy nikampa Regulator wao (SSRA). Nadhani kwa kasi hii ya Mzee wa Majipu inabidi wachangamke.


Mkuu mengine yaweza kuwa uzembe au ni Mipango yao!
Iko hivi Mwajiri anaweza kuwa amepeleka pesa lakini wakati wa kuzihamisha kwa Akaunti ya Kila mfanyakazi hapo ndipo palipo na madudu! Sijui hizo pesa inakuwa monitored kivipi!
e.g Kampuni B wafanyakazi 10 kati ya hao watano pesa hazisomeki kwenye Akaunti zao na wakati huu risiti ni mmoja na List,kiasi na akaunti ya wafanyakazi wote imekuwa attached kwenye payment inayofanywa na Kampuni B!

CAG amekwisha dokezo upungufu Mkubwa kwenye mfumo wa uhifadhi wa taarifa za NSSF!
 
Mkuu mengine yaweza kuwa uzembe au ni Mipango yao!
Iko hivi Mwajiri anaweza kuwa amepeleka pesa lakini wakati wa kuzihamisha kwa Akaunti ya Kila mfanyakazi hapo ndipo palipo na madudu! Sijui hizo pesa inakuwa monitored kivipi!
e.g Kampuni B wafanyakazi 10 kati ya hao watano pesa hazisomeki kwenye Akaunti zao na wakati huu risiti ni mmoja na List,kiasi na akaunti ya wafanyakazi wote imekuwa attached kwenye payment inayofanywa na Kampuni B!

CAG amekwisha dokezo upungufu Mkubwa kwenye mfumo wa uhifadhi wa taarifa za NSSF!

Hapo ndipo wanapopiga pesa zetu mkuu. Yawezekana hizo pesa wanazichukuwa na kupeleka kwenye biashara zao.
Inapotokea Mwanachama ame-claim, basi zinawekwa kwenye akaunti yake mara moja. Nasema hivyo kwa sababu siyo mara ya kwanza kukutwa na hali hii. Miaka kama minne iliyopita nilienda kuangalia salio nikakuta lina upungufu wa mil 12. Baada ya kuongea na mhusika akasema hajui kitu ila akasema labda ziko kwenye suspend account. Mwezi mmoja baadaye kwenda kufuatilia ili nichukuwe hatua nikakuta hicho kiasi tayari kimeishaingia kwenye akaunti yangu.
Nasema kuwa kuna wajanja wachache wanaofanya mchezo wa kuchezea pesa za wanachama kwa kuzifanyia biashara kwa sababu ilishatokea pia ofisini kwangu. Enzi hizo Mishahara ikitoka Hazina inaenda Wizarani Wizara ndo inashusha kwenye taasisi zake. Sasa Mhasibu wa Pale kwetu na yule wa Wizarani walikuwa wakicheza mchezo mchafu. Pesa inatoka Wizarani, inaenda kwenye account yao ( Fixed account) baada ya muda wanazitoa hapo tayari wameishapata interest. Huku sisi wafanyakazi tunaambiwa Pesa hazijatoka Hazina. Yaani kipindi hicho Mishahara tulikuwa tunapata 20 ya mwezi unaofuata.
Hata pesa za OC nazo walikuwa wanafanya hivyo hivyo kwa kushirikiana na watu wa Benki
 
Nasema hivyo kwa sababu siyo mara ya kwanza kukutwa na hali hii. Miaka kama minne iliyopita nilienda kuangalia salio nikakuta lina upungufu wa mil 12. Baada ya kuongea na mhusika akasema hajui kitu ila akasema labda ziko kwenye suspend account

Hawa jamaa wa SSRA sijui hii kitu kama hawajui!
Kuna hajakwenye Dunia hii ya DIGITALI hii habari ya suspend Account ife kabisa na pili NSSF walazimishwa kuwa wanachama wao wanakuwa informed kupitia SMS mara mmoja pale Mwajiri anapofanya Malipo kupitia Mobile naamini mwanachama wengi wanasimu.

Hili hapa chini iliishiaga wapi?
Mwisho wamebaki kufungua maofisi kwa gharama kubwa!


Smart cards to help NSSF tame graft and curb losses ...
www.theeastafrican.co.ke/business/-/2560/866108/-/.../-/index.html
Feb 22, 2010 - Smart cards to help NSSF tame graft and curb losses ... unique identification and allows capturing of members' details through electronic forms, ... Mr Mugo says the solution has also enabled Tanzania's NSSF to create mobile .
Mr Mugo says the solution has also enabled Tanzania’s NSSF to create mobile registration terminals, which saves members the cost of going to the institution’s headquarters for services.

To bolster its presence across the world, Techno Brain has partnered with leading information technology organisations such as Microsoft, Oracle, 3i Infotech and Serenic Corporation.
 
Back
Top Bottom