NSSF wana nia nzuri na ni kati ya taasisi zinazoongozwa vizuri kuliko zote Tanzania kwa mawazo yangu binafsi. NSSF ina viongozi waliofunguka kimawazo na wamaobadilika kutokana na wakati na bahati nzuri nimetokea kuwafahamu kwa ukaribu hawa viongozi.
Ushauri wangu ni kwamba pamoja na mazuri mnayofanya NSSF msijiingize kwenye biashara ya Umeme tena kwasababu zifuatazo
1. Matumizi ni makubwa sana: Matumizi ya kufanya biashara ya kufua mafuta kwa njia ya Gas yanaweza kufika $1 Billion hiki ni kiasi kikubwa sana kwa biashara ya umeme pekee. Vilevile kwa Fund yenu yenye $2 Billion ni karibu 50% ya fund nzima. Kuweka uzito mkubwa kiasi hiki kwenye biashara ambayo haieleweki vizuri hasa ukizingatia pesa za NSSF ni za wananchi si vizuri.
2. Siasa: Umeme umekuwa na siasa sana hivyo viongozi wengi huko mbele watafanya mambo mengi ambayo ni ya kishabiki kufurahisha watu bila kujali hadhari za muda mrefu za huduma. Kama mfano bei serikali itakuwa na mkono mrefu kwenye bei ya kufua umeme. Wanasiasa wa serikalini hawana cha ku gain kuwasaidia nyie bali kuongoza ushabiki wa siasa.
3. China na USA: Tanzania na East Africa kwa ujumla inapiganiwa na USA na China na vita imeanza rasmi Tanzania. USA Mfano ndiyo waliowaleta Symbion kutoka kwenye project ya kuweka umeme Afighanistan kuja Tanzania na wanataka kuwaleta GE ili walete Generators. Hizi kampuni hazilipwi na Goverment kama tunavyoambiwa bali zimehakikishiwa na USA kwamba watalipwa kwa njia ya Millinium fund na pesa kutoka kwenye budget la jeshi la Marekani. Balozi wa Marekani naye ni spy wa kijeshi na ni mwanajeshi msaafu. China nao wamekuja na mapigo kwa kutoa Mkopo wa $1 Billion kwa miaka 20 kwa rate ya 2% kwa mwaka au $60m ambayo ni ndogo sana.Wanajua atakaye control Tanzania ndiye atakaye Control Zambia, Kenya, Uganda, Congo, Rwanda, Burundi na hata Mozambique. Obama kapeleka wanajeshi 100 mwezi huu huko Uganda kupambana na waahasi lakini ukweli ni mafuta na yatapita Tanzania.
4. NSSF Tunawahitaji: Tanzania inahitaji sana NSSF kwani Fund nyingine zimelega sana NSSF ndiyo wanaojenga mabweni ya vyuo, vyumba za polisi, nyumba za kukaa n.k. Mkitumia pesa nyingi kwenye miradi ya umeme hakuna pesa itakayobaki kwa maendeleo ya ujenzi.
Pamoja na kwamba kuna wakati niliunga mkono hoja ya NSSF kuingia kwenye umeme sikujua watu wote na mapambano yaliyoko kwenye hili swala. Kwa manufaa ya nchi tunaomba achaneni na mambo ya umeme na rudini kwenye mambo mengine ya maendeleo.
Ushauri wangu ni kwamba pamoja na mazuri mnayofanya NSSF msijiingize kwenye biashara ya Umeme tena kwasababu zifuatazo
1. Matumizi ni makubwa sana: Matumizi ya kufanya biashara ya kufua mafuta kwa njia ya Gas yanaweza kufika $1 Billion hiki ni kiasi kikubwa sana kwa biashara ya umeme pekee. Vilevile kwa Fund yenu yenye $2 Billion ni karibu 50% ya fund nzima. Kuweka uzito mkubwa kiasi hiki kwenye biashara ambayo haieleweki vizuri hasa ukizingatia pesa za NSSF ni za wananchi si vizuri.
2. Siasa: Umeme umekuwa na siasa sana hivyo viongozi wengi huko mbele watafanya mambo mengi ambayo ni ya kishabiki kufurahisha watu bila kujali hadhari za muda mrefu za huduma. Kama mfano bei serikali itakuwa na mkono mrefu kwenye bei ya kufua umeme. Wanasiasa wa serikalini hawana cha ku gain kuwasaidia nyie bali kuongoza ushabiki wa siasa.
3. China na USA: Tanzania na East Africa kwa ujumla inapiganiwa na USA na China na vita imeanza rasmi Tanzania. USA Mfano ndiyo waliowaleta Symbion kutoka kwenye project ya kuweka umeme Afighanistan kuja Tanzania na wanataka kuwaleta GE ili walete Generators. Hizi kampuni hazilipwi na Goverment kama tunavyoambiwa bali zimehakikishiwa na USA kwamba watalipwa kwa njia ya Millinium fund na pesa kutoka kwenye budget la jeshi la Marekani. Balozi wa Marekani naye ni spy wa kijeshi na ni mwanajeshi msaafu. China nao wamekuja na mapigo kwa kutoa Mkopo wa $1 Billion kwa miaka 20 kwa rate ya 2% kwa mwaka au $60m ambayo ni ndogo sana.Wanajua atakaye control Tanzania ndiye atakaye Control Zambia, Kenya, Uganda, Congo, Rwanda, Burundi na hata Mozambique. Obama kapeleka wanajeshi 100 mwezi huu huko Uganda kupambana na waahasi lakini ukweli ni mafuta na yatapita Tanzania.
4. NSSF Tunawahitaji: Tanzania inahitaji sana NSSF kwani Fund nyingine zimelega sana NSSF ndiyo wanaojenga mabweni ya vyuo, vyumba za polisi, nyumba za kukaa n.k. Mkitumia pesa nyingi kwenye miradi ya umeme hakuna pesa itakayobaki kwa maendeleo ya ujenzi.
Pamoja na kwamba kuna wakati niliunga mkono hoja ya NSSF kuingia kwenye umeme sikujua watu wote na mapambano yaliyoko kwenye hili swala. Kwa manufaa ya nchi tunaomba achaneni na mambo ya umeme na rudini kwenye mambo mengine ya maendeleo.