NSSF Kinondoni acheni usanii na uswahili

NSSF Kinondoni acheni usanii na uswahili

Mwaikibaki

JF-Expert Member
Joined
Mar 19, 2015
Posts
3,047
Reaction score
3,784
Wadau,
Nayaandika haya baada ya mdogo wangu ku lodge document kwa ajili ya kujitoa na kuchukua michango yake mwezi mmoja uliopita,baada ya hapo alipewa appointment ya kwenda kuchukua cheki yake jana tarehe 14 april.
Chaajabu alipofika mhusika wa counter ya kutoa cheki akawa anapepesa macho tu baada ya muda akamwandikia arudi baada ya wiki.
Dogo akauliza kama kuna tatizo kwenye documents alizowasilisha awali ila akaambiwa hakuna shida.
Kinachofanya kuandika haya ni kutilia shaka umakini wa NSSF ikizingatiwa kuwa kuna mtumishi mwenzake bwana mdogo waliyefungua wote madai tarehe moja yeye kapewa cheki jana.
My argument:
Kama NSSF mnaona hatari kurudisha michango ya wateja on time mseme tu ifahamike manake mifuko iko mingi si lazima nyinyi,na nimemshauri dogo akishalipwa asirudi mfuko huo tena.
 
Hivi wameshaacha uswahili hawa?? Na hili swala la miezi 6 wana-comply au ndio njoo kesho, njoo kesho kutwa??
BTW, nimesikia Ilala wako vizuri, hata approach na response kwa wateja wao ni nzuri sana. Hawa wa Kinondoni wana tatizo gani haswaa?? Meneja wa NSSF tawi/mkoa wa Kiondoni ameshindwa kazi??
 
Back
Top Bottom