North Korea 'yasemekana' imefanya jaribio la kombora la balistiki lililolipukia angani

Sikirimimimasikini

JF-Expert Member
Dec 27, 2019
2,921
15,613
North Korea 'inasemekana' imerusha leo hii kombora 'linalodhaniwa' ni la balistiki, ambalo limelipukia angani, muda mchache baada ya kurushwa. Hayo yamezungumzwa na South Korea.

Cheong Seong-chang, mtafiti mwandamizi ktk Taasisi ya Sejong ameiambia AFP kuwa dalili zaashiria kuwa jaribio la leo la North Korea lilihusisha kombora kuubwa zaidi la balistiki kuvuka mabara (ICBM) liitwalo Hwasong-17.

Mtafiti huyo akaendelea kusema kuwa jaribio hili lililofeli litachunguzwa na kufanyiwa utafiti zaidi na North Korea. Inaweza ikachukua karibia majaribio matatu kuhakikisha kombora hilo limefanikiwa kufikia malengo ya North Korea. Mtafiti huyo akasema anategemea North Korea kufanya jaribio moja au mawili kabla ya April 15.

Hata hivyo, historia yaonesha North Korea iliisharusha makombora matatu ya balistiki ya kuvuka mabara (ICBM). Kombora la mwisho lilikuwa ni Hwasong-15 lilirushwa November 2017. Kombora hilo lilionesha uwezo mkubwa zaidi na linaweza kufika Washington pamoja na ardhi yote ya Marekani.

novaya-severokoreiskaya-mezhkontinentalnaya-ballisticheskaya-raketa-hwasong-17-hvason-17-gzwdy...jpg


pervye-ispytaniya-severokoreiskoi-mezhkontinentalnoi-ballisticheskoi-rakety-hwasong--d63m122z-...jpg

Picha: Kombora la Hwasong-17 likiwa kwenye gari ya kulibebea lenye pea ya matairi 11 (matairi 22) lilipooneshwa kwa mara ya mwanzo kwenye paredi ya kijeshi mjini Pyongyang mnano October 10, 2020

 
Yaani kuna mijitu iko standby ili kuiangamiza dunia tu.. Haiwazi vitu vya msingi, ni vita tuu muda wote
 
Korea Kusini imepata mpya raisi mpya kichwa maji, kasema anaboresha mifumo ya ulinzi wa anga, ila pia kasema hataogopa kuishambulia Korea Kaskazini ilikiwa ikiwa itaonekana ni tishio kwa Korea Kusini. Kiongozi anayemaliza muda wake alikuwa mwoga mwoga na Kiduku alimsumbua sana.
Mkuu kwani wameputa marais wangapi South Korea?! Halafu mbona waongea maneno matupu matupu bila kuweka hata ushahidi?

Alishindwa Trump rais chizi na baba wa South Korea aliyeahidi kuifuta North Korea, ndio itakuwa hichi kifaranga cha US kipya kilichototolewa juzi kati (rais mpya wa South Korea)?

SmartSelect_20220316-192539_Chrome.jpg
 
Yaani kuna mijitu iko standby ili kuiangamiza dunia tu.. Haiwazi vitu vya msingi, ni vita tuu muda wote
Ndugu yangu Dunia hii ni kama msituni TU,wanyama wakubwa huwala wanya wadogo,hivyo bila mbio utaliwa TU.

Ama ni kama baharini TU,samaki wakubwa huwala samaki wadogo.

Sasa NOKO hataki unyonge huo.

Bila hivyo USA anaweza kuingia nchini kwako na kuoa watu wote bila kujali jinsia.
 
Korea Kusini imepata mpya raisi mpya kichwa maji, kasema anaboresha mifumo ya ulinzi wa anga, ila pia kasema hataogopa kuishambulia Korea Kaskazini ilikiwa ikiwa itaonekana ni tishio kwa Korea Kusini. Kiongozi anayemaliza muda wake alikuwa mwoga mwoga na Kiduku alimsumbua sana.
ikiwa tayari huu uoga
hamnamo rahisi humo nakwambia
 
Mkuu kwani wameputa marais wangapi South Korea?! Halafu mbona waongea maneno matupu matupu bila kuweka hata ushahidi?

Alishindwa Trump rais chizi na baba wa South Korea aliyeahidi kuifuta North Korea, ndio itakuwa hichi kifaranga cha US kipya kilichototolewa juzi kati (rais mpya wa South Korea)?

View attachment 2153142
Jifunze kufanyia kazi hoja moja kwa wakati, Trump katokea wapi kwenye hii hoja au labda nikuulize, unajua Trump alikuwa na hoja gani kuhusu vita katika mataifa ya kigeni?
 
Yaani kuna mijitu iko standby ili kuiangamiza dunia tu.. Haiwazi vitu vya msingi, ni vita tuu muda wote

Hiyo inatokana na dharau na uonevu ukizidi. Watu wanaamua kujihami kwa gharama yoyote ile.
 
Hawa jamaa huenda wanaongoza kwa kuwa na silaha za maangamizi
 
Back
Top Bottom