jojipoji koromije
JF-Expert Member
- Mar 22, 2017
- 1,127
- 1,634
Huwezi kupambana na kuleta mabadiliko makubwa ya kikatiba kwa Nchi ambayo imeongozwa na chama kimoja kwa zaidi ya miongo mitano kwa harakati za barabarani (maandamano & mikutano ya hadhara) na vikao vya majadiliano tu bila nguvu ya bunge, ni ngumu sana. Ili kulainisha mabadiliko haya lazima uwe na wabunge makini katika Bunge hata kwa uchache.
CHADEMA mwaka huu 2025 ilipaswa iingie kwenye uchaguzi kwa namna yoyote ile ili ipambane kupata Rais, Wabunge na Madiwani kwa katiba hii hii iliyopo. Who knows matokeo yangekuwaje? Lakini wasingekosa washindi kwa nafasi hizo. Who knows!!?
Tujiulize CHADEMA hii hii ilipomsimamisha Lowasa kugombea Urais si ilipata viti vingi tu vya wabunge kwa katiba hii hii!!!?
Tujiulize angelisimama Tundu Antipas Lisu ingekuwaje? Hata kama isingeshinda U Rais lakini wangepata viti vingi vya wabunge na Madiwani.
Kupitia hawa wabunge na harakati za barabani na vikao vya majadiliano kuelekea uchaguzi wa 2030 ndo CHADEMA ingelianza na utekelezaji wa mkakati wao wa NO REFORM NO ELECTION.
Basi itoshe kusema kama CHADEMA haitoshiriki katika uchaguzi wa 2025 itakuwa pigo la mageuzi ya kisiasa, ki Katiba, kiutawala na kiuchumi Nchini.
Muda bado upo. Ifanyike kila namna maridhiano yafanyike (vikao vya majadiliano) ili vyama vyote ikiwemo CHADEMA vishiriki uchaguzi hata ikibidi Uchaguzi usogezwe mbele na hii italeta hali ya maridhiano na kuboresha haki na usawa wa kisiasa Nchini.
CHADEMA mwaka huu 2025 ilipaswa iingie kwenye uchaguzi kwa namna yoyote ile ili ipambane kupata Rais, Wabunge na Madiwani kwa katiba hii hii iliyopo. Who knows matokeo yangekuwaje? Lakini wasingekosa washindi kwa nafasi hizo. Who knows!!?
Tujiulize CHADEMA hii hii ilipomsimamisha Lowasa kugombea Urais si ilipata viti vingi tu vya wabunge kwa katiba hii hii!!!?
Tujiulize angelisimama Tundu Antipas Lisu ingekuwaje? Hata kama isingeshinda U Rais lakini wangepata viti vingi vya wabunge na Madiwani.
Kupitia hawa wabunge na harakati za barabani na vikao vya majadiliano kuelekea uchaguzi wa 2030 ndo CHADEMA ingelianza na utekelezaji wa mkakati wao wa NO REFORM NO ELECTION.
Basi itoshe kusema kama CHADEMA haitoshiriki katika uchaguzi wa 2025 itakuwa pigo la mageuzi ya kisiasa, ki Katiba, kiutawala na kiuchumi Nchini.
Muda bado upo. Ifanyike kila namna maridhiano yafanyike (vikao vya majadiliano) ili vyama vyote ikiwemo CHADEMA vishiriki uchaguzi hata ikibidi Uchaguzi usogezwe mbele na hii italeta hali ya maridhiano na kuboresha haki na usawa wa kisiasa Nchini.