Habari wadau,Km mfanyakazi wa Serikali natoa hoja ya sisi wafanyakazi wa Serikalini tuhame kuitumia NMB kupitishia mishahara yetu kwani uongozi na wafanyakazi wameonesha kushindwa au kuzidiwa na kazi kiasi kwamba kuna baadhi ya wafanyakazi hasa wa tasnia ya Ualim wameshindwa kupata mishahara yao kwa muda sasa kwa kosa la hao wafanyakazi wa NMB wakati wa kuituma wanaituma kwa mtu mwengine na mtu anafuatilia miezi kadhaa anapewa ahadi tu na uongozi idara husika hawaoneshi ushirikiano wowote nina wasiwasi na taaluma ya watu wa idara husika kufuatilia wapi mshahara umeenda na kuomba uidhinishaji wa kuurudisha katika akaunti husika kuchukua miezi kadhaa kama ni hivyo hiyo idara iondoshwe wawe wanaomba watu waliobobea kutoka field husika yaani consultants wawasaidie kila mwisho wa mwezi au huenda wamezidiwa na kazi au wamewachoka wateja hasa wafanyakazi wa Serikali kutokana na wengi wao kupitishia mishahara NMB,naishauri kama si kuhama basi Serikali iwaache watu wachague Bank nyengine na mishahara iende huko moja kwa moja bila kupitia NMB wanachosha sana hawa jamaa hasa majibu na kiburi wanachoonesha.Nakusudia NMB Makao Makuu pale Phoenix House.