NMB Mobile ni janga la kitaifa

NMB Mobile ni janga la kitaifa

Ukiendekeza huduma za benki utafilisika... wanatafuta kila njia ili wakate tu hela zako... badala ya saving imekuwa spending... bora niendelee na upatu na vibubu basi.
 
Du, masaa 72!!!

Kwa hiyo tatizo ni Mpesa na NMB au? Sasa mbona wateja hatujajulishwa kuwa tutegemee uchelewaji wa huduma ili tuogope hiyo service kama ukoma.
.
M pesa iko slow kweli. Tigo pesa ni rahisi zaidi kitu kinaingia hapo hapo. Nadhani tatizo ni mtandao wa Vodacom.
 
Mi nadhani siku hiyo ilikuwa na matatizo kiujumla , inawezekana kama mdau mmoja alivyosema selcom ni moja ya tatizo, Natumia crdb mobile jumamosi pia nilihamisha pesa kutoka crdb kwenda tigopesa , hadi muda huu hela haijafika lakini ilishatoka kwenye akaunti yangu.
 
Karibu katika tawi letu lolote la NMB lililo karbu nawe. Ukifka nenda, customer service depatment, ukfka jieleze, then kuna fomu watakupa uijaze. Ukmaliza kuijaza warudshie, then wao wataituma mda huo huo Makao Makuu na ndani ya masaa 24 Makao Makuu watakua wamekurudshia hela yako.
NOTE: Jumamosi na Jumapili Makao Makuu huwa hawafanyi kazi, kwahyo ni bora ukaenda kati ya J3 na Alhamisi.

hela zako unaambiwa ujaze fomu kulikuwa haja gani ya kuanzisha huduma ya nmb mobile wakat hamjajipanga ovyo kabisa
 
Hawa jamaa kinachowapa chati ni kwa vile wamefika katika kila wilaya na wanafanya biashara na taasisi nyingi za serikali hasa halmashauri za wilaya, vinginevyo wangekuwa wameishafutika siku nyingi. Utoaji huduma wao ni wa karne ya 19.

Pia regulators wa shuguli za kibenki inaonekana wamelala fofofo hawajui nini walitendalo ndio maana wateja tunataabika[/QUOTE
Pesa ya serilali na taasisi zake ziwekwe Benki kuu.Hapo NMB itakuwa kwishne.
 
hela zako unaambiwa ujaze fomu kulikuwa haja gani ya kuanzisha huduma ya nmb mobile wakat hamjajipanga ovyo kabisa

Wala kulikuwa hakuna haja..maana tayari wana picha details zako zote utakapowapa card ya benki..ni mambo ya karne ya 19 kabisa..kupotezeana muda kabisa
 
Duh ilinitokea Mbeya kama wiki 3 zilizopita niko tundu fulani na wadau linaitwa green lounge pembeni nikaona wakala wa M-Pesa nikaleta mambo ya digitali kuhamisha pesa kutoka NMB kuja M-pesa weeeee nlitamani ardhi ipasuke maana nimezungusha round za kutosha huku nasubiri muamala thubutuuu masaa yanayoyoma nikawapigia simu naambiwa eti nalo tatizo kitaifa labda kesho,nimejifunza pesa za kuweka kwenye mifumo ya digitali sio zako mpaka ziwe kwenye wallet yako.
 
Nadhani ni mtandao wa voda.

Mleta mada anachanganya mambo,hapa voda ndo hawako serious.nmb hawana tabu,ndo maana ukitupia tigo ni dakika tu unapata majibu.Wateja wa mpesa wangekuwa kama mimi tungeheshimiana,customer care namfokea kama binti yangu
 
Nenda karatu hayana msaada wowote kila cku nenda rudi.rombo ndo usiseme mteja wa alfu 90 anamaliza nusu sa.wako slowly




Hapo bado hujaenda tawi la Mafinga. Wale wahudumu watawahudumia wateja wanaojuana nao kwanza kupitia mlango wa nyuma, huku wewe usiye na anwani umebong'alala tu hadi wajisikie,wenyewe. Looooooo! kwasababu tu ya sababu, or else nisinge kuwa mteja wao
 
Kuna wizi wa fedha kwa wateja NMB, hasa vijijini,na wakopaji wanaibiwa kwa makato yasiyoeleweka nk !

"NMB NI JANGA !"
 
Kuna mtandao wa wizi wa fedha kupitia NMB MOBILE,kwa sababu ya wafanyakazi wezi wa NMB na kampuni za simu.
Ni mhathirika
 
Mleta mada anachanganya mambo,hapa voda ndo hawako serious.nmb hawana tabu,ndo maana ukitupia tigo ni dakika tu unapata majibu.Wateja wa mpesa wangekuwa kama mimi tungeheshimiana,customer care namfokea kama binti yangu

Mkuu wewe ndio umechanganya mambo, Vodacom hiyo hela haijafika nimepiga simu CS
 
Hatimaye nimewapata hawa jamaa wa NMB Mobile kwa njia ya simu. Jibu nililopewa limeniacha hoi bin taaban. Mhudumu bila hata ya kusema samahani ameniambia "kulikuwa na tatizo kwenye mtandao tunalishugulikia hela yako itarudishwa kwenye account yako Jumatano jioni"

Kirahisi rahisi kabisa hela yangu haiko kwenye possession yangu kwa siku tano na sina cha kufanya. Hii benki ni ya kipuuzi, kibazazi, kipumbavu, kijinga na haifai kabisa kuendelea kutoa huduma karne hii. Kama ningekuwa nilihamisha hela kwa ajili ya kulipia huduma muhimu ingekuwa imekula kwangu mazima, unaweza kuua mgonjwa hivihivi kama utategemea hii benki ya hovyohovyo. Hiyo customer service ni kama nimeongea na muuza gongo, sauti kavu iliyojaa kiburi. Hii benki naiombea kila laana iipate ikiwezekana hata ifilisike. Ngoja foleni ya wachukua mshahara ipungue naenda kutoa hela zangu zote kwenye account nahamishia kwenye Kibubu...
 
Hata mimi kuna siku nilijuta. Nilikuwa Mbeya kikazi nilienda ATM yao nikaona foleni kubwa. Wazo likanijia nihamishie pesa ktk mpesa account. Ilinichukua siku nne sms kuingia ktk cm. NMB kwa hilo nina afikiana na mleta mada kuwa mnaudhi wateja wenu.
 
Karibu katika tawi letu lolote la NMB lililo karbu nawe. Ukifka nenda, customer service depatment, ukfka jieleze, then kuna fomu watakupa uijaze. Ukmaliza kuijaza warudshie, then wao wataituma mda huo huo Makao Makuu na ndani ya masaa 24 Makao Makuu watakua wamekurudshia hela yako.
NOTE: Jumamosi na Jumapili Makao Makuu huwa hawafanyi kazi, kwahyo ni bora ukaenda kati ya J3 na Alhamisi.

Kile kitengo cha customer services kifutilieni mbali na zile namba mziblock mnapotezea muda wateja bure. Hii benki yenu ni janga kubwa mno, heri kuweka fedha kwenye kibubu kuliko huko kwenu. Salama yenu ni kuwa regulators mmewaweka mfukoni vinginevyo mneshikishwa adabu
 
Tatizo nikuajiri unprofessional . nadhani management kunatakiwa waliangalie sana hamna professional banker anayeweza kufanya hivyo
 
Inaumiza sana mkuu mimi ni banker by professional ila sidhani kama inaruhusiwa hili swala. kwa uzi huu watajirekebisha usijali mkuu.
Hatimaye nimewapata hawa jamaa wa NMB Mobile kwa njia ya simu. Jibu nililopewa limeniacha hoi bin taaban. Mhudumu bila hata ya kusema samahani ameniambia "kulikuwa na tatizo kwenye mtandao tunalishugulikia hela yako itarudishwa kwenye account yako Jumatano jioni"

Kirahisi rahisi kabisa hela yangu haiko kwenye possession yangu kwa siku tano na sina cha kufanya. Hii benki ni ya kipuuzi, kibazazi, kipumbavu, kijinga na haifai kabisa kuendelea kutoa huduma karne hii. Kama ningekuwa nilihamisha hela kwa ajili ya kulipia huduma muhimu ingekuwa imekula kwangu mazima, unaweza kuua mgonjwa hivihivi kama utategemea hii benki ya hovyohovyo. Hiyo customer service ni kama nimeongea na muuza gongo, sauti kavu iliyojaa kiburi. Hii benki naiombea kila laana iipate ikiwezekana hata ifilisike. Ngoja foleni ya wachukua mshahara ipungue naenda kutoa hela zangu zote kwenye account nahamishia kwenye Kibubu...
 
mimi nakerwa na unapotakawkuangalia salio au kufanza manunuzi kwa NMB mobile, wanakata pesa hata kama hujukamilisha muhamala unakuta umekatwa hela yako, ukweli wanakera, mbona mitandao mingne kama airtel na tigo hawakati salio?
 
Back
Top Bottom