NMB Mobile ni janga la kitaifa

NMB Mobile ni janga la kitaifa

Hivi Vodacom na Tigo wangekuwa na utaratibu mpaka ufike vodashop ndio tatizo lako LA hela litashughulikiwa ingekuwa hatari.

Ni kweli kabisa Mkuu, ila kumbuka hapa tunazungumzia makampuni mawili tofauti NMB na Vodacom, ndo mana mlolongo unakuwa mrefu kidogo. Kuna baadhi ya case huwa hazna mlolongo, mf. labda mteja anatoa hela katka ATM, alafu zkatoka pungufu, akleta malalamiko ndani ya mda mfupi tunampatia hela yake iliyopungua. Vodacom na Tigo wanakuwa faster kwa sababu miamala yao inakuwa inakuwa katika kampuni hiyo hiyo. Nadhani umenisoma mkuu.
 
Hujasema ni lini ulifanya hiyo transaction - isiwe kipindi M-Pesa ilikuwa na matatizo makubwa.

All in all NMB wanajisikia sana matawini na majibu yao sio ya kumvutia mteja - sijui wana idadi kubwa ya wafanyakazi waliokuwapo wakati Benki haina ushindani, enzi za Ujamaa, au ni kwa vile imejipanua kwa ukubwa zaidi kuliko benki nyingine.
 
Niliwahi kutuma pesa fasta.
Niliyemtumia alipata sms ya kutumiwa.
Mimi niliyetuma sikupata sms ya kumpatia
niliyemtumia ili aweze kutoa hiyo hela.
kwenda bank nikapewa fomu nijaze.
miezi nne hela yangu haijarudi.
 
Transaction kupitia mobile banking kutoka Bank account kwenda akaunti ya namba ya simu (m-pesa, tigo pesa, airtel money n.k) and vice versa hapa katikati kuna kitu inaitwa MiddleWere Operator.
Unapohamisha pesa mfano from bank to m-pesa unapata sms kuwa your amount will be credited within 30 minutes, ni kwamba kwenye a/c ya bank imekuwa debited lakini ukiangalia m-pesa haijawa credited (inakuwa hapa kwenye a/c ya middlewere operator - Namzungumzia Selcom Wireless Limited.
Huyu jamaa/mdosi ndiye tatizo kubwa, mtarusha lawama NMB, M-pesa lakini bila kujua system ilivyo mtagaragara hapa bila mafanikio. Unahamisha pesa toka bank, m-pesa haijafika, ukipiga simu NMB bank wanakuambia muamala umekamilika pesa imeshahama lakini ukipiga Voda wakiangalia wanakuambia pesa haijafika huku...funguka akili hapa sasa!
Na inakuwa majanga zaidi kwenye kununua umeme, transfer of funds kwenda makampuni mbali mbali kama Loan Board (HESLB), Necta, Multichoice (Dstv), Startimes etc. Mtandao wake unapokuwa down ama akaunti yake inapokuwa amount low anatumia muda mrefu sana kusort out maana akaunti inayopokea/debit ni kitu kimoja then inayocredit to part B (destination a/c) ni kitu ingine na inachukua muda sana for transaction to reflect from debit (Selcom) to Credit (Destination) customer a/c
Kwa hiyo sasa tunaporusha lawama hapa inabidi tujue tunamlaumu nani, na TCRA na BOT wanatakiwa wadeal na nani hapa na of course wanajua vizuri tu.
 
Niliwahi kutuma pesa fasta.
Niliyemtumia alipata sms ya kutumiwa.
Mimi niliyetuma sikupata sms ya kumpatia
niliyemtumia ili aweze kutoa hiyo hela.
kwenda bank nikapewa fomu nijaze.
miezi nne hela yangu haijarudi.

Are you sure.??? That is too much.. ubovu mmoja, hata Bank wenyewe sijajua wana regulate je, maana ukipitia BAFIA,.2006 au BASEL I na II sidhani kama kuna kitu kama hicho
Bank / BOT ni udhaifu huu waziwazi
 
Mimi nilituma 270,000 kwa mtu jana kwa m-pesa. mpaka leo hajapata! Customer care hawapokei simu pia!

Very frustrating kuwa mteja wa NMB.
 
mm sina hisa Nmb ila aliye toa hoja au maada/thread nakushauri ubadilishe title kwani tatizo siyo NMB tatizo ni Vodacom mpesa kwa sababu ukitoa pesa nmb mobile kwenda mitandao mingine kwamfano tigopesa inakubali fasta so mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni
 
Jumamosi asubuhi nilihamisha hela kwa NMB Mobile toka account yangu ya benki kuja kwenye namba ya simu kwa njia ya MPesa jumla ya shilingi laki mbili. Toka hiyo Jumamosi hadi Leo Jumatatu hela yangu haijafika, nimepiga simu zaidi ya mara 60 kwenye customer service yao sijafanikiwa kuzungumza na mtoa huduma licha ya kwamba kuna wakati nimekaa hewani dakika 18 wananiimbia nyimbo Tu huku namaliza charge kwenye simu yangu.

Nilikuwa naihitaji hiyo hela Jumamosi nimekwamishwa, nimeulizia watu wengine wameniambia imeishawatokea kusubiri hadi wiki nzima ndio hela ikahama.
Wito wangu kwa BOT, haya makampuni ambayo kutoa huduma za hovyo ndio sera zao msiwape leseni ya kutoa huduma sensitive kama za mobile money, wanatutesa na kutunyanyasa wateja na hatuna mtetezi. Hapa nilipo hela haipo kwenye account na haipo kwenye simu kwa siku mbili, nini haki yangu. NMB Ni janga la kitaifa, ingawa tumejiunga kwa sababu za ukabwela wetu, tunaomba mtuthamini walau kidogo.

KAKA SI WEWE TU. WENGI TUMEKUMBWA NA TATIZO HILI LAKINI MIMI PERSONALLY NIMEBAINI TATIZO LIKO M.PESA. MIMI JANA NIMEMTUMIA MKWE WANGU ELA YA FUTARI KWANGU IMETOKA LAKINI KWAKE HAIJAFIKA MPAKA MDA HUU
NILIPOJARIBU KUTUMIA TIGO PESA. ON THE SPOT ELA IMEFIKA i.e. TUJIEPUSHE NA USUMBUFU TUKOME KUTUMIA MTANDAO WA M.PESA TUKI HAMISHA ELA. M.PESA POSSIBLY IMEZEEKA IYO.
 

Nakuunga kwa mikono na miguu, NMB bado wako nyuma sana kiutendaji, labda wafanyakazi wanajichukulia kama wa serikalini ambako hakuna performance review au efficiency indicators, wako bure kabisa kwenye customer care, sifuri kabisa, kiutendaji kwenye ma branch ndio usiombe, wanapiga domo tu, wengine wamekaa tu hujui kama kweli wanaipenda hiyo kazi au vipi, kila kukicha kuna foleni, wana tills kibao, lakini cha kushangaza utakuta moja au mbili tu zinafanya kazi, electronic transfers ndio usiombe, ukiwapigia hawapokei na wakipokea wako hovyo kabisa, mashine zao za ATM zinabuma kila muda..
Benki nying zimewapiga bao kwa kuwa na VISA au MASTERCARD, wao wamekaa tu wako hovyo hovyo, hawajali NMB ikifilisika au iendelee..
Si ajabu utakuta wameajiri ma graduates na wenye masters pale, INASIKITISHA MNO...
 
naendelea kusisitiza tusikariri majibu nimetuma pesa mda huu kutoka nmb mobile to tigopesa no problem pesa imefika fasta ila nimetuma mpesa imegoma SO TATIZO NI MPESA NA SIYO NMB MOBILE TRY TO UNDERSTAND
 
Ni kweli kabisa Mkuu, ila kumbuka hapa tunazungumzia makampuni mawili tofauti NMB na Vodacom, ndo mana mlolongo unakuwa mrefu kidogo. Kuna baadhi ya case huwa hazna mlolongo, mf. labda mteja anatoa hela katka ATM, alafu zkatoka pungufu, akleta malalamiko ndani ya mda mfupi tunampatia hela yake iliyopungua. Vodacom na Tigo wanakuwa faster kwa sababu miamala yao inakuwa inakuwa katika kampuni hiyo hiyo. Nadhani umenisoma mkuu.

Hata ukitetea mkuu...NMB ni miyeyusho tu huduma feki.
 
nikisikia benki hii naanza kuumwa kabisa wafanyakazi wanajisikia mno huwa naomba yafirisike ukipiga simu customer care utaambiwa tutalifanyia kazi tatizo lako hujaulizwa hata accounti na amekata simu siku nyingine unakuta hela zimepungua nilifunga account kabisa

Hawa ni shidaa, mara nyingi nkienda ATM zao unakutana na vidada vinakuuliza tukusajili na NMB mobile? Navyowajibu MUNGU anisamehe bure
 
Jumamosi asubuhi nilihamisha hela kwa NMB Mobile toka account yangu ya benki kuja kwenye namba ya simu kwa njia ya MPesa jumla ya shilingi laki mbili. Toka hiyo Jumamosi hadi Leo Jumatatu hela yangu haijafika, nimepiga simu zaidi ya mara 60 kwenye customer service yao sijafanikiwa kuzungumza na mtoa huduma licha ya kwamba kuna wakati nimekaa hewani dakika 18 wananiimbia nyimbo Tu huku namaliza charge kwenye simu yangu.

Nilikuwa naihitaji hiyo hela Jumamosi nimekwamishwa, nimeulizia watu wengine wameniambia imeishawatokea kusubiri hadi wiki nzima ndio hela ikahama.
Wito wangu kwa BOT, haya makampuni ambayo kutoa huduma za hovyo ndio sera zao msiwape leseni ya kutoa huduma sensitive kama za mobile money, wanatutesa na kutunyanyasa wateja na hatuna mtetezi. Hapa nilipo hela haipo kwenye account na haipo kwenye simu kwa siku mbili, nini haki yangu. NMB Ni janga la kitaifa, ingawa tumejiunga kwa sababu za ukabwela wetu, tunaomba mtuthamini walau kidogo.

Ogopa kufanya miamala ya NMB MOBILE kuanzia pale Mishahara inapotoka mpaka tarehe 05 ya Mwezi unaofuata hiyo ni tahadhari kwako! Mifumo ya Kibenki na Simu kipindi hiki inakuwa hovyo kupita kiasi kwa kuwa Serikali imelazimisha vitu ambavyo tuko tunavitumia ila hatujajiandaa.
 
Ni janga sana mi nlikosea namba ya simu kutoka huko NMB mobile kwenda tigo Nmewaambia wakanambia hawana cha kumfanya, tigo wamempigia jamaa kawatukana na wao hawana cha kumfanya sasa sijui usalama wa hiz pesa zetu uko wapi
 
hii huduma ya nmb mobile ni janga ata mie niliwatimia watu wawili fedha tokea ijumaa yani ela walipata kesho yake mbaya zaidi ukiangalia salio limekatwa na mpaka leo hakuna na notification yoyote ile inayoonesha kua nimetuma kwa mtu fulani
 
wanaboa yan mtu unatoapesa asubuh then jion ndio sms inakuja wakati inatakiwa on the sport unavyotoa pesa sms ikufikie hali hii itasababisa wizi
 
Next time tumia Nmb mobile kutoa au kuweka kwa kutumia Tigo pesa within no seconds muamala wako utakuwa umekamilika,

ila usijali si mda itaiingia maana Mpesa hutumia saa 24 hadi 72 kukamilisha muamala wa kibenki.
Upo vizuri mkuu,na mimi nimeshauriwa hivyo.Leo nipo huku mikoani nikijaribu kutoa fedha kwa M-pesa wananiambia akaunti haina fedha,kilichoniokoa niliacha kadi yangu nyumbani wakanitolea kwenye ATM. Nilipowauliza washikaji zangu town wakanishauri nikirudi niamie tigo pesa ndo ipo vizuri kwa NMB.
 
Back
Top Bottom