Nmb
Washamba kinoma, ingia crdb ujionee maajabu. Watu wapo vizuri, vijana wengi. Wanazijua product fresh. Nmb wazee wengi, wamechoka kinoma. Mfano nilitaka kupurchase online yani nilizungushwa hiyo siku, mwingine anasema chap chap haiwez mwingine anasema inaweza ikiwezeshwa. Me nikawambia basi iwezesheni.
Wakajaribu weee, mwisho wakasema system inasumbua itabid niibadili hiyo akaunti iwe ya kawaida. Hilo nikalikataa maana ingeanza kuincur makato.
Basi wakanipa option ya kufungua prepaid akaunti tena wanasema ni special kwa manunuzi. Nikakubali. Mchakato ukaanza. Nilipomaliza nikaambiwa niiwekee hela. Nilikuwa nina 90k. Nimeenda kwa cashier akawa haelewi eti, kabla hata hajalogin akasema mtandao wa hiz haupo, eeh bwana ee, niliudhika hiyo siku, nikarudi kwa aliyeifungua akanambia ingia bulk kuna mtu atakusaidia.
Kule nikakuta kuna sister flani nikamuuliza kwann mtandao wa prepaid haupo eti akajifanya kushangaa, akaniuliza nimejuaje. Nikamwambia cashier kasema. Akaichukua kadi yangu na hela akalogin akadeposit ile hela fresh. Akachukua simu akamcall huyo cashier akaanza kumind. Mwisho akamwambia akija mteja wa prepaid mwelekeza aje bulk.
Hii ikanipa picha kabisa kuwa hawa staff ni viazi kwakuwa hawazijui product zao.