Ngaliba Dume
JF-Expert Member
- Oct 6, 2010
- 1,710
- 3,685
Katika hali inayoonyesha kubanwa na kupata upinzani mkubwa ndani ya chama chake cha CCM,mbunge wa Chemba Juma Nkamia,amejikuta akizomewa na wananchi wake wakati wa kujinadi kuomba kura za kuteuliwa kuwa mbunge wa Jimbo hilo kupitia CCM.
Nkamia alijikuta ktk hali ngumu baada ya kupanda jukwaani ili kuomba ridhaa ya wanachama kumchagua kwa mara nyingine kupeperusha bendera ya chama,kundi la vijana lilikatiza hotuba yake kwa kupiga kelele na kumzomea kuwa ashuke jukwaani kwani hakuna kitu alichokifanya kwa kipindi cha miaka mitano zaidi ya porojo ndani ya bunge.
"Sema ulichotufanyia kwenye ubunge wako wa miaka mitano,hatutaki upoteze muda,hapa tuna migogoro ya ardhi,shida ya maji,huduma mbovu za afya,elezea umefanyaje ili serikali itatue?".Hata hivyo Nkamia akaishia kusema tu wananchi wakasome vipeperushi vyake alivyogawa watajua nini kafanya.
Akijibu swali la kuzuia mauwaji mpakani mwa Chemba na Kiteto,Mh. Nkamia alisema ya aliwaamuru wananchi wa Chemba wakapambane na wafugaji,na walifanikiwa na kuanza kulima..hali hii ilimfurahisha Rais Kikwete mpaka akamteua kuwa Naibu Waziri wa Habari,Michezo na Utamaduni.
Hali imezidi kuwa mbaya kwa mbunge huyo ndani ya hekaheka za kula za maoni.
Nkamia alijikuta ktk hali ngumu baada ya kupanda jukwaani ili kuomba ridhaa ya wanachama kumchagua kwa mara nyingine kupeperusha bendera ya chama,kundi la vijana lilikatiza hotuba yake kwa kupiga kelele na kumzomea kuwa ashuke jukwaani kwani hakuna kitu alichokifanya kwa kipindi cha miaka mitano zaidi ya porojo ndani ya bunge.
"Sema ulichotufanyia kwenye ubunge wako wa miaka mitano,hatutaki upoteze muda,hapa tuna migogoro ya ardhi,shida ya maji,huduma mbovu za afya,elezea umefanyaje ili serikali itatue?".Hata hivyo Nkamia akaishia kusema tu wananchi wakasome vipeperushi vyake alivyogawa watajua nini kafanya.
Akijibu swali la kuzuia mauwaji mpakani mwa Chemba na Kiteto,Mh. Nkamia alisema ya aliwaamuru wananchi wa Chemba wakapambane na wafugaji,na walifanikiwa na kuanza kulima..hali hii ilimfurahisha Rais Kikwete mpaka akamteua kuwa Naibu Waziri wa Habari,Michezo na Utamaduni.
Hali imezidi kuwa mbaya kwa mbunge huyo ndani ya hekaheka za kula za maoni.