fikirikwanza
JF-Expert Member
- Jan 25, 2012
- 7,452
- 3,065
Ni kweli kuwa TANU na CCM zimesaidia sana kutupatia mafanikio ambayo tunayo kama yapo; Ni kweli kwamba uongozi wa Mwl Nyerere umetusaidia sana TZ kujenga nchi na huruka ya wananchi wake. Hongera CCM ya Mwalimu.
Kwa mpenda maendeleo ambaye pia ni mwanachama wa CCM kama ambavyo wengi wa watanzania waliwahi kuwa wana TANU au CCM, ni wazi ili kuondoka hapa tulipofika, ambayo si sehemu mbaya japo sio sehemu tuliyotaka kwenda tunahitaji wanaCCM wengi kuachana na CCM na kuungana na mbadala wa CCM ili wote kwa pamoja tufike tulikotaka kwenda. Hii hatua ni lazima, maana tumekwama lazima tujaribu mbinu nyingine za kujikwamua- Shime wanaCCM rudisheni kadi zenu kisha mchukue kadi mbadala kwa manufaa ya taifa lenu. UOGA ndo adui mkubwa ya maendeleo, acheni uoga ktk kusimamia taifa.
Nadhani furaha ya kufika kwenye mafanikio, kwenye taifa linalojitegemea ni furaha ya taifa; CCM wamejaribu bila mafanikio. Nachokili kuwa wamefanikiwa ni kuonesha kuwa kwa mbinu na uongozi wao taifa lolote haliwezi kufikia maendeleo yanayo kusudiwa. Hongereni kwa kuonesha mbinu ambazo haziwezi kunufaisha taifa.
Shime watanzania, tuungane kurekebisha makosa; moja, kwa kuwapumzisha CCM ili tushinde; ni kama kwenye mpira substitution huwanyika ili kufanikisha lengo la mchezo ambao mara nyingi ni kushinda; pili, faida ya CCM kumpuzika ni ya taifa zima, hivyo waone furaha kubwa kupumzika. Pumzikeni kwa furaha na amani kwamba, watanzania wenzenu pia wanaweza kuongoza ili kuona kama tunaweza kujikwamua na umaskini wa taifa tajiri kama letu; PUMZIKA KIKWETE, PUMZIKA MSEKWA, PUMZIKA PINDA, PUMZIKA SHEIN, PUMZIKA CCM. Pole kwa kazi ngumu ambayo haikuzaa matunda, umejaribu kwa kiasi chako. ACHENI CCM IFE, ili TAIFA LISIFE, hamna cha kupoteza maana TAIFA litabaki.
Ushauri wangu kwa CCM na WanaCCM, Tanzania.
Kwa mpenda maendeleo ambaye pia ni mwanachama wa CCM kama ambavyo wengi wa watanzania waliwahi kuwa wana TANU au CCM, ni wazi ili kuondoka hapa tulipofika, ambayo si sehemu mbaya japo sio sehemu tuliyotaka kwenda tunahitaji wanaCCM wengi kuachana na CCM na kuungana na mbadala wa CCM ili wote kwa pamoja tufike tulikotaka kwenda. Hii hatua ni lazima, maana tumekwama lazima tujaribu mbinu nyingine za kujikwamua- Shime wanaCCM rudisheni kadi zenu kisha mchukue kadi mbadala kwa manufaa ya taifa lenu. UOGA ndo adui mkubwa ya maendeleo, acheni uoga ktk kusimamia taifa.
Nadhani furaha ya kufika kwenye mafanikio, kwenye taifa linalojitegemea ni furaha ya taifa; CCM wamejaribu bila mafanikio. Nachokili kuwa wamefanikiwa ni kuonesha kuwa kwa mbinu na uongozi wao taifa lolote haliwezi kufikia maendeleo yanayo kusudiwa. Hongereni kwa kuonesha mbinu ambazo haziwezi kunufaisha taifa.
Shime watanzania, tuungane kurekebisha makosa; moja, kwa kuwapumzisha CCM ili tushinde; ni kama kwenye mpira substitution huwanyika ili kufanikisha lengo la mchezo ambao mara nyingi ni kushinda; pili, faida ya CCM kumpuzika ni ya taifa zima, hivyo waone furaha kubwa kupumzika. Pumzikeni kwa furaha na amani kwamba, watanzania wenzenu pia wanaweza kuongoza ili kuona kama tunaweza kujikwamua na umaskini wa taifa tajiri kama letu; PUMZIKA KIKWETE, PUMZIKA MSEKWA, PUMZIKA PINDA, PUMZIKA SHEIN, PUMZIKA CCM. Pole kwa kazi ngumu ambayo haikuzaa matunda, umejaribu kwa kiasi chako. ACHENI CCM IFE, ili TAIFA LISIFE, hamna cha kupoteza maana TAIFA litabaki.
Ushauri wangu kwa CCM na WanaCCM, Tanzania.