SteveMollel
JF-Expert Member
- Jul 12, 2015
- 8,803
- 25,444
- Thread starter
- #461
*Njia nyembamba -- 14*
Mtunzi: SteveMollel
“Ah – ah! Sina shida!” Alijibu mfanyakazi akitikisa kichwa. Macho yake hayakuwa yanamtazama Talib, aliogopa. Talib alimdaka mkono uliobebelea kinywaji, akamkazia macho yake makali.
“Una nini?”
Macho ya mwanamke yalikuwa mekundu, na ghafla yakaanza kujaza machozi.
“Sina kitu mheshimiwa!”
Talib alikwapua chupa ya kinywaji, akamwamuru mfanyakazi apotee mbele ya macho yake. Hakuona tena haja ya kutumia glasi iliyokuwa imetapakaa kinywaji, basi akapeleka mdomo wa chupa kinywani mwake na kunywa mafundo kadha wa kadha kana kwamba anakunywa juisi.
Aliendelea kunywa na kunywa akiwaza na kuwazua, akingoja Rose aletwe mbele yake kwa ajili ya adhabu. Alimaliza chupa yote pasipo mrejesho wowote wa oparesheni, akampigia simu kiongozi kumuuliza kinachoendelea.
“Bado hatujampata, mkuu. Tunaendelea kutafuta!”
Talib alingoja akibinua mdomowe. Kinywaji kimoja alichokunywa kilimtosha asihitaji kuongeza cha ziada. Kichwa kilikuwa kinapiga marimba kwa mbali, Jack Daniel akizurura. Basi taratibu usingizi ukaanza kumkweza.
Walinzi lukuki waliokuwa wamekaa nje, hawakuwa wanajua kinachoendelea huko ndani. Macho na midomo yao ya bunduki ilikuwa imeelekezea nje wakiwa wamejiweka tayari kabisa kwa ajili ya kupambana dhidi ya watu wa aina yeyote watakaotishia uwepo wa amani. Hawakujua adui mkubwa zaidi alikuwepo ndani na si nje.
Baada ya muda kupita, Rose aling’amua ya kwamba Talib alikuwa amelala usingizi wa kilevi kochini. Taarifa hiyo alipewa na mfanyakazi wake baada ya kukiri kushindikana kwa zoezi la kwanza – kumpatia sumu ‘adui’. Alichungulia kuhakikisha. Akatazama pia na nje, mazingira yalikuwa sawia.
Alienda jikoni kutwaa kisu. Mkono wake ulikuwa unatetemeka. Alisogeza hatua zake kufuata ngazi za kushuka chini sebuleni. Kichwa chake kilikuwa kinagonga kwa mawazo, vipi kama akishindwa? Lakini moyo wake ulimwambia vipi kama akifanikiwa? Na huo ndio uliofanikiwa kumshinda.
Huu ulikuwa ni wasaa wake wa kumaliza mzizi wa fitna. Kwa namna moja ama nyingine alijehesabia kama akifanikiwa kufanya hilo tukio, basi ataonekana shujaa mbele ya wafanyakazi lakini pia wale wote wanaoteseka kwa njia moja kwasababu ya utawala wa Talib. Aliwaza pia huo ndio utakuwa mwanzo wa mapinduzi ya kweli nchini Sierra Leone.
Mapigo yake ya moyo yalikimbia, jasho likamtiririka. Macho yake kama mbwa mwizi yalizunguka huku na kule akihema taratibu.
Kweli alikuwa amelala. Rose alisimama mbele ya Talib pasipo mwanaume huyo kufanya chochote, isipokuwa kukoroma. Aliutoa mkono wake uliobebea kisu nyuma ya mgongo, akaukutanisha na mwingine kushikilia mpini.
Lahaula! Kabla ya ncha ya kisu kutoboa kifua cha Talib, ghafla mkono mnene wa Taib ulidaka mikono yote miwili ya Rose. Macho mekundu ya mwanaume huyo yalitoka nje kwa namna ya kuogopesha. Mkono wake mwingine ulikwapua kisu toka kwenye mikono ya Rose, kisha ukamzaba kofi zito. Rose akarukia maili moja mbali!
“Pumbavu uliyekithiri!” Talib alilaani akinyanyuka, mkono wake wa kulia ulikuwa umebebelea kisu.
“Unadhani mimi nakufa kikondoo hivyo? Nimekwepa risasi nyingi mpaka kuwepo hapa. Mikono mingi ya wanaume ilishindwa, itaweza ya mwanamke malaya kama wewe!”
Rose hakujibu kitu. Uso wake upande wa kushoto ulikuwa mwekundu kana kwamba bendera. Kiganja na vidole vya Talib vilikuwa vimemwachia chapa ya uhakika. Macho yake yalikuwa mekundu pia mdomo wake akiubenua.
Mlinzi mmoja alifungua mlango kutazama usalama, Talib akamwagiza awahabarishe wenzake warejee kwani ameshampata mhusika. Mlinzi akafunga mlango na kutekeleza agizo.
“Sasa leo itakuwa ni siku yako ya kujifunza,” alisema Talib. “Kama mama yako alishindwa kukufunda, acha nimsaidie.”
Alivua mkanda wa sare yake ya jeshi, akaukamata mkononi. Alimtandika nao Rose kana kwamba anamchapa punda. Rose alipiga kelele kali za maumivu, ila hakuna aliyediriki kuja kumsaidia. Mfanyakazi wake aliyekuwa anatazama zoezi hilo kwa mbali aliishia kububujikwa tu na machozi. Alitamani kumkomboa lakini asingeweza kuthubutu abadani.
Mwili wa Rose ulikuwa mwekundu. Ulivijilia damu na hata kutokwa na majeraha yaliyosababishwa na chuma cha mkanda wa Talib. Hakukoma kupokea kipigo mpaka pale alipozirai. Talib alikuwa anavuja jasho kwa kazi hiyo pevu, hata pumzi yake alikuwa anahangaika kuitafuta.
“Beba katupieni jela akafie huko!” Aliagiza Talib juu ya Rose. Wanajeshi walimbeba Rose kama kiroba cha bidhaa, wakamtupia kwenye gari lao.
***
Mwanaume aliyevalia kombati nyeusi alikuwa amesimama mbele ya kundi la watu mia tatu kwa idadi ya haraka. Kichwa chake kilikuwa kimefunikwa na kiremba cheupe, uso wake ulikuwa umejawa ndevu. Mwanaume huyu, mwenye ‘ka asili’ ka uchotara wa kiarabu na ngozi nyeusi, macho yake yalikuwa makubwa na ya kutisha. Uso wake ulikuwa mgumu na wenye dhamira.
Miaka ya nyuma alikuwa mshiriki mkubwa wa mapinduzi ya Liberia akiwa na nyadhifa kubwa tu ndani ya kundi la Les Tueurs lililofanikiwa kutwaa dola ya Liberia. Ilikuwa hivyo mpaka pale alipokuja kukosana na wenzake kwa kutaka kuingiza itikadi kali za dini, hali iliyoleta mpasuko kundini.
Watu kadhaa waliomuamini na kumwona yupo sahihi walienenda naye, huku waliobakia, chini ya Al Saed, wakiendeleza harakati. Ila kabla ya kwenda, alimwachia Al Saed ujumbe mzito. Ujumbe ambao unamtesa mpaka leo hii.
Ilikuwa ni siku moja tu baada ya yeye kujiengua toka kundini kwa misingi ya dini. Siku hiyo ilikuwa ndefu mno kwa kundi la Les Tueurs kwani kwanzia alfajiri walikuwa kwenye mpambano mazito na wanajeshi wa Liberia: pambano la pili toka mwisho kuelekea kutwaa dola. Ikiwa wamepumzika toka kwenye siku hiyo ambayo iliisha kwa kupata ushindi wa mbinde, mwanaume huyu alizama kambini.
Ndani ya kambi iliyokuwa na wanaume lukuki, tena wakiwa na silaha, alipita kwa ustadi akilenga kwenda kuonana na Al Saed ndani ya hema lake lililopo katikati ya kambi. Mpaka anafika hapo hemani, alikuwa amefanikiwa kuwamaliza wanaume watano kwa kuwanyonga, hakuna aliyepiga kelele! Al Saed alijua ya kwamba amevamiwa baada tu ya zipu ya hema kufunguliwa.
“Samahani kwa kuja pasipo mwaliko,” alisema mwanaume huyu akitabasamu. Alikuwa amevalia kombati za jeshi, kwenye paja lake la kuume alining’iniza bunduki ndogo, paja lake la kushoto likibebelea kisu kirefu.
“Unataka nini kwangu?” Al Saed aliuliza. Mwanaume huyu akaketi pasipo ruhusa.
“Huu ni ujio wangu wa mwisho kwako. Baada ya hapa, ni wewe ndiye utakayekuwa unanitafuta.”
“Unataka nini kwangu?” Al Saed alirudia swali.
“Nataka kukupa nafasi ya mwisho,” mwanaume huyu akajibu. “Badili mawazo yako kabla hujakawia.”
“Ni wewe ndiye utabadili, si mimi!” alisema Al Saed kwa kujiamini kisha akaamuru;
“Toka machoni mwangu kabla sijakuvunja vipande vipande!”
Mwanaume huyu alisimama akachomoa kisu chake na kukichomeka mezani kwanguvu.
“Hili litakuwa agano langu na wewe!”
Wapambanaji wa Al Saed waligundua kwamba wamevamiwa. Walifurika mbele ya hema la kiongozi wao wakiwa wamebebelea silaha. Al Saed aliwakataza kuingia ndani. Hata pale alipomalizana kuongea na mgeni wake huyu, alitaka aachiwe aende kwa amani.
Tangu hapo alipotea, na alipokuja tena kwenye macho na masikio ya Al Saed, jina lake halikuwa Odong tena kama alivyokuwa anajulikana huko nyuma, bali Mr. X. mwanaume mwenye jeshi sasa akidhamiria kumtoa Al Saed madarakani na kuanzisha utawala wa kidini.
Mkononi mwake akiwa na silaha aina ya SMG, alitazama wapambanaji wake kama mtu achambuaye chuya toka kwenye mchele. Watu hao waliokuwa wamesimama kwa ukakamavu walivalia kombati za kijani, mkononi mwa kila mmoja kukiwa na bunduki kama ya kiongozi wao.
Mazingira yaliyokuwa yamewazunguka yalikuwa ni tulivu mno wakizingirwa na milima na miti iliyojazana kedekede. Hakika ilikuwa ni sehemu salama kwa mafunzo na makutano yao. Lakini kama vile haitoshi bado kulikuwa kuna walinzi maili kadhaa toka eneo hilo la kazi wakihakikisha usalama zaidi.
Mr. X alisafisha koo lake kisha akasema:
“Pongezi sana kwa oparesheni ya mwisho, bila shaka itakuwa salamu nzuri sana kwa makafiri!”
Wanamgambo wake wakanyoosha bunduki zao juu na kupiga kelele za kushangilia.
“Hatutakoma mpaka pale tutakapohakikisha tunawamaliza wote, na kuliweka taifa kwenye mikono ya mwenyezi Mungu! Ukae ukijua kila siku, unapokuwa vitani kupambana, haupambani kwasababu yangu; haupambani kwasababu yako; haupambani kwasababu ya wa Liberia, bali unapambana kwa sababu ya mwenyezi Mungu pekee!”
Wanamgambo wake wakanyoosha bunduki zao juu na kupiga kelele za kushangilia.
“Zawadi na malipo yetu hayapo duniani bali akhera!”
Wanamgambo wakanyoosha bunduki zao juu na kupiga kelele za kushangilia.
Baada ya kusisimuana huko, Mr. X alichukua wasaa wake kuanza kueleza mipango ya mbele, hufanya hivi kila baada ya muda fulani kwa ajili ya kuondoa sintofahamu ndani ya kundi lakini pia kutengeneza njia ya kutimiza malengo yao. Aliteua wanaume watano kwa kuwaita majina, wanaume hao kwa utiifu mkubwa wakajongea mbele kiukakamavu. Walikuwa na miili ya mazoezi na sura za kazi. miongoni mwao, ni mmoja tu aliyekuwa mfupi na mweupe, wote walikuwa wanaikimbiza anga kwa urefu na ngozi zao zikiwa nyeusi barabara.
“Siku ya keshokutwa, kuna ujio mkubwa nchini. Wanadiplomasia watano toka nchi kubwa ughaibuni watakuja kwa ajili ya kuketi meza moja na Al Saed kujadiliana kuhusu mustakabali wa nchi … nataka wanadiplomasia hao wakiwa wafu! Kwa njia na gharama yoyote ile.
Kwenye majira ya saa tisa jioni, watatua kwenye uwanja wa ndege wa Monrovia wakitokea kwenye ndege ya shirika la ndege la Delta. Siku hiyo usalama utakuwa mkubwa uwanjani hapo, hivyo mnatakiwa kuwa makini sana. Muweke vichwani kwamba sehemu pekee ya kuwamaliza wanadiplomasia hao kiurahisi ni hapo uwanjani pekee. Hivyo ni lazima wauawe siku hiyo!”
Baada ya maelezo hayo walitawanyika ila wanaume wale watano wateule waliongozana na Mr. X mpaka makaoni, chini ya msikiti. Mr. X alitoa ramani ya uwanja wa ndege toka kwenye nyaraka zake, akaitandaza mezani. Aliwaelekeza wapambanaji wake kitu cha kufanya, na namna ya kufanya kuhakikisha kila kitu kinaenda kama kilivyopangwa. Alipomaliza alimkabidhi mmojawapo ramani ile.
“Sitegemei kushindwa. Bila shaka mnajua gharama ya kushindwa.”
“Ndio, mkuu!”
“Mnaweza mkaenda.”
***
Giza liliingia kwa haraka siku hiyo, kwa sasa ilikuwa ni saa nne usiku. Ndani ya kituo walikuwepo polisi wachache sana, watatu tu kwa idadi. Polisi hao walikuwa wote wapo kaunta, wawili walikuwa wamelala mmoja akiwa anachezea simu yake kwa kuperuzi mitandaoni.
Mazingira ya kituo yalikuwa hafifu, taa moja kubwa iliyokuwa mbele ndiyo pekee ilisimama huko nje, nyuma ya kituo kulikuwa ni giza totoro. Kwa upande wa ndani, ni kaunta tu ndipo kulipokuwa na mwanga, lakini huko kwengine kwa mahabusu kulikuwa ni giza totoro. Shukrani kwa wale ambao vyumba vyao vilikuwa vinaibiaibia mwanga wa ile taa moja ya nje.
Polisi hao wakiwa hawana habari, na aidha wakiwa wanauvuta muda kutafuta siku mpya wapate kumaliza ‘shifti’ yao warudi nyumbani, mara mambo taratibu yanaanza kwenda kombo.
Sauti kubwa ya mahabusu mmoja inaita kwanguvu.
“Afandee, kuna mtu kazidiwa! Afandee!”
Polisi aliyekuwa anaperuzi alisonya na kupuuzia, wenzake hata hawakushtuka. Sauti ya mahabusu haikukoma kuita, ikaendelea kuomba msaada. Mwishowe polisi mmoja aliyekuwa usingizini akaamka kwa kufungua jicho moja.
“Kuna nini?”
“Si hao wajinga wameanza usumbufu!” Alijibu polisi anayechezea simu.
“Kawasikilize basi.”
“Siendi, sina muda huo.”
“Nenda kawasikilize bana, si unajua wakifia humo ndani huwa bonge la ishu!” aliendelea kusisitizia polisi yule akiwa anatazama kwa jicho moja asiupoteze usingizi wake.
“We nawe ni usingizi tu ndio unaokusumbua,” alilalama polisi aliyekuwa anachezea simu. “Unanisumbua tu ili ulale.”
Aliamka akaenda huko sauti ya kuitwa inapotokea. Alisimama mlangoni mwa mahabusu akatazama ndani. Kulikuwa kuna mwanga hafifu, hususani kwake kulikuwa giza totoro kwakua alitoka kwenye mwanga – wa taa na wa simu. Hivyo ikawa inamchukua muda kuona ndani.
Ghafla alijikuta amedakwa shingo, akavutwa kubamizwa kwenye nondo za mlango wa mahabusu, kang’! Akazirai. Haraka kabla hajadondoka chini, ufunguo wa mahabusu uliokuwa unaning’inia kiunoni mwake ukachomolewa, na mlango wa mahabusu ukafunguliwa upesi.
Mwanaume wa kwanza kutoka ndani, alikuwa Kone. Mkononi mwake ndiye alikuwa amebebelea funguo!
****
☆Steve
Mtunzi: SteveMollel
“Ah – ah! Sina shida!” Alijibu mfanyakazi akitikisa kichwa. Macho yake hayakuwa yanamtazama Talib, aliogopa. Talib alimdaka mkono uliobebelea kinywaji, akamkazia macho yake makali.
“Una nini?”
Macho ya mwanamke yalikuwa mekundu, na ghafla yakaanza kujaza machozi.
“Sina kitu mheshimiwa!”
Talib alikwapua chupa ya kinywaji, akamwamuru mfanyakazi apotee mbele ya macho yake. Hakuona tena haja ya kutumia glasi iliyokuwa imetapakaa kinywaji, basi akapeleka mdomo wa chupa kinywani mwake na kunywa mafundo kadha wa kadha kana kwamba anakunywa juisi.
Aliendelea kunywa na kunywa akiwaza na kuwazua, akingoja Rose aletwe mbele yake kwa ajili ya adhabu. Alimaliza chupa yote pasipo mrejesho wowote wa oparesheni, akampigia simu kiongozi kumuuliza kinachoendelea.
“Bado hatujampata, mkuu. Tunaendelea kutafuta!”
Talib alingoja akibinua mdomowe. Kinywaji kimoja alichokunywa kilimtosha asihitaji kuongeza cha ziada. Kichwa kilikuwa kinapiga marimba kwa mbali, Jack Daniel akizurura. Basi taratibu usingizi ukaanza kumkweza.
Walinzi lukuki waliokuwa wamekaa nje, hawakuwa wanajua kinachoendelea huko ndani. Macho na midomo yao ya bunduki ilikuwa imeelekezea nje wakiwa wamejiweka tayari kabisa kwa ajili ya kupambana dhidi ya watu wa aina yeyote watakaotishia uwepo wa amani. Hawakujua adui mkubwa zaidi alikuwepo ndani na si nje.
Baada ya muda kupita, Rose aling’amua ya kwamba Talib alikuwa amelala usingizi wa kilevi kochini. Taarifa hiyo alipewa na mfanyakazi wake baada ya kukiri kushindikana kwa zoezi la kwanza – kumpatia sumu ‘adui’. Alichungulia kuhakikisha. Akatazama pia na nje, mazingira yalikuwa sawia.
Alienda jikoni kutwaa kisu. Mkono wake ulikuwa unatetemeka. Alisogeza hatua zake kufuata ngazi za kushuka chini sebuleni. Kichwa chake kilikuwa kinagonga kwa mawazo, vipi kama akishindwa? Lakini moyo wake ulimwambia vipi kama akifanikiwa? Na huo ndio uliofanikiwa kumshinda.
Huu ulikuwa ni wasaa wake wa kumaliza mzizi wa fitna. Kwa namna moja ama nyingine alijehesabia kama akifanikiwa kufanya hilo tukio, basi ataonekana shujaa mbele ya wafanyakazi lakini pia wale wote wanaoteseka kwa njia moja kwasababu ya utawala wa Talib. Aliwaza pia huo ndio utakuwa mwanzo wa mapinduzi ya kweli nchini Sierra Leone.
Mapigo yake ya moyo yalikimbia, jasho likamtiririka. Macho yake kama mbwa mwizi yalizunguka huku na kule akihema taratibu.
Kweli alikuwa amelala. Rose alisimama mbele ya Talib pasipo mwanaume huyo kufanya chochote, isipokuwa kukoroma. Aliutoa mkono wake uliobebea kisu nyuma ya mgongo, akaukutanisha na mwingine kushikilia mpini.
Lahaula! Kabla ya ncha ya kisu kutoboa kifua cha Talib, ghafla mkono mnene wa Taib ulidaka mikono yote miwili ya Rose. Macho mekundu ya mwanaume huyo yalitoka nje kwa namna ya kuogopesha. Mkono wake mwingine ulikwapua kisu toka kwenye mikono ya Rose, kisha ukamzaba kofi zito. Rose akarukia maili moja mbali!
“Pumbavu uliyekithiri!” Talib alilaani akinyanyuka, mkono wake wa kulia ulikuwa umebebelea kisu.
“Unadhani mimi nakufa kikondoo hivyo? Nimekwepa risasi nyingi mpaka kuwepo hapa. Mikono mingi ya wanaume ilishindwa, itaweza ya mwanamke malaya kama wewe!”
Rose hakujibu kitu. Uso wake upande wa kushoto ulikuwa mwekundu kana kwamba bendera. Kiganja na vidole vya Talib vilikuwa vimemwachia chapa ya uhakika. Macho yake yalikuwa mekundu pia mdomo wake akiubenua.
Mlinzi mmoja alifungua mlango kutazama usalama, Talib akamwagiza awahabarishe wenzake warejee kwani ameshampata mhusika. Mlinzi akafunga mlango na kutekeleza agizo.
“Sasa leo itakuwa ni siku yako ya kujifunza,” alisema Talib. “Kama mama yako alishindwa kukufunda, acha nimsaidie.”
Alivua mkanda wa sare yake ya jeshi, akaukamata mkononi. Alimtandika nao Rose kana kwamba anamchapa punda. Rose alipiga kelele kali za maumivu, ila hakuna aliyediriki kuja kumsaidia. Mfanyakazi wake aliyekuwa anatazama zoezi hilo kwa mbali aliishia kububujikwa tu na machozi. Alitamani kumkomboa lakini asingeweza kuthubutu abadani.
Mwili wa Rose ulikuwa mwekundu. Ulivijilia damu na hata kutokwa na majeraha yaliyosababishwa na chuma cha mkanda wa Talib. Hakukoma kupokea kipigo mpaka pale alipozirai. Talib alikuwa anavuja jasho kwa kazi hiyo pevu, hata pumzi yake alikuwa anahangaika kuitafuta.
“Beba katupieni jela akafie huko!” Aliagiza Talib juu ya Rose. Wanajeshi walimbeba Rose kama kiroba cha bidhaa, wakamtupia kwenye gari lao.
***
Mwanaume aliyevalia kombati nyeusi alikuwa amesimama mbele ya kundi la watu mia tatu kwa idadi ya haraka. Kichwa chake kilikuwa kimefunikwa na kiremba cheupe, uso wake ulikuwa umejawa ndevu. Mwanaume huyu, mwenye ‘ka asili’ ka uchotara wa kiarabu na ngozi nyeusi, macho yake yalikuwa makubwa na ya kutisha. Uso wake ulikuwa mgumu na wenye dhamira.
Miaka ya nyuma alikuwa mshiriki mkubwa wa mapinduzi ya Liberia akiwa na nyadhifa kubwa tu ndani ya kundi la Les Tueurs lililofanikiwa kutwaa dola ya Liberia. Ilikuwa hivyo mpaka pale alipokuja kukosana na wenzake kwa kutaka kuingiza itikadi kali za dini, hali iliyoleta mpasuko kundini.
Watu kadhaa waliomuamini na kumwona yupo sahihi walienenda naye, huku waliobakia, chini ya Al Saed, wakiendeleza harakati. Ila kabla ya kwenda, alimwachia Al Saed ujumbe mzito. Ujumbe ambao unamtesa mpaka leo hii.
Ilikuwa ni siku moja tu baada ya yeye kujiengua toka kundini kwa misingi ya dini. Siku hiyo ilikuwa ndefu mno kwa kundi la Les Tueurs kwani kwanzia alfajiri walikuwa kwenye mpambano mazito na wanajeshi wa Liberia: pambano la pili toka mwisho kuelekea kutwaa dola. Ikiwa wamepumzika toka kwenye siku hiyo ambayo iliisha kwa kupata ushindi wa mbinde, mwanaume huyu alizama kambini.
Ndani ya kambi iliyokuwa na wanaume lukuki, tena wakiwa na silaha, alipita kwa ustadi akilenga kwenda kuonana na Al Saed ndani ya hema lake lililopo katikati ya kambi. Mpaka anafika hapo hemani, alikuwa amefanikiwa kuwamaliza wanaume watano kwa kuwanyonga, hakuna aliyepiga kelele! Al Saed alijua ya kwamba amevamiwa baada tu ya zipu ya hema kufunguliwa.
“Samahani kwa kuja pasipo mwaliko,” alisema mwanaume huyu akitabasamu. Alikuwa amevalia kombati za jeshi, kwenye paja lake la kuume alining’iniza bunduki ndogo, paja lake la kushoto likibebelea kisu kirefu.
“Unataka nini kwangu?” Al Saed aliuliza. Mwanaume huyu akaketi pasipo ruhusa.
“Huu ni ujio wangu wa mwisho kwako. Baada ya hapa, ni wewe ndiye utakayekuwa unanitafuta.”
“Unataka nini kwangu?” Al Saed alirudia swali.
“Nataka kukupa nafasi ya mwisho,” mwanaume huyu akajibu. “Badili mawazo yako kabla hujakawia.”
“Ni wewe ndiye utabadili, si mimi!” alisema Al Saed kwa kujiamini kisha akaamuru;
“Toka machoni mwangu kabla sijakuvunja vipande vipande!”
Mwanaume huyu alisimama akachomoa kisu chake na kukichomeka mezani kwanguvu.
“Hili litakuwa agano langu na wewe!”
Wapambanaji wa Al Saed waligundua kwamba wamevamiwa. Walifurika mbele ya hema la kiongozi wao wakiwa wamebebelea silaha. Al Saed aliwakataza kuingia ndani. Hata pale alipomalizana kuongea na mgeni wake huyu, alitaka aachiwe aende kwa amani.
Tangu hapo alipotea, na alipokuja tena kwenye macho na masikio ya Al Saed, jina lake halikuwa Odong tena kama alivyokuwa anajulikana huko nyuma, bali Mr. X. mwanaume mwenye jeshi sasa akidhamiria kumtoa Al Saed madarakani na kuanzisha utawala wa kidini.
Mkononi mwake akiwa na silaha aina ya SMG, alitazama wapambanaji wake kama mtu achambuaye chuya toka kwenye mchele. Watu hao waliokuwa wamesimama kwa ukakamavu walivalia kombati za kijani, mkononi mwa kila mmoja kukiwa na bunduki kama ya kiongozi wao.
Mazingira yaliyokuwa yamewazunguka yalikuwa ni tulivu mno wakizingirwa na milima na miti iliyojazana kedekede. Hakika ilikuwa ni sehemu salama kwa mafunzo na makutano yao. Lakini kama vile haitoshi bado kulikuwa kuna walinzi maili kadhaa toka eneo hilo la kazi wakihakikisha usalama zaidi.
Mr. X alisafisha koo lake kisha akasema:
“Pongezi sana kwa oparesheni ya mwisho, bila shaka itakuwa salamu nzuri sana kwa makafiri!”
Wanamgambo wake wakanyoosha bunduki zao juu na kupiga kelele za kushangilia.
“Hatutakoma mpaka pale tutakapohakikisha tunawamaliza wote, na kuliweka taifa kwenye mikono ya mwenyezi Mungu! Ukae ukijua kila siku, unapokuwa vitani kupambana, haupambani kwasababu yangu; haupambani kwasababu yako; haupambani kwasababu ya wa Liberia, bali unapambana kwa sababu ya mwenyezi Mungu pekee!”
Wanamgambo wake wakanyoosha bunduki zao juu na kupiga kelele za kushangilia.
“Zawadi na malipo yetu hayapo duniani bali akhera!”
Wanamgambo wakanyoosha bunduki zao juu na kupiga kelele za kushangilia.
Baada ya kusisimuana huko, Mr. X alichukua wasaa wake kuanza kueleza mipango ya mbele, hufanya hivi kila baada ya muda fulani kwa ajili ya kuondoa sintofahamu ndani ya kundi lakini pia kutengeneza njia ya kutimiza malengo yao. Aliteua wanaume watano kwa kuwaita majina, wanaume hao kwa utiifu mkubwa wakajongea mbele kiukakamavu. Walikuwa na miili ya mazoezi na sura za kazi. miongoni mwao, ni mmoja tu aliyekuwa mfupi na mweupe, wote walikuwa wanaikimbiza anga kwa urefu na ngozi zao zikiwa nyeusi barabara.
“Siku ya keshokutwa, kuna ujio mkubwa nchini. Wanadiplomasia watano toka nchi kubwa ughaibuni watakuja kwa ajili ya kuketi meza moja na Al Saed kujadiliana kuhusu mustakabali wa nchi … nataka wanadiplomasia hao wakiwa wafu! Kwa njia na gharama yoyote ile.
Kwenye majira ya saa tisa jioni, watatua kwenye uwanja wa ndege wa Monrovia wakitokea kwenye ndege ya shirika la ndege la Delta. Siku hiyo usalama utakuwa mkubwa uwanjani hapo, hivyo mnatakiwa kuwa makini sana. Muweke vichwani kwamba sehemu pekee ya kuwamaliza wanadiplomasia hao kiurahisi ni hapo uwanjani pekee. Hivyo ni lazima wauawe siku hiyo!”
Baada ya maelezo hayo walitawanyika ila wanaume wale watano wateule waliongozana na Mr. X mpaka makaoni, chini ya msikiti. Mr. X alitoa ramani ya uwanja wa ndege toka kwenye nyaraka zake, akaitandaza mezani. Aliwaelekeza wapambanaji wake kitu cha kufanya, na namna ya kufanya kuhakikisha kila kitu kinaenda kama kilivyopangwa. Alipomaliza alimkabidhi mmojawapo ramani ile.
“Sitegemei kushindwa. Bila shaka mnajua gharama ya kushindwa.”
“Ndio, mkuu!”
“Mnaweza mkaenda.”
***
Giza liliingia kwa haraka siku hiyo, kwa sasa ilikuwa ni saa nne usiku. Ndani ya kituo walikuwepo polisi wachache sana, watatu tu kwa idadi. Polisi hao walikuwa wote wapo kaunta, wawili walikuwa wamelala mmoja akiwa anachezea simu yake kwa kuperuzi mitandaoni.
Mazingira ya kituo yalikuwa hafifu, taa moja kubwa iliyokuwa mbele ndiyo pekee ilisimama huko nje, nyuma ya kituo kulikuwa ni giza totoro. Kwa upande wa ndani, ni kaunta tu ndipo kulipokuwa na mwanga, lakini huko kwengine kwa mahabusu kulikuwa ni giza totoro. Shukrani kwa wale ambao vyumba vyao vilikuwa vinaibiaibia mwanga wa ile taa moja ya nje.
Polisi hao wakiwa hawana habari, na aidha wakiwa wanauvuta muda kutafuta siku mpya wapate kumaliza ‘shifti’ yao warudi nyumbani, mara mambo taratibu yanaanza kwenda kombo.
Sauti kubwa ya mahabusu mmoja inaita kwanguvu.
“Afandee, kuna mtu kazidiwa! Afandee!”
Polisi aliyekuwa anaperuzi alisonya na kupuuzia, wenzake hata hawakushtuka. Sauti ya mahabusu haikukoma kuita, ikaendelea kuomba msaada. Mwishowe polisi mmoja aliyekuwa usingizini akaamka kwa kufungua jicho moja.
“Kuna nini?”
“Si hao wajinga wameanza usumbufu!” Alijibu polisi anayechezea simu.
“Kawasikilize basi.”
“Siendi, sina muda huo.”
“Nenda kawasikilize bana, si unajua wakifia humo ndani huwa bonge la ishu!” aliendelea kusisitizia polisi yule akiwa anatazama kwa jicho moja asiupoteze usingizi wake.
“We nawe ni usingizi tu ndio unaokusumbua,” alilalama polisi aliyekuwa anachezea simu. “Unanisumbua tu ili ulale.”
Aliamka akaenda huko sauti ya kuitwa inapotokea. Alisimama mlangoni mwa mahabusu akatazama ndani. Kulikuwa kuna mwanga hafifu, hususani kwake kulikuwa giza totoro kwakua alitoka kwenye mwanga – wa taa na wa simu. Hivyo ikawa inamchukua muda kuona ndani.
Ghafla alijikuta amedakwa shingo, akavutwa kubamizwa kwenye nondo za mlango wa mahabusu, kang’! Akazirai. Haraka kabla hajadondoka chini, ufunguo wa mahabusu uliokuwa unaning’inia kiunoni mwake ukachomolewa, na mlango wa mahabusu ukafunguliwa upesi.
Mwanaume wa kwanza kutoka ndani, alikuwa Kone. Mkononi mwake ndiye alikuwa amebebelea funguo!
****
☆Steve