NJIA 10 ZA UHAKIKA ZA KUHARIBU MAISHA YAKO YA SASA NA YAJAYO
BISHOP DICKSON CORNEL KABIGUMILA
1. Kataa kabisa kulipa gharama ya kumjua Mungu na kutembea naye kwa uadilifu!
Daniel 11:32b, Ayubu 22:21
2. Zifanye dhambi zote hasa zinaa na uasherati kuwa kitu cha kawaida, zitende kwa bidii, jifiche kwenye kichaka cha kutubu bila kuacha na kugeuka, na hakika utayapata mavuno uyatakayo!
Warumi 6:23, Mithali 28:13
3. Kataa kabisa kuheshimu wanaokuzidi umri, matokeo na mafanikio, fanya kama vile wangechelewa ungewazidi, wadharau, waongelee vibaya waziwazi na sirini, amua kupambana nao au kuwachafua kwa uongo au ukweli, na hakika utajionea njia rahisi na ya bei nafuu ya kwenda kwenye uharibifu!
Mithali 15:20, Mithali 30:17
4. Jiambatanishe na marafiki wa ovyo, wasio na mwelekeo wa maisha na wapumbavu!
Mithali 13:20, Zaburi 1:1, 1Wakorintho 15:33
5. Tumia muda wako kiholela na kijinga kwenye vitu visivyokujenga na kukuongezea thamani, hasa vile vinavyokuburudisha tu kama movie, series, comedy, michezo nakadhalika!
Zaburi 90:12, Waefeso 5:15-16
6. Yaepuke maarifa na hekima kwa gharama zote, hakikisha huongezeki kiufahamu wala kukuza akili yako! Epuka vitabu, video za mafundisho, matukio ya kukuongezea uwezo na watu wanaojua kukuzidi!
Mithali 24:3-5, Isaya 5:13, Hosea 4:6-7
7. Fanya vita na watumishi wa Mungu hasa wale waliotumiwa na Mungu kukupa hatua kwenye nyakati fulani maishani mwako au waliotumiwa na Mungu kukuchonga na kukusaidia kuwa mtu wa maana!
Waebrania 13:17, Mithali 30:17
8. Kataa kabisa kupangilia maisha yako, goma kabisa kuwa na maono unayoyakimbiza, ishi kwa kubahatisha, subiri vitu vitokee kimiujiza bila kuwajibika!
Luka 14:28-30, Mithali 16:1, 9, Luka 12:47
9. Kataa, pinga na usiamini kabisa kwenye kulelewa, kukuzwa chini ya wengine, jiamini na nenda kafanye vitu mwenyewe kiholela na usisikilize la yeyote!
Luka 15:11-24
10. Baada ya kusoma ujumbe huu na mambo haya 9, kataa kubadilika kwenye yale uliyokuwa tayari umeharibu, baki hivyo hivyo, halafu maisha yatakulipa waziwazi sawa na upumbavu wako!
Yeremia 30:12-13
Bishop Dickson Cornel Kabigumila,
ABC GLOBAL DUNIANI
BISHOP DICKSON CORNEL KABIGUMILA
1. Kataa kabisa kulipa gharama ya kumjua Mungu na kutembea naye kwa uadilifu!
Daniel 11:32b, Ayubu 22:21
2. Zifanye dhambi zote hasa zinaa na uasherati kuwa kitu cha kawaida, zitende kwa bidii, jifiche kwenye kichaka cha kutubu bila kuacha na kugeuka, na hakika utayapata mavuno uyatakayo!
Warumi 6:23, Mithali 28:13
3. Kataa kabisa kuheshimu wanaokuzidi umri, matokeo na mafanikio, fanya kama vile wangechelewa ungewazidi, wadharau, waongelee vibaya waziwazi na sirini, amua kupambana nao au kuwachafua kwa uongo au ukweli, na hakika utajionea njia rahisi na ya bei nafuu ya kwenda kwenye uharibifu!
Mithali 15:20, Mithali 30:17
4. Jiambatanishe na marafiki wa ovyo, wasio na mwelekeo wa maisha na wapumbavu!
Mithali 13:20, Zaburi 1:1, 1Wakorintho 15:33
5. Tumia muda wako kiholela na kijinga kwenye vitu visivyokujenga na kukuongezea thamani, hasa vile vinavyokuburudisha tu kama movie, series, comedy, michezo nakadhalika!
Zaburi 90:12, Waefeso 5:15-16
6. Yaepuke maarifa na hekima kwa gharama zote, hakikisha huongezeki kiufahamu wala kukuza akili yako! Epuka vitabu, video za mafundisho, matukio ya kukuongezea uwezo na watu wanaojua kukuzidi!
Mithali 24:3-5, Isaya 5:13, Hosea 4:6-7
7. Fanya vita na watumishi wa Mungu hasa wale waliotumiwa na Mungu kukupa hatua kwenye nyakati fulani maishani mwako au waliotumiwa na Mungu kukuchonga na kukusaidia kuwa mtu wa maana!
Waebrania 13:17, Mithali 30:17
8. Kataa kabisa kupangilia maisha yako, goma kabisa kuwa na maono unayoyakimbiza, ishi kwa kubahatisha, subiri vitu vitokee kimiujiza bila kuwajibika!
Luka 14:28-30, Mithali 16:1, 9, Luka 12:47
9. Kataa, pinga na usiamini kabisa kwenye kulelewa, kukuzwa chini ya wengine, jiamini na nenda kafanye vitu mwenyewe kiholela na usisikilize la yeyote!
Luka 15:11-24
10. Baada ya kusoma ujumbe huu na mambo haya 9, kataa kubadilika kwenye yale uliyokuwa tayari umeharibu, baki hivyo hivyo, halafu maisha yatakulipa waziwazi sawa na upumbavu wako!
Yeremia 30:12-13
Bishop Dickson Cornel Kabigumila,
ABC GLOBAL DUNIANI