Nitawasilisha hoja tatu kwa chama changu CHADEMA

Yericko Nyerere

JF-Expert Member
Dec 22, 2010
16,987
20,271
Nikiwa kama mwanachama hai wa chama kinachojiandaa kushika madaraka nchini, na nikiwa mmoja ya Watanzania wanaolitazama taifa hili kama lulu ya ulimwengu, nikiwa na akili timamu, nitawasilisha hoja zangu tatu kwa chama changu Chadema ziwe agenda muhimu katika uchaguzi 2O2O.
Agenda hizo ni:

1. Mabadiliko ya mfumo wa ulinzi na usalama.

2. Uraia Pacha

3. Jamii za Wahindi na Waarabu wa Tanzania zitambuliwe rasmi na zishiriki shughuli zozote za utumishi wa nchi katika maeneo yote nyeti ya nchi.

Hoja ya kwanza nimeitafiti na kujiridhisha kwamba maendeleo ya taifa kwa vina vyote katika mlinganyo wa ulimwengu, mfumo wa vyombo hivi kwa sasa ni kikwazo kikubwa sana kufikia malengo.

Hoja ya 2. Nimejiridhisha kuwa taifa linakosa fursa na nyingi na hasa utaalamu na mitaji ya watanzania wenye uraia wa nchi nyingine kwasababu ambazo zimepitwa na wakati kwaulimwengu wa leo, Izingatiwe kuwa sababu kuu ya kuweka zuio la Watanzania walioghaibuni waliopata uraia wa nchi nyingine huko zilikuwa ni usalama hasa baada ya uhuru na kwenye harakati za ukombozi kusini mwa jangwa la sahara na katika kipindi cha Uhujumu Uchumi chini ya akina Sokoine. Sababu hizo na nyingi leo hazina mashiko....

Hoja ya tatu ni kuwa jamii hizi za wahindi na waarabu ambao ni watanzania halisi na tena kimsingi hazina uraia wa nchi zingi bali Tanzania tu, ndizo zinazochangia pato la taifa kwa ujumla kupitia mitaji yao ya uwekezaji nchini, ni jamii zilizo na wataalamu wa fani mbalimbali kama madaktari, wahandisi, na wachumi ambao leo wangeingia kwenye mifumo ya kiutumishi wa nchi kwa nyanja zote wataleta mafaa kwa taifa kuliko kukumbatia kasumba ambazo nadharia yake ni ubaguzi tu kwa raia nchini.

Ziko sababu nyingi sana za kutetea hoja zangu hizi, nitawasilisha hoja na utetezi wake naamini chama changu kitanielewa na kuzipokea hoja hizi kuwa sehemu ya agenda uchaguzi ujayo, na hazuwi agenda tu za maneno ili kujipatia ufuasi tu kama wale wenzetu 2OO5 walikuja na agenda ya OIC walipewa madaraka wakawatelekeza waliowaahidi.

Kisha 2O1O wakaja na utapeli mwingine wa Mahakama ya Kadhi, hawakutekeleza hadi 2O15, wakaja na utapeli mwingine kwamba watagawa milioni hamsini kila kijiji na watagawa laptop kila mwanafunzi wa Tanzania, matokeo yake kila mwanafunzi nchini anabeba dumu la maji na mfagio wa chelewa...

Chadema kama chama imara nchini usanii kwetu mwiko, tunaahidi unaloweza kutekeleza...!


Ili uelewe zaidi faida na hasara ya hoja hizi, soma kitabu cha Ujasusi wa Kidola na Kiuchumi.



MREJESHO;


Nimesoma maoni/hoja za watu wengi juu ya hoja zangu tatu ninazokusudia kwasilisha kwa Chama changu cha Chadema, Hoja zangu hizo ni:

1. Mabadiliko ya mfumo wa ulinzi na usalama.

2. Uraia Pacha

3. Jamii za Wahindi na Waarabu wa Tanzania zitambuliwe rasmi na zishiriki shughuli zozote za utumishi wa nchi katika maeneo yote nyeti ya nchi.

Nimeona kwamba hoja ya kwanza inakubalika bila kikwazo kwa wengi wenu mliochangia, lakini hoja ya 2 na 3 nimeona kuna michango tofauti, kumbwa zaidi hoja ya Tatu wengi hamna hoja za msingi za kuikataa zaidi ya chuki na mitazamo ya kibaguzi tu. Bado naamini hoja yangu inanguvu kuliko zenu.

Nichambue kidogo hoja ya 2 ya Uraia wa Nchi Mbili,....

Kimsingi, Hakuna sababu yoyote ya kiusalama inaweza kuwa justification ya jambo hili la Uraia wa nchi mbili, Watanzania waelewe, msingi wa jambo hili ulitumika kwakuwa baada ya Uhuru nchi yetu ilikuwa sio mwanachama wa ulinzi na usalama wa kimataifa yaani Interpol, ambayo ni polisi ya kimataifa, leo ni wanachama, hivyo hoja ya usalama kwamba wahujumu uchumi watakimbilia nchi nyingine wakishaiba ni DHAIFU na inadhihirisha ujinga na ubaguzi tulio nao kama taifa. Unaweza kujiuliza sababu za kujiunga Inter
pol ni nini ikiwa tunashindwa mambo madogo kama haya ya kudhibiti watu wetu tunaodhani watakimbilia nchi nyingine wakifanya makosa huku.

Ukweli unasimama kuwa makosa mengi yanayowakimbiza watanzania wanaoitwa wahalifu nchini ni makosa yanayotokana na sheria za kisiasa zinazopingwa na jumuiya za kimataifa kama vile sheria ya uhuru wa Habari, Sheria ya Mitandao, sheria ya vyombo vya habari na sheria ya uchochezi ambazo nyingi yazo ni sheria za kikoloni ambazo ulimwengu unazipinga...hivyo mtu aliyetenda kosa la uchochezi kwa sheria ya Tanzania, kosa hilo kwa sheria ya Marekani sio kosa na hatakamatwa na Interpol ikiwa Serikali ya Tanzania itamhitaji ili kufunguliwa kesi...

Na Yericko Nyerere

pass.jpg
 
Last edited:
Yericko Yericko !!!!
Dhana ya tatu hujaitendea haki kabisa.

Unaizungumzia kama vile hilo jina lako la mwisho umechovya yaani J.K. Nyerere hukumfuatilia au hukumuelewa kabisa hasa pale alipowapa uongozi sehemu mbalimbali hata zile sehemu au idara nyeti jamii ya hao watu uliowataja.

Hujamuelewa Nyerere mwenzio hata pale alipotoa tafsiri ya makaburu na wabaguzi.

Kama Nyerere asingefanya hicho unachojaribu kushauri leo wa Tz wangemjulia wapi Prof. Issa Shivj?

Daah nimesikitika sana jinsi ulivyo shindwa kutambua nchi yetu ilivyo wapa fursa watu wa jamii ulizozisema hasa kipindi cha Nyerere na Mwinyi muondoe huyu wa sasa ambae sio mwanasiasa au mwana diplomasia au sio mwanafalsafa kama viongozi wa awamu ya kwanza na ya pili.
 
Yericko Yericko !!!!
Dhana ya tatu hujaitendea haki kabisa.

Unaizungumzia kama vile hilo jina lako la mwisho umechovya yaani J.K. Nyerere hukumfuatilia au hukumuelewa kabisa hasa pale alipowapa uongozi sehemu mbalimbali hata zile sehemu au idara nyeti jamii ya hao watu uliowataja.

Hujamuelewa Nyerere mwenzio hata pale alipotoa tafsiri ya makaburu na wabaguzi.

Kama Nyerere asingefanya hicho unachojaribu kushauri leo wa Tz wangemjulia wapi Prof. Issa Shivj?

Daah nimesikitika sana jinsi ulivyo shindwa kutambua nchi yetu ilivyo wapa fursa watu wa jamii ulizozisema hasa kipindi cha Nyerere na Mwinyi muondoe huyu wa sasa ambae sio mwanasiasa au mwana diplomasia au sio mwanafalsafa kama viongozi wa awamu ya kwanza na ya pili.
Mkuu unaamini Shivji anaweza kuwa mfano halisi na hitimisho la hoja ya tatu????
 
Yeriko chadema kwanza haijui ulikuwa
CCM ukatimka Na Lowasa kuwinda fursa kujibu chadema haina jeshi huo ulinzi unaoongelea ni upi? Wahindi Na waarabu mbona wako wengi tu serikalini bungeni Na mahajamani? Hadi usalama wa taifa wapo unataka uandikiwe majina au? Hata chadema kullikuwa Na wagombea ubunge waarabu Na wahindi CuF ndio usiseme wako kibao Mbona wapo.Kuhusu uraia pacha sahau hakuna kitu kama hicho angalia diaspora akina Mange KIMAMBI,Evarist Chahali,ANSBERT NGURUMO wanavyotufanyia Tanzania hapo hata uraia huko waliko hawajapata.Ukiruhusu wa nchi mbili ni hatari Kwa usalama wa nchi Arab spring yote iliyosabsbisha nchi za kiarabu kupinduliwa ikiwemo Libya waliohusika ni diaspora hao wenye duo citizenship.Tanzahia sahau hayo ya uraia pacha yalishapekekwa hadi bungeni yakapigwa chini
 
Thread inayoelea ; Hakuna hitimisho linalolandana na hoja za awali;

Chadema sio chama cha kushika dola; ni kikundi cha wanasiasa wanaotafuta fursa za Ubunge tu.

Mngemsikiliza Lowasa labda mngekuwa Chama chenye lengo la kushika dola.

Ila kwa sasa mpo Katika vita ya kutetea majimbo ya ubunge Hakuna la Ziada toka Chadema.
 
Thread inayoelea ; Hakuna hitimisho linalolandana na hoja za awali;

Chadema sio chama cha kushika dola; ni kikundi cha wanasiasa wanaotafuta fursa za Ubunge tu.

Mngemsikiliza Lowasa labda mngekuwa Chama chenye lengo la kushika dola.

Ila kwa sasa mpo Katika vita ya kutetea majimbo ya ubunge Hakuna la Ziada toka Chadema.
Huyu "jasusi" uchwara Yericko Nyerere anaishi kwenye dunia ya kufikirika.
 
Huyu "jasusi" uchwara Yericko Nyerere anaishi kwenye dunia ya kufikirika.
Nikiwa kama mwanachama hai wa chama kinachojiandaa kushika madaraka nchini, na nikiwa mmoja ya Watanzania wanaolitazama taifa hili kama lulu ya ulimwengu, nikiwa na akili timamu, nitawasilisha hoja zangu tatu kwa chama changu Chadema ziwe agenda muhimu katika uchaguzi 2O2O.
Agenda hizo ni:

1. Mabadiliko ya mfumo wa ulinzi na usalama.

2. Uraia Pacha

3. Jamii za Wahindi na Waarabu wa Tanzania zitambuliwe rasmi na zishiriki shughuli zozote za utumishi wa nchi katika maeneo yote nyeti ya nchi.

Hoja ya kwanza nimeitafiti na kujiridhisha kwamba maendeleo ya taifa kwa vina vyote katika mlinganyo wa ulimwengu, mfumo wa vyombo hivi kwa sasa ni kikwazo kikubwa sana kufikia malengo.

Hoja ya 2. Nimejiridhisha kuwa taifa linakosa fursa na nyingi na hasa utaalamu na mitaji ya watanzania wenye uraia wa nchi nyingine kwasababu ambazo zimepitwa na wakati kwaulimwengu wa leo, Izingatiwe kuwa sababu kuu ya kuweka zuio la Watanzania walioghaibuni waliopata uraia wa nchi nyingine huko zilikuwa ni usalama hasa baada ya uhuru na kwenye harakati za ukombozi kusini mwa jangwa la sahara na katika kipindi cha Uhujumu Uchumi chini ya akina Sokoine. Sababu hizo na nyingi leo hazina mashiko....

Hoja ya tatu ni kuwa jamii hizi za wahindi na waarabu ambao ni watanzania halisi na tena kimsingi hazina uraia wa nchi zingi bali Tanzania tu, ndizo zinazochangia pato la taifa kwa ujumla kupitia mitaji yao ya uwekezaji nchini, ni jamii zilizo na wataalamu wa fani mbalimbali kama madaktari, wahandisi, na wachumi ambao leo wangeingia kwenye mifumo ya kiutumishi wa nchi kwa nyanja zote wataleta mafaa kwa taifa kuliko kukumbatia kasumba ambazo nadharia yake ni ubaguzi tu kwa raia nchini.

Ziko sababu nyingi sana za kutetea hoja zangu hizi, nitawasilisha hoja na utetezi wake naamini chama changu kitanielewa na kuzipokea hoja hizi kuwa sehemu ya agenda uchaguzi ujayo, na hazuwi agenda tu za maneno ili kujipatia ufuasi tu kama wale wenzetu 2OO5 walikuja na agenda ya OIC walipewa madaraka wakawatelekeza waliowaahidi.

Kisha 2O1O wakaja na utapeli mwingine wa Mahakama ya Kadhi, hawakutekeleza hadi 2O15, wakaja na utapeli mwingine kwamba watagawa milioni hamsini kila kijiji na watagawa laptop kila mwanafunzi wa Tanzania, matokeo yake kila mwanafunzi nchini anabeba dumu la maji na mfagio wa chelewa...

Chadema kama chama imara nchini usanii kwetu mwiko, tunaahidi unaloweza kutekeleza...!


Na Yericko Nyerere
hii nchi tuna tatizo kubwa sana,Yeriko umeleta hoja nzuri lakini zimeishia mipasho! Umesema ya OIC,KADHI,million 50 kila kijiji etc,nakubari kuwa siasa za Tanzania siyo za CCM au CDM wote hawaeleweki! Kuna watu walimtukana saaaana Jakaya kuwa kafeli karibu kila sekta ila Leo kwao ndo shujaa! Kuna watu(na wewe) walimtusi sana Lowasa na kumwita Fisadi BT leo ukiwauliza hawana la kusema! Mm naona CDM mnashindwa kuwa serious na mnaiga siasa za CCM ambazo mnasema zimefail so hamuwez kuiondoa ccm madarakani kirahisi. Kuweni serious,fanyeni mambo yenu bila blabla na muwe na msimamo thabiti. Rekebisheni kwanza huko ndani ili muwe na moral authority ya kuwakosoa ccm na muonekane kama mbadala wa kweli siyo mlivyo sasa hivi kama makanjanja.- peleka hizi hoja CDM ili mjirekebishe kwanza ndo tuwape nchi otherwise vyombo visipowaamini hampewi nchi hata mtembee uchi.
 
"Chadema kama chama imara nchini usanii kwetu mwiko, tunaahidi unaloweza kutekeleza...!"

Hili hitimisho lako limenichekesha sana!

Mwenyekiti wako wa taifa aliwahi kusema kama CCM itachomoka kwenye Uchaguzi Mkuu 2015 basi yeye ataachia ngazi ya Uenyekiti wa Taifa.

Leo ni July 2018 bado yupo! Kama huu sio usanii basi nadhani neno usanii lina maana nyingine.
 
Hii ni thread ya hekaya ya kusadikika..vijana kina yericko angalieni ndoto za kusimulia...si kila ndoto unayoota unasimulia watu...hivi bado ni heshima kwa Mungu kumzomea fisadi na mwizi jama lowasa, bado vibaka wa kuku wanavhomwa moto kisha lowasa anapeta tu barabarani?? Bado lowasa anastahili hata kufa kwa alichowatendea vijana wa bodaboda??
 
Nasema hiviii!!
hata cdm waje na sera nzuri kiasi gani,
kwa utawala huu watakachofanya wiki 2 za mwisho za kampeni kabla ya uchaguzi, viongozi ote watakaooneka wana nguvu watawekwa lumande na watahakikisha hawatoki hadi uchaguzi unaisha.

uchaguzi mkuu wa 2020 wapinzani ote wakipata wabunge 15 wakachinje kuku.
 
Ushawahi kuona mwafrica india anashiriki nafasi yoyote wenye siasa. Yaan I always say hiki chama kinakoelekea sio, uraia pacha wa kazi gani and tutapata faida gani na hiyo kitu zaidi mtu anaiba huku anapeleka kule kama yule waziri wa fedha alofariki ki miujiza na msiba wake hakuruhusiwa mtu kuhudhuri
 
"Chadema kama chama imara nchini usanii kwetu mwiko, tunaahidi unaloweza kutekeleza...!"

Hili hitimisho lako limenichekesha sana!

Mwenyekiti wako wa taifa aliwahi kusema kama CCM itachomoka kwenye Uchaguzi Mkuu 2015 basi yeye ataachia ngazi ya Uenyekiti wa Taifa.

Leo ni July 2018 bado yupo! Kama huu sio usanii basi nadhani neno usanii lina maana nyingine.
Kwenye ilani ya Chadema hayo maneno yameandikwa ukurasa gani ndugu?
 
Back
Top Bottom