Nitamani turudiane tena

mshai

Senior Member
Joined
Sep 10, 2014
Posts
104
Reaction score
38
Habari zenu JF

Nilikuwa na mpenzi wangu tulipendana sana. Na yeye ndo alionesha kunipenda zaidi.. Alikuwa mckivu sana na mvumilivu pia..Ilifikia wakati hawezi hata kumckiliza hata mama yake ikiwa ni kwa ajili ya kutetea penzi letu.Sio siri mimi nilijivuna kwa kupendwa kiasi kile.

Nilianza kuhisi kuwa Hawezi kuniacha kwa lolote lile.. Hata nikimuudhi kiasi gani nilijua atanisamehe tu.. Kwa mapenzi yale...Sasa nikaanza kuwa huru kupitiliza.. Nikawa si hofii tena kwa na mchepuko. Nilianzisha mahusiano na msichana wengine akiwa anajua nina mpenzi kabla yake.

Mwanzoni tuli-date kwa siri ila baadae mchepuko alianza kuona kuwa yeye Ndio anayenistahili mimi zaidi.. Basi alianza kufanya harakati za kuvunja mahusiano aliyoyakuta.. Alimtumia picha nilizopiganae.. Na hata videos tulizojirecord na txt za hapa na pale hadi alifanikiwa kupoteza mapenzi ya yule mpenzi wangu..aliniacha akaenda zake

Sasa huku nyuma nikabaki na huyu pasua kichwa.. Nilijionea tabia chafu zote niliwahi kuzickia na ambazo ckuwahi kuzickia. Mbaya zaidi tulipima afya ila bahati mbaya alikuwa ameathirika.. Na bahat nzuri kwangu ni kwamba ckuwa nimeambukizwa. Niliamua kumuacha na kurudi kuomba msamaha kwa kipenzi changu cha zamani.

Ila kwa bahati mbaya ameshachumbiwa tayari na utambulisho pia. Ila bado anasema ananipenda sana. Yupo tayari hata kuvunja uchumba na kurudi kwangu tena maana asema mimi ndio ndoto yake

Nipo njia panda ndugu zangu. Nashindwa kukubaliana na maoni yake ila moyo wangu bado unampenda sana pamoja na wivu mwingi
 
Hii umeipost kimakosa au?? mbona haiendana na maada tajwa hapo
??
 
Muache mwenzio aendelee na maisha yake. Usimchanganye. Usi-take advantage ya udhaifu wake wa kukupenda sana (naita udhaifu kwasababu wewe unautumia kama silaha). Wajibika kwa matendo yako. Anza upya. Don't manipulate her...you don't deserve her my big brother! Nisamehe kwa kuwa so blunt rafiki
 

Serious
 
niachoona hapa,,, huyo ex wako hana msimamo, wewe ni kimeo,,, coz akija kwako tabia yako iko palepale sbb ww unatumia udhaifu wake kwako kama kinga,,, nakushauri achana na binti aende na maisha yake....
 
USIMUHARIBIE MDADA WA WATU HATA KAMA KASEMA YUKO TAYAR KUFANYA HVYO MOVE FOWARD NA MAISHA MENGINE MKUU
 
Unapotezea thread za wenzio " ukifanyiwa wewe hivi ulivofanya utajiskiaje acha utoto wewe ' mbona alichoongea ni jambo ambalo lipo kabisa na linatokea katika maisha halisi
 
Baada ya miezi mitatu nenda tena kapime Ukimwi
 
Reactions: irk

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…