Nitaendelea kupinga kitendo cha TBC1 kinachoendelea kufanywa

Nitaendelea kupinga kitendo cha TBC1 kinachoendelea kufanywa

jnuswe

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2010
Posts
1,270
Reaction score
549
The media is too bias to the ruling party, habari kutoka magazetini wanakuwa na magazeti mengi , kuanza kusoma lazima waanze na habari leo then uhuru, aliyesoma habari za vichwa vya magazeti leo ni aibu tupu.

Unajua unaposoma vichwa vya magazeti ni kuwahabarisha watu wajue yaliyomo katika magazeti ya siku husika sasa inapotokea kupotosha hapo sijui taaluma ya waandishi wa habari ndivyo ilivyo au ni kupotosha maksudi.

Leo nimemfuatilia kwa karibu mchambuzi wa magazeti , amesoma jinsi mh. mkulo alivyomjibu mh. zitto kuhusiana na suala la posho za vikao, habari iliyokuwa kwenye gazeti la uhuru na habari leo mahudhui yake yalikuwa yanafanana lakini si sawa na ilivyokuwa kwenye gazeti la Mwananchi na Tanzania Daima.

Mchambuzi amenisikitisha sana ilipofika zamu ya kuchambua yaliyojiri kwenye gazeti la Mwananchi na Tanzania Daima akasema ni yaleyale tuliokwisha kusoma katika magazeti yaliyotangulia, this is no fair, you are praying a dirt game, lindeni sana taaluma yenu kuliko ushabiki, mnaogopa kufukuzwa mbona kazi zipo nyingi mahali kwingine?
 
Wala usihangaikee sana hakuna mwananchi wa kuswagwa kama ng'ombe siku hizi, pumba na mchele unafahamika. Naomba nikujuze tu TBC1 wanafanya mambo mengi sana kwa mazoea bila kuweka uwiano wa utoaji habari, ni kama umekuwaa mdomo wa serikali indirect.
 
Hi si TV ya kuangalia ni yawana wa CCM SI TENA TV ya TAIFA kama tunavyojua,watanzania wote waache kuiangalia waangalie ITV.
 
Washukuru kuwa na mitambo mizuri ambayo hata ukiwa na antenna ya Chadema unaipata vinginevyo watu ingekuwa upatikanaji wake ni shida basi tena ni ingekiuwa haitazamwi kabisa labda mkurungenzi wake, familia ya JK na wafanyakazi basi.
Ikifa na Original Komedi ndiyo itakuwa janga lingine,
 
Mkurugenzi mpya wa TBC Mshana wakati anashika hatamu za uongozi wa shirika hilo alisema habari zitakazotangazwa na chombo hicho ni zile tu zenye kuimarisha na kudumisha mshikamano wa taifa. Inavyoelekea,kwa tafsiri ya TBC habari za aina hiyo ni zile tu zinazojenga CCM na serikali yake.
 
wakati hosni mubarak alipoondolewa madarakani TV za seriakli zilikuwa live zikitangaza ushindi wake dhidi ya waandamaji kwahiyo hawa ni siafu
wanaangalia njia gani waende nao wanpelekwa huko huko utawala ukibadilika utaona nao kama majua wanacheza ngoma nyingine kwahiyo
usishangae sana kwani muda wao utakwisha siku moja.
 
Kwa bahati mbaya TBC 1 hawasomi alama za nyakati, aina ya Watanzania wa leo ni tofauti na wanavyodhani. Itawagharimu kwa kudharauliwa na wao kuonekana ovyo.
 
Mimi nilishaacha kuitazama hiyo stesheni. Natazama Mlimani TV na ITV tu
 
kpleo.jpg
 
Watatetea chama tawala,watafanya kila mbinu ionekana safi mbele za watu,watatumia nguvu za dola,watatumia hela,ila mkweli akisimama hata akiwa mmoja anaweza akasabaratisha kila ngome zao.
 
The media is too bias to the ruling party, habari kutoka magazetini wanakuwa na magazeti mengi , kuanza kusoma lazima waanze na habari leo then uhuru, aliyesoma habari za vichwa vya magazeti leo ni aibu tupu
Unajua unaposoma vichwa vya magazeti ni kuwahabarisha watu wajue yaliyomo katika magazeti ya siku husika sasa inapotokea kupotosha hapo sijui taaluma ya waandishi wa habari ndivyo ilivyo au ni kupotosha maksudi.
Leo nimemfuatilia kwa karibu mchambuzi wa magazeti , amesoma jinsi mh. mkulo alivyomjibu mh. zitto kuhusiana na suala la posho za vikao, habari iliyokuwa kwenye gazeti la uhuru na habari leo mahudhui yake yalikuwa yanafanana lakini si sawa na ilivyokuwa kwenye gazeti la Mwananchi na Tanzania Daima,
Mchambuzi amenisikitisha sana ilipofika zamu ya kuchambua yaliyojiri kwenye gazeti la Mwananchi na Tanzania Daima akasema ni yaleyale tuliokwisha kusoma katika magazeti yaliyotangulia, this is no fair, you are praying a dirt game, lindeni sana taaluma yenu kuliko ushabiki, mnaogopa kufukuzwa mbona kazi zipo nyingi mahali kwingine ?

pamoja na kuniuma kwamba inaendeshwa kwa kodi yangu, nliacha kuangalia TV hii siku nyingi sana.
 
The media is too bias to the ruling party, habari kutoka magazetini wanakuwa na magazeti mengi , kuanza kusoma lazima waanze na habari leo then uhuru, aliyesoma habari za vichwa vya magazeti leo ni aibu tupu
Unajua unaposoma vichwa vya magazeti ni kuwahabarisha watu wajue yaliyomo katika magazeti ya siku husika sasa inapotokea kupotosha hapo sijui taaluma ya waandishi wa habari ndivyo ilivyo au ni kupotosha maksudi.
Leo nimemfuatilia kwa karibu mchambuzi wa magazeti , amesoma jinsi mh. mkulo alivyomjibu mh. zitto kuhusiana na suala la posho za vikao, habari iliyokuwa kwenye gazeti la uhuru na habari leo mahudhui yake yalikuwa yanafanana lakini si sawa na ilivyokuwa kwenye gazeti la Mwananchi na Tanzania Daima,
Mchambuzi amenisikitisha sana ilipofika zamu ya kuchambua yaliyojiri kwenye gazeti la Mwananchi na Tanzania Daima akasema ni yaleyale tuliokwisha kusoma katika magazeti yaliyotangulia, this is no fair, you are praying a dirt game, lindeni sana taaluma yenu kuliko ushabiki, mnaogopa kufukuzwa mbona kazi zipo nyingi mahali kwingine ?

Hivi mtumishi wa umma anatakiwa kuwa mshabiki wa chama fulani kazini. Mbona mshana anaonyesha wazi wazi kuwa ni kada wa CCM. Mimi hii sikubali, kama hatabadilika aondolewe TBC, Tido ashike kwa muda mpaka atakapopatikana mzalendo wa kweli. Tunataka kushindana na aljazira soi redio uhuru. Hawa watu sijui wakoje utafikiri hawakwenda shule. unaipendelea CCM kwa nini hasa. aiseeee!:smash:
 
Ukiangalia TBC1 unaweza vunja kioo cha tv yako kwa hasira, acha usiiangalie, imejaa pumba na uozo kibao wa majalalani.

Binafsi niliacha kuangalia TBC (TB =kifua kikuu channel 1) muda mrefu, niliacha kusikiliza RTD-redio tanzania mwaka 1992. Niliacha kusoma magazeti ya Uhuru na Mzalendo mwaka 1982. Niliona heri kutopata habari kabisa kuliko kuendelea kudanganywa na kufanywa zezeta. TAFAKARI CHUKUA HATUA
 
tatizo lenu you just think negatively(pessimists) hamna mbele wala nyuma mnadandia tu vyombo vya habari ambavyo si vyenu km mwanahalisi,jamii forum, itv etc.siku wakiwatema na kurudi ccm mtafanyaje? anzisheni vya kwenu.....slaa tv,mbowe radio,kabwe news etc.mtafurahi eeh..............
 
tatizo lenu you just think negatively(pessimists) hamna mbele wala nyuma mnadandia tu vyombo vya habari ambavyo si vyenu km mwanahalisi,jamii forum, itv etc.siku wakiwatema na kurudi ccm mtafanyaje? anzisheni vya kwenu.....slaa tv,mbowe radio,kabwe news etc.mtafurahi eeh..............
pessimists while they are being unfair?!national tv should never be biased!think before u write! Au kwajili ni 'yakwenu' ndo maana mnafanya hivo?
 
Back
Top Bottom