Nissan X-Trail

Styvo254

JF-Expert Member
Aug 5, 2015
246
226
Vipi WanaJamii

Kwa mda mfupi nliliokua hapa nimeona wengi wakilalamika kuhusu gari hizi za Nissan. Kweli kila mtu ana haki na uhuru wa maoni/mawazo yake ni muhimu kufanya maamuzi na kua na mawazo ya ukweli na kamilifu. Kwa hili, nimeona nianzishe uzi huu ambao utakua ni wa kuhoji na kuangalia kwa kina gari hili la Nissan.

Gari hili liko kwenye toleo la tatu sasa na hii ni kudhihirisha umaarufu wake na kupendwa kwake ulimwenguni mzima. Lisingalikua zuri na bora, lisingalinunuliwa kwa wingi na kwingi hivyo. Wala sidhanii mJapan/Nissan angaliendelea kulitengeneza na kuliboresha kwa miaka karibia ishirini. Hapa hapa nchini kuna wengi wanaapa kwa hili gari na sio matani, hata uumpe gari aina nyingine na hela juu hakuskii!
Basi shida iko wapi?

Gari hili ni la kisasa na lina tumia mifumo na teknolojia ya hali ya juu. Magari haya yanauzwa soko tofauti na lazima yazingatie sheria na kanuni za nchi au maeneo husika. Mambo haya mawili ni ya muhimu sana katika kuielewa gari hili.

Kwa minajili ya usalama, kuboresha na kutofautisha chombo chao, Nissan wametumia teknolojia za kisasa kw. mf. X-Trail ya diesel yawezakua na mfumo wa DPF, huu ni wa kumaliza gesi sumu kwenye moshi wa exhaust.

Engine hii utumia oili na ratba tofauti na ya kawaida kwa matunzo yake. Gari hili laja na transmission/gearbox ya manual(sawa kabisa) na automatic aina tatu; planetary, CVT na eCVT(hapo basi baharia). Bila kusisitiza zaidi mwaona hawa ni wanyama aina tatu labda wafanane kwa kua wanafungwa kwenye engine, shaft zatoka mle na hutumia mafuta ila sio sawa.

Gari la DPF usijaribu bidhaa na mambo ya uswazi.
 
Kama Nissan au chochote cha gharama na maana, lazima uipe matunzo yaifaayo na kwa mda maalum.

Jaribu usichukue ilio na mfumo wa DPF labda uwe tayari kuipa the specialised care it needs. Pale twaweka Low Ash oil pekee, diesel toka pump za kuamini sio iliochakachuliwa, matunzo kwa fundi anayeielewa vizuri na pia ustarabu wa matumizi. Lakini ukijipata na la DPF, njoo pia tutayaganga, ki-mJapan lakini.

Kwa ufupi, sio gari baya au isiofaa Afrika ila yahitaji uelewa na makini.
 
Vipi WanaJamii
Leo tuna 'real-life situation'. Gari letu hili la X-Trail likanipata ofisini na tatizo la kelele toka blower ya Climate Control - yaani feni ya ndani au kiyoyozi kikiwashwa kunakua na kelele hasa ukipiga kona upande wa kushoto.

Gari letu lilikua limesha badilishwa blower motor na nyingine used sio zaidi ya miezi tatu iliyopita. Mmiliki gari alikua anaelewa issue ni ipi pale, wakati huu alitaka a "permanent solution". Hivyo basi alipiga simu kwa wakala na akauliza bei ya blower mpya. Aliyesema 'Pride comes before a fall' labda alikua ameshaona kwa ndoto ile arrogance ya jamaa wangu.

Alipopewa bei yake, both in dollar and Tshs na pia kiasi cha deposit required, jamaa alinywea na kaagiza Mountain Dew baridi sana! Kwa kweli hata sasa hajanidokezea aliyopata pale, bei na nini, ila tu itabidi iagizwe toka nje na itachukua wiki tano, basi tu!
Kwa problem yetu basi - ile blower ilikua imemaliza bushes zake, ndio bushes sio bearings. Design yao ni kutumia pre-greased porus bushes kabla ya bearings. Udhaifu wa hii design au bush zenyewe ni kwa mda zalika kiupande sababu ya uzito wa motor ikitembea nje ya axis of rotation sababu ya movement ya gari - kama pale inavyopiga kona.

Kwa kulielewa tatizo liko wapi na la sababishwa na nini, tuliweza kupata ile "permanent solution" mteja wetu aliyotaka. Hadi leo Climate Control yatumika kama kawaida na bila kelele yeyote.

Toleo lililofata la X-Trail linatumia blower motor design tofauti na isio na udhaifu huu. Mambo mengine hayawezi onekana kwenye design au initial stages za kifaa/chombo, lazima kipitie matumizi na mazingira mengi ili kuonekana ustadi au udhaifu wake.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu wacha niku add kwenye phone book yangu hembu fanya nipate namba yako nipo dar mm ni fundi umeme wa magari huwa nakuja sana moro..

Ishu ya nissan kwa upande wangu nilikuwa na mpango wa kuanzisha club au group la nissan.

Tena nawafanyia golo kwa watakao taka wawe wanaweza kuifanyia diagnosis popote pale watakapo kuwa dunian iki mkadi wawe na smartphone yao tuu tatizo likiwa kubwa nawapimia mm hata wakiwa nje ya nch na gari.

Juu ya dpf isikutishe sana.ukijua matumizi yake harafu wazungu sio wajinga sana dpf huwa wanaweka batan ukibonya inajisafisha yenyewe ishu ni kuwa wengi huwa hawajui na hawafanyi hivyo.

All in all solution yake ipo ikiziba inatolewa na kuidelet dpf kwenye control box mambo yana songa
 
Vipi WanaJamii
Leo tuna 'real-life situation'. Gari letu hili la X-Trail likanipata ofisini na tatizo la kelele toka blower ya Climate Control - yaani feni ya ndani au kiyoyozi kikiwashwa kunakua na kelele hasa ukipiga kona upande wa kushoto.

Gari letu lilikua limesha badilishwa blower motor na nyingine used sio zaidi ya miezi tatu iliyopita. Mmiliki gari alikua anaelewa issue ni ipi pale, wakati huu alitaka a "permanent solution". Hivyo basi alipiga simu kwa wakala na akauliza bei ya blower mpya. Aliyesema 'Pride comes before a fall' labda alikua ameshaona kwa ndoto ile arrogance ya jamaa wangu.

Alipopewa bei yake, both in dollar and Tshs na pia kiasi cha deposit required, jamaa alinywea na kaagiza Mountain Dew baridi sana! Kwa kweli hata sasa hajanidokezea aliyopata pale, bei na nini, ila tu itabidi iagizwe toka nje na itachukua wiki tano, basi tu!
Kwa problem yetu basi - ile blower ilikua imemaliza bushes zake, ndio bushes sio bearings. Design yao ni kutumia pre-greased porus bushes kabla ya bearings. Udhaifu wa hii design au bush zenyewe ni kwa mda zalika kiupande sababu ya uzito wa motor ikitembea nje ya axis of rotation sababu ya movement ya gari - kama pale inavyopiga kona.

Kwa kulielewa tatizo liko wapi na la sababishwa na nini, tuliweza kupata ile "permanent solution" mteja wetu aliyotaka. Hadi leo Climate Control yatumika kama kawaida na bila kelele yeyote.

Toleo lililofata la X-Trail linatumia blower motor design tofauti na isio na udhaifu huu. Mambo mengine hayawezi onekana kwenye design au initial stages za kifaa/chombo, lazima kipitie matumizi na mazingira mengi ili kuonekana ustadi au udhaifu wake.


Sent using Jamii Forums mobile app
Hbr za masiku WanaJF
Siku mingi sija changia uzi, mtanisamehe ila shughuli na kazi zinabana.
Leo nimeipata Xtrail ya petrol imesumbua kwa mda. 'Wasanii wameipigia show'; cat converter wameitoa matumbo, oxygen sensor wamebadilisha, head wameng'oa na mambo mengine mengi.
La kwanza kufanya pale ni kukagua 'vital parameters' kwa engine kama vile oili, air filter na kadhalika. Niligundua oili imechoka kweli na nyeusi sana - kumbuka gari lilikua kwa fundi siku tatu awali. Hili lilieleza mambo/observations flani nilipo liwasha gari. Engine Idle Speed ilikua juu na haijatulia; 900-970 rpm, exhaust ilinukia rich sana na mengine.
Diagnosis report ilitoa code zifatazo: P0172- fuel trim, too rich
P0120- throttle position sensor
P1123- ETC motor control circuit; mambo haya matatu yanahusu mfumo wa mafuta - fuel system. Observations zetu pale tulipoliwasha gari ziliashiria haya lakini bila kuyapata 'from the horses mouth' hakuna uhakika ila ni kukisia tu.
Bila kuongea mengi kuhusu ufundi au ujuzi wa mafundi, taratibu na itikadi za kiufundi ni muhimu kuzingatiwa. Mambo ya msingi kama kubadilisha oili na filter yana adhiri utendakazi wa engine na mifumo mingine. Ni wazi kwa kila mtu kua oili ulainisha vyuma na sehemu kwenye mfumo. Utelezi huu unahitajika kurahisisha mizunguko na kadhalika
Ubora/property hizi upotea oili inavyozeeka au inavyotumika kwenye mfumo - iwe engine, gearbox(manual au auto), diff, pump za hydraulic na pia compressors. Utapata unavyokaa na oili chafu kwenye mfumo, mfumo unapata uzito mkubwa na hapo kuhitaji nguvu zaidi kuendeleza mzunguko.
Zoezi la marekebisho kwa hili gari litaanzia na kuifanya engine service ndio tufanye tune-up ya mfumo wa mafuta. Ni muhimu kuelewa kua mifumo ya computer imewezeshwa kusoma, kusahihisha na pia kutarajia mabadiliko/mapungufu flani kwa ajili ya kuzeeka au mazingira.
Bila kujua hili, 'adaptation' za kawaida za mfumo zaweza chukuliwa kama matatizo na pale 'fundi' akaliharibu gari. Itaeleweka pia mambo haya yanafanyika kwa/na mitambo ya umeme. Mawasiliano yanategemea na kulingana na misingi flani ya kiufundi, kilele chake hua ni pale mtu anapotumia mfumo wa muunda gari - OEM, unaposhuka ngazi ndio mawasiliano yanavyokua ya kubahatisha.
Unapohisi gari/engine ina behave tofauti, ebu jiulize service iko due au kama ni baada yake, ni kipi kilichobadili kwa zoezi.
Pamoja!



Sent using Jamii Forums mobile app
 
6c08da2929d1561108531a903212483c.jpg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Daaa mkuu nakuelewa sana.sio kule jamaa check engine imewaka anasema kifuniko cha tanki.
Hbr za masiku WanaJF
Siku mingi sija changia uzi, mtanisamehe ila shughuli na kazi zinabana.
Leo nimeipata Xtrail ya petrol imesumbua kwa mda. 'Wasanii wameipigia show'; cat converter wameitoa matumbo, oxygen sensor wamebadilisha, head wameng'oa na mambo mengine mengi.
La kwanza kufanya pale ni kukagua 'vital parameters' kwa engine kama vile oili, air filter na kadhalika. Niligundua oili imechoka kweli na nyeusi sana - kumbuka gari lilikua kwa fundi siku tatu awali. Hili lilieleza mambo/observations flani nilipo liwasha gari. Engine Idle Speed ilikua juu na haijatulia; 900-970 rpm, exhaust ilinukia rich sana na mengine.
Diagnosis report ilitoa code zifatazo: P0172- fuel trim, too rich
P0120- throttle position sensor
P1123- ETC motor control circuit; mambo haya matatu yanahusu mfumo wa mafuta - fuel system. Observations zetu pale tulipoliwasha gari ziliashiria haya lakini bila kuyapata 'from the horses mouth' hakuna uhakika ila ni kukisia tu.
Bila kuongea mengi kuhusu ufundi au ujuzi wa mafundi, taratibu na itikadi za kiufundi ni muhimu kuzingatiwa. Mambo ya msingi kama kubadilisha oili na filter yana adhiri utendakazi wa engine na mifumo mingine. Ni wazi kwa kila mtu kua oili ulainisha vyuma na sehemu kwenye mfumo. Utelezi huu unahitajika kurahisisha mizunguko na kadhalika
Ubora/property hizi upotea oili inavyozeeka au inavyotumika kwenye mfumo - iwe engine, gearbox(manual au auto), diff, pump za hydraulic na pia compressors. Utapata unavyokaa na oili chafu kwenye mfumo, mfumo unapata uzito mkubwa na hapo kuhitaji nguvu zaidi kuendeleza mzunguko.
Zoezi la marekebisho kwa hili gari litaanzia na kuifanya engine service ndio tufanye tune-up ya mfumo wa mafuta. Ni muhimu kuelewa kua mifumo ya computer imewezeshwa kusoma, kusahihisha na pia kutarajia mabadiliko/mapungufu flani kwa ajili ya kuzeeka au mazingira.
Bila kujua hili, 'adaptation' za kawaida za mfumo zaweza chukuliwa kama matatizo na pale 'fundi' akaliharibu gari. Itaeleweka pia mambo haya yanafanyika kwa/na mitambo ya umeme. Mawasiliano yanategemea na kulingana na misingi flani ya kiufundi, kilele chake hua ni pale mtu anapotumia mfumo wa muunda gari - OEM, unaposhuka ngazi ndio mawasiliano yanavyokua ya kubahatisha.
Unapohisi gari/engine ina behave tofauti, ebu jiulize service iko due au kama ni baada yake, ni kipi kilichobadili kwa zoezi.
Pamoja!



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Vipi WanaJamii

Kwa mda mfupi nliliokua hapa nimeona wengi wakilalamika kuhusu gari hizi za Nissan. Kweli kila mtu ana haki na uhuru wa maoni/mawazo yake ni muhimu kufanya maamuzi na kua na mawazo ya ukweli na kamilifu. Kwa hili, nimeona nianzishe uzi huu ambao utakua ni wa kuhoji na kuangalia kwa kina gari hili la Nissan.

Gari hili liko kwenye toleo la tatu sasa na hii ni kudhihirisha umaarufu wake na kupendwa kwake ulimwenguni mzima. Lisingalikua zuri na bora, lisingalinunuliwa kwa wingi na kwingi hivyo. Wala sidhanii mJapan/Nissan angaliendelea kulitengeneza na kuliboresha kwa miaka karibia ishirini. Hapa hapa nchini kuna wengi wanaapa kwa hili gari na sio matani, hata uumpe gari aina nyingine na hela juu hakuskii!
Basi shida iko wapi?

Gari hili ni la kisasa na lina tumia mifumo na teknolojia ya hali ya juu. Magari haya yanauzwa soko tofauti na lazima yazingatie sheria na kanuni za nchi au maeneo husika. Mambo haya mawili ni ya muhimu sana katika kuielewa gari hili.

Kwa minajili ya usalama, kuboresha na kutofautisha chombo chao, Nissan wametumia teknolojia za kisasa kw. mf. X-Trail ya diesel yawezakua na mfumo wa DPF, huu ni wa kumaliza gesi sumu kwenye moshi wa exhaust.

Engine hii utumia oili na ratba tofauti na ya kawaida kwa matunzo yake. Gari hili laja na transmission/gearbox ya manual(sawa kabisa) na automatic aina tatu; planetary, CVT na eCVT(hapo basi baharia). Bila kusisitiza zaidi mwaona hawa ni wanyama aina tatu labda wafanane kwa kua wanafungwa kwenye engine, shaft zatoka mle na hutumia mafuta ila sio sawa.

Gari la DPF usijaribu bidhaa na mambo ya uswazi.
Nikajua post yako ipo technical, ila na ww umekuja kuleta hisia zako. Basi sawa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hbr za masiku WanaJF
Siku mingi sija changia uzi, mtanisamehe ila shughuli na kazi zinabana.
Leo nimeipata Xtrail ya petrol imesumbua kwa mda. 'Wasanii wameipigia show'; cat converter wameitoa matumbo, oxygen sensor wamebadilisha, head wameng'oa na mambo mengine mengi.
La kwanza kufanya pale ni kukagua 'vital parameters' kwa engine kama vile oili, air filter na kadhalika. Niligundua oili imechoka kweli na nyeusi sana - kumbuka gari lilikua kwa fundi siku tatu awali. Hili lilieleza mambo/observations flani nilipo liwasha gari. Engine Idle Speed ilikua juu na haijatulia; 900-970 rpm, exhaust ilinukia rich sana na mengine.
Diagnosis report ilitoa code zifatazo: P0172- fuel trim, too rich
P0120- throttle position sensor
P1123- ETC motor control circuit; mambo haya matatu yanahusu mfumo wa mafuta - fuel system. Observations zetu pale tulipoliwasha gari ziliashiria haya lakini bila kuyapata 'from the horses mouth' hakuna uhakika ila ni kukisia tu.
Bila kuongea mengi kuhusu ufundi au ujuzi wa mafundi, taratibu na itikadi za kiufundi ni muhimu kuzingatiwa. Mambo ya msingi kama kubadilisha oili na filter yana adhiri utendakazi wa engine na mifumo mingine. Ni wazi kwa kila mtu kua oili ulainisha vyuma na sehemu kwenye mfumo. Utelezi huu unahitajika kurahisisha mizunguko na kadhalika
Ubora/property hizi upotea oili inavyozeeka au inavyotumika kwenye mfumo - iwe engine, gearbox(manual au auto), diff, pump za hydraulic na pia compressors. Utapata unavyokaa na oili chafu kwenye mfumo, mfumo unapata uzito mkubwa na hapo kuhitaji nguvu zaidi kuendeleza mzunguko.
Zoezi la marekebisho kwa hili gari litaanzia na kuifanya engine service ndio tufanye tune-up ya mfumo wa mafuta. Ni muhimu kuelewa kua mifumo ya computer imewezeshwa kusoma, kusahihisha na pia kutarajia mabadiliko/mapungufu flani kwa ajili ya kuzeeka au mazingira.
Bila kujua hili, 'adaptation' za kawaida za mfumo zaweza chukuliwa kama matatizo na pale 'fundi' akaliharibu gari. Itaeleweka pia mambo haya yanafanyika kwa/na mitambo ya umeme. Mawasiliano yanategemea na kulingana na misingi flani ya kiufundi, kilele chake hua ni pale mtu anapotumia mfumo wa muunda gari - OEM, unaposhuka ngazi ndio mawasiliano yanavyokua ya kubahatisha.
Unapohisi gari/engine ina behave tofauti, ebu jiulize service iko due au kama ni baada yake, ni kipi kilichobadili kwa zoezi.
Pamoja!



Sent using Jamii Forums mobile app
Leo pia gari limerudi limewasha MIL. Baada ya kuisoma code tumepata ni zile zile za jana.
Tukiangalia exhaust ya gari, ina kosa CAT converter na kuleta shida mbili, kwanza zile gesi zinapita kwa kasi kubwa sana na kwa hivyo Oxygen sensor zinaashindwa kusahihisha air/fuel mixture vizuri, pili, bila kuchuja au convert zile gesi, mfumo unapata taarifa zisizoeleweka kuhusu jiko/combustion.
Baada ya kubadilisha oili, gari ilitulia kiasi. Wacha tuitaftie CAT converter yake halafu twende kutoka hapo.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom