Nishaurini nifanye nini?

Hakikisha mama mkwe asijue kama ulikuwa utani. Maana the whole thing itaonekana ni upuuzi na na wenyewe utaonekama mswahili. unaweza poteza imani kwa hao watu. Wanaweza wasikuambie wazi. But that thing will be in their mind forever.
Solution wewe mtafute jamaa mtengeneze mimba. Hamna cha zaidi ya hapo. Sacrifice kazi kwa kipindi hiki, bt kama uko serious na relation yako
 
Usijali nitakuombea ila nawe ujiombee,
Cha kufanya piga hesabu zako vizuri ili uvizie siku muafaka ya kupata mimba na usifanye makosa kbs,
Yani ikiwezekana km jamaa yuko mbali msafirie umfate huko huko!

Hapa MUNGU hatawasikia msidanganyane. Hata ukitubu MUNGU lazima akuadhibu.
Biblia ina sema: WATU WANGU WANAANGAMIZWA KWA KUKOSA MAARIFA.
hapa sio maombi ni maarifa
 
Nilitaman iwe hivyo ila sasa naona kama siku za kupata uwo ujauzito nao nitakuwa kazini kwan nipo mbali nae.

Ila ntajaribu kufanya hivyo kama nikipta ujauzito nitashukuru sana Mungu.

kama uliweza kumdanganya imo wakati haimo fanya hivyo hivyo mwezi huu ukiwa kwenye joto tutafutane tuoteshe kitu....jamaa atalea hana shida....angalizo mbona wakwe wanashabikia sana isijekuwa wanajua mtoto wao alikuwa kimeo ndo kabahatisha imeingia kwako!!!
 
dada cha msingi hapo cha kufanya ni kujifanya hata bado huamini kama una mimba jifanye unataka kwenda tena ukahakikishe kama unayo hiyo mimba ikiwezekana mchukue huyo boyfriend wako muende wote halafu mnaenda wote kupima na mkifika kule itaonekana hauna na yeye atashuhudia halafu unajifanya kumuuliza docta ni kwanin mbona nilipima juz juz tu nilionekana ninayo>?hii ni kwa kulinda penzi lako dada,,,,,mdau
 
swala la msing dada unaogopa wakijua ukweli watahairisha kuja kwenu au unaogopa kumuumiza mchumba wako? kama unaogopa kumuumiza mchumba then jitegeshe upate mimba mambo yaendelee, kama unaogopa watahairisha kuja kujitambulisha basi jua wazi humpendi huyo mwanaume ila upo desperate na ndoa
 
Labda nikuulize ulimdanganya ulienda kupima muda gani baada ya kukutana nae??
 
Na akiulizwa na mchumba ni hospitali gani alieenda akakutwa nayo?vyeti vikowapi? na wakatakiwa kwenda wote kuhakikisha tena kwa siku na muda atakao utaka mchumba?bila bishost kuambiwa ni lini n saa ngap itakuwaje?bidada unayo hela ya kuwahonga madocta wa hospitali yote utakayoitaja ili wakutetee?na tena wakukumbuke maana mchumba kama ni mwerevu anaweza kujifanya ***** kwa sasa halafu siku akakusuprize kwamba muende huko hospitali,ukizingatia madocta wenyewe wengi walevi,halafu utawaaminije kwamba watakutunzia siri yako??binaadam hao ujue...wengine ni watu na wengine viatu..
 
dada cha msingi hapo cha kufanya ni kujifanya hata bado huamini kama una mimba jifanye unataka kwenda tena ukahakikishe kama unayo hiyo mimba ikiwezekana mchukue huyo boyfriend wako muende wote halafu mnaenda wote kupima na mkifika kule itaonekana hauna na yeye atashuhudia halafu unajifanya kumuuliza docta ni kwanin mbona nilipima juz juz tu nilionekana ninayo>?hii ni kwa kulinda penzi lako dada,,,,,mdau



Na akiulizwa na mchumba ni hospitali gani alieenda akakutwa nayo?vyeti vikowapi? na wakatakiwa kwenda wote kuhakikisha tena kwa siku na muda atakao utaka mchumba?bila bishost kuambiwa ni lini n saa ngap itakuwaje?bidada unayo hela ya kuwahonga madocta wa hospitali yote utakayoitaja ili wakutetee?na tena wakukumbuke maana mchumba kama ni mwerevu anaweza kujifanya ***** kwa sasa halafu siku akakusuprize kwamba muende huko hospitali,ukizingatia madocta wenyewe wengi walevi,halafu utawaaminije kwamba watakutunzia siri yako??binaadam hao ujue...wengine ni watu na wengine viatu..
 
Mweleze jamaa ukweli ili ashiriki uongo pamoja nawe.Itakuwa mbaya kwa muda mrefu kuwaeleza jamaa wote kwenye hii picha kuwa ulikuwa unatesti upendo.Bora ukubaliane na mwenzio muweze singizia kuwa mimba imepolochoka.Otherwise it is suicidal to tell the truth to all the people you mentioned.JIFUNZE SANA BAADA YA HAPA!
 
Hodi humu ndani! Salamu wote wana Jamii Forum. Nianaomba msaada jamani.
MM nina Boyfriend wangu tumedumu kwa mwaka mmoja, tunapendana sana, na anaonyesha jitihada za kuwa na mm kama mke na mume, ameshanitambulisha kwa Mama yake, Dada zake na Kaka zake ila kwa kutumia simu kwan kwao ni mbali na tunapofanyia kazi kwahiyo umbali umechangia kuto onana face to face. Mara nyingi ndugu zake hao huwa wananipigia simu tunawasaliana na mm pia huwa nawapigia simu.
Mpaka hapo Mama yake anaonyesha upendo mkubwa sana wa mimi kuendelea kuwa na kijana wao. Ndugu wakinipigia simu wanakuwa wanani sihi sana kutulia na kumpenda kijana wao kwa moyo wote. Na mimi ki ukweli ninampenda sana kijana wao.
Week mbili zilizopita tulikutana kimwili na huyu Boyfriend wangu ambaye kwa sasa ni Mchumba mtarajiwa.. Baada ya siku kama tatu nikataka kumpima kama kweli anaupendo wa dhati kwangu au ni mambo ya ujana tu, nikamwambia nahisi kama nimepata ujauzito, kijana wa watu akaonyesha kufurahishwa sana na kauli ile akaniomba niende kupima ili niwe na uhakika kwan tupo wilaya tofauti hatuonani mara kwa mara, nikamwambia sawa nitaenda kupima, kesho yake nikampa majibu kuwa ni kweli nimepima na ninaujauzito. NILIKUWA NAMTANIA. Akaniambia sasa upendo wake kwangu umeongezeka mara dufu kwani anaamini nitakuwa mke wake.
Akampigia mama yake simu akamueleza juu ya jambo hilo na mama yake akamwambia basi hakuna shida atawaeleza baba zake wadogo ili wajiandae waje kwetu kutoa posa na taratibu nyingine za uchumba zifanyike ili tuoane mapema iwezekanavyo. Nikapigiwa simu na Mama yake akaniambia hongera mwanangu nimepewa taarifa zote na Mchumba wako kwa hiyo naomba usiogope sisi tunashughulikia swala la kuja huko kwenu.. Nilishtuka sana kwan Mchumba alikuwa ajaniambia kama amemwambia mama yake.
Na mimi nikamsikiliza mama yake mpaka mwisho. Swali langu je nimwambie mchumba kuwa nilikuwa namtania sina ujauzito? Na je atanichukuliaje? Na je wanaweza kusitisha zoezi la kwenda kujitambulisha nyumbani? Na mama yake atanionaje mimi? Nisaidieni mawazo ndugu yenu ntaumbuka mimi.
NB. Nilimtania ili kujua atachukua hatua gani baada yakujua mm ni mjamzito.
Ushauri wenu ndio silaha ya kuokoa ndoa hii itarajiwayo. Na Mungu atawabariki.

Huyo Boi frendi kichwa maji kweli, mmekutana peku peku kwa mara ya kwanza, ndani ya siku tatu anaamimi kuwa umepata mimba? nae atakuwa anakutania huyo..mimba ya baada ya siku tatu ya tendo la ndoa umeipimia nini?
 
Uongo ni uongo tu,na utabaki kuwa uongo,na hiyo itakusumbua konshas yako mpaka umweleze ukweli mwenza wako,na kwa nini ufanye masihara kwa mambo kama hayo?perhaps mwenzako yuko desperate kupata mtoto,weee vipiiiii?hebu tubu haraka alaaa
 
Mweleze jamaa ukweli ili ashiriki uongo pamoja nawe.Itakuwa mbaya kwa muda mrefu kuwaeleza jamaa wote kwenye hii picha kuwa ulikuwa unatesti upendo.Bora ukubaliane na mwenzio muweze singizia kuwa mimba imepolochoka.Otherwise it is suicidal to tell the truth to all the people you mentioned.JIFUNZE SANA BAADA YA HAPA!

Yeah wewe umesoma mawazo yangu kabisaaaaaaaaaaaaa na kwa kuongezea bi shost ajue vyovyote itakavyokuwa ameshateteresha mapenzi lake,wanaume hawajaribiwi kwa style kama hizo,jiandae kabisa kwa yote ikiwemo kupungua kabisa kwa upendo,na wewe ndio ukomae sasa kuhakikisha haumpotezi kabisa huyo mchumba,jipendekeze na ongeza molovedave hata kam yeye atayapungza na mshawishi kuwa unajutia kosa lako na hutakaa ulirudie
ohoooooooo nilitaka kusahau tengeneza mazingira mazuri ya kumwambia usikurupuke tu na ni vizuri ukamwambia mkionana face 2 face,jitahidi uonane nae mapema iwezekanavyo kuweka mambo sawa.....pole shost ila ndio usirudie tena yaan ukomage...
 
Halafu hivi ukidanganya mimba imetoka,halafu ukaolewa den usipate mtoto...itakuwaje?ukaenda hospital mkaambiwa wewe hauna uzazi kabisa huwezi kuzaa unafikiri utaeleweka kwa mumee n familia??na pia vipi kama ikaja tokea jamaa yeye ndiye mwenye matatizo akaambiwa hana uwezo wa kumpa mtu mimba,unadhani mtaelewana??
 
Nimecheka peke yangu, kweli hii ni jamii forums hakuna kinachoshindikana kwa ma-greater thinkers, TrueLove upo hapa?

Wewe kichwa maji kabisa jambo dogo hivyo. Mwambie hivi unaumwa tumbo, na baadaye neda kaongee na dokta akuandikie cheti kuwa mimba imetoka la sivyo, your going to die.

Mwambie ulikuwa kenye daladala watu wakakubana vilivyo, wakambana mtoto tumboni na mimba imetoka.

Baada ya hapo nenda Kanisani au Msikitini ukatubu

Byeeeeeeee
 
wanaweza wasisitishe au wakasitisha mambo ya ndoa, ila wasopositisha, imani itakua imepotea kabisa kwani uongo uliotumia ni mkubwa sana. hukupaswa kusubiri hata masaa mawili yapite kabla ya kumwambia unamtania. sasa umesubiri siku zinazidi kwenda na uinaomba hapa ushauri ili sijui tukuambie nini. kipimo cha upendo anacho mtu mwenyewe. wewe kama wewe huna kipimo cha kupima kua eti unapendwa kiasi gani... huo ni upuuzi ukioufanya. omba mungu uwe na kizazi cha karibu, ushike mimba mapema, kama kizazi kiko mbali, utajuta... pole sana, na iwe mwisho kutania kama utani huuwezi.
 
Jamani usinitusi... majuto mjukuu... ndo nimeona uzembe wangu sitorudia tena siku nyingine. Asante kwa ushauri.


KILAZA kweli ww!! siku ya mwanzo ulivyomwambia si uliona reaction yake? sasa ulivyopima ulitaka riaction ipi ya zaid!! badala ndio ungemwambia umepima umekuta huna ....... kama jamaa yako yupo mbali njoo mimi nipo karibu nikusidie kutengeneza mtoto wa kiukweli.
 
Baada ya kugundua kuwa umekosea na umeikosea familia nzima, mi nadhani ni jambo la busara kumwambia huyo kaka ukweli tena mwambie mapema. Koz unaweza kujifanya ati uende kwake siku za kushika mimba na ukashangaa isishike na ukawa unaongeza tatizo. Na siku zote Mungu akitaka kukufichua hakuna kichaka utakachojificha usionekane.

Ukweli tu ndio utakaokusaidia hapo na sio kuongeza uongo juu ya mwengine.
 
kila kona MAPENZI, watu kibao MAPENZI. wat is this?


:focus:
swahiba angalia sana kuna kitu kinaweza kusmell bad in your relationship,
1 -kuna mchangiaji kasema jiuguze then ujifanye imetoka..... sawa utawaeleza watakuelewa sasa issue itakuja mtakapooana alafu accidentally ikajulikana wewe huwezi zaa au jamaa ni infertility. apo tayari ni hatari tupu.

2 -mcahngiaji mwingine kakushauri fanya juu chini akupe mimba katika hii miezi miwili...... apo naona ndo the best option, ata kama umesema thoz days atakuwa kazini jitahidi umfuate na umuonyeshe kwamba umemimiss sana na uongo kibao wa kike hope hatashangaa wewe kumfuata huko kazini kwake.


3== all in all soma comments zetu then changanya na zako fanya maamuzi, kumbuka mapenzi hayashauriki ila muamuzi ni wewe mwenyewe.:A S 465:
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom