Nishauri tafadhali niokoe ndoa yangu

Nishauri tafadhali niokoe ndoa yangu

sifa

Member
Joined
Sep 15, 2009
Posts
19
Reaction score
2
Wana MMU salamu kwenu. Niko kwenye ndoa miaka miwili tuu sasa lakini naona ndoa inataka kuwa ya majonzi kwangu.
Kabla na baada ya kuoana na mume wangu maisha yalikuwa poa sana na tendo la ndoa ambalo tulianza kufanya hata kabla ya kuoana ilikuwa poa ttuu na wakati mwingine tulikuwa tunafanya hadi nahisi moto unaniwakia. Mume wangu ana matatizo ya kifua kuna kipindi aliugua sana akaanza kuchoma sindano zinaitwa DIPROFOS kwa kweli hali ikawa shwari kila kikiamka anachoma kinatulia tena kwa muda mrefu. wakati huohuo nilianza kuona mabadiliko kwa mume wangu kwani alianza kupoteza hamu ya tendo la ndoa twaweza kaa hadi wiki 2 haulizi chochote hadi nilianzishe. wakati huohuo tukifanya basi dakika mbili hadi 3 ashamaliza na yuko hoi na kurudia haiwezekani. Na pia nilihisi mabadiliko na ile kitu ilikuwa imekuwa kibamia ha ikisimama haifiki popote. Kwa kweli niliona napata tabu kwani nilianza kuhisi upweke na kukosa raha nikaamua kuvunja ukimya. Mume wangu alilia hio siku hiyo na kuniambia na yeye alikaa na kutafakari na kugundua tatizo lilianza alipoanza kuchoma zile sindano.Binafsi sikuwahi kufikiri chanzo chaweza kuwa hizo sindano. Nilimtuliza tukakubaliana tutaenda kumwona Dr. kabla ya kwenda alimwona Dr fulani akiwa peke yake na kumwelezea yule Dr akamwambia ndio madhara ya zile sindano hivyo aache kuzitumia na baada ya muda mambo yatarejea kama mwanzo. Alirudi nyumbani naa kunieleza baada ya hapo habari ya kwenda wote hsptl ikaishia hapo. Ni muda sasa umepita lakini hali bado ni ileile, nimejikuta nakosa raha na silali usiku kwa mawazo. nina kila kitu ninachohitaji lakini swala la mume wangu linanipa wakati mgumu sana. Tafadhali kwa yeyote anayeelewa kuhusu hizo injection anijuze, na pia nahitaji ushauri wenu. Nampenda sana mume wangu nahitaji kuwa na furaha na yeye pia afurahi. Please advice
 
mumeo anahitaji support yako.

Zungumza nae kuhusu hiyo sindano

Andamaneni pamoja hospitali mpate ushauri pamoja na mbadala wa dawa ikibidi

Mjengee confidence mumeo na ongeza muda wa romance kabla ya kuingiza dudu

Ukisikia for better for worse ndo hiyo.....
 
pole sana,mwombee atapona
 
Pole sana kwa yanayo wakuta. Kama wewe unajiskia vibaya amini mume wako nae anajiskia vibaya, maybe even worse than you, hivo hakikisha kua mnapo ongelea hili swali you dont make him feel guilty sababu hakufanya kusudi.
Nadhani cha kufanya hapo ni kwenda PAMOJA kuonana na daktari na kutafuta origin ya mapungufu hayo ni nini. Maybe huyo daktari wa kwanza alisema ni hizo sindano but sio? Inaweza kua ni ugonjwa mngine, au miaka, au hata huo ugonjwa unao mfanya apewe hizo sindano ndio umeaffect na uwezo wake wa ku-sex.
As mnatafuta sababu na suluhisho you people need to adapt. usiangaalie nyuma na kusema there was a time, there was a day... Just accept the situation kwanza kua sasa itakua ni hivo hadi pale mtakapo pata solution. develop other means to get satisfied kwanza. Be creative (both of you).
 
mumeo anahitaji support yako.

Zungumza nae kuhusu hiyo sindano

Andamaneni pamoja hospitali mpate ushauri pamoja na mbadala wa dawa ikibidi

Mjengee confidence mumeo na ongeza muda wa romance kabla ya kuingiza dudu

Ukisikia for better for worse ndo hiyo.....
nadhani ni ushauri mzuri tu ufanyie kazi na usishawishike kutoka nje ya ndoa maana utammaliza kabisha huyo mmeo
 
hiyo ndo kwa shida na raha, mpende sana mumeo na jifunzeni jinsi ya kutumia shortcut kuridhishana kabla ya kupata suluhu. Halafu usiwaze sana japo inaumiza bt amini mumeo anakupenda na anatamani kukuridhisha ila hali ndo hivyo. Ngono ni muhimu ila si kila kitu kwenye maisha. Mungu akupiganie na usali sana.
 
Pole ...utakuwa na wakati mgumu kwa kuwa ndoa ni changa...ila kama mlipendana kwa dhati jaribu kumfanya rafiki na ondoa mawazo kwenye ku do...kuna lots of ways za kufurahia maisha kama marafiki zaidi ya ku do...but if ndoa yenu haikuwa ile ya 'lazima nioe/niolewe'

otherwise kama unataka kujua madhara ya hiyo sindano; (hata mimi ningetaka kujua) kwa nini usi google tu? Ma doctor wenyewe wana google hayo wanayotuambia...na kwa kuwa wana wagonjwa lukuki hata tukiwa consult wanatupa taharifa kidunchu tuuuu...google upate full data
 
mumeo anahitaji support yako.

Zungumza nae kuhusu hiyo sindano

Andamaneni pamoja hospitali mpate ushauri pamoja na mbadala wa dawa ikibidi

Mjengee confidence mumeo na ongeza muda wa romance kabla ya kuingiza dudu

Ukisikia for better for worse ndo hiyo.....

Kweli apunguze ubinafsi, maana kama yeye anaumia basi mume anaumia mara 2 yake ndio maana akadondosha na machozi; si unajua ego za wanaume zimelala pale zaidi. Mbona sisi ambao tupo tupo twaweza piga hata mwaka bila ngono na tunaishi; hiyo sio chakula kwamba usipopata utakufa.
Anyway, do what your heart tells you.
 
Back
Top Bottom