Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 42,241
- 33,002
Mkuu Solarpanelninakuongezea ujuzi mwengine akufanyie mume wako nao ni hivi:Asante sana mzizi mkuu kwa ushauri mzur,mengi ya hayo ananifanyia mume wangu,ila nimetek point kuwa mengine nimuoneshe nitaufanyia kaz na nitaleta fidbak hapa....kana loh nilisema naomba ushaur sahihi huo wa kwako ni wa kejel cjaupenda na siko tayar,ona aibu badilika,....mzz mkuu nilimjibu mjumbe pale juu kuwa ciipend japo ikitokea nikafanya ndo naenjoy.asante
KUMCHEZEA MKE
Hakika katika jambo ambalo ni muhimu kwa mume kulichunga na kulilinda ni kumchezea chezea mke wake na haswa kabla ya kumuingilia, hili lina athari kubwa sana kati ya wanandoa wawili katika mahusiano yao ya kiroho na ya kijinsi.
Katika kufikia kilele cha raha ya kiwiliwili kunahitaji kwa mwanamme awe na diplomasia ili aweze kumpa mke wake hamu na matamanio ya kweli, na ushiriki mzuri ulio kamili na mapenzi yaliyokita.
Mke mwenye hekima anaweza kwa diplomasia aliyokuwa nayo na mapambo yake na usafi wa kiwiliwili chake kumvuta mume wake na kumtamanisha. Hivyo basi kumhimiza katika kuwasiliana kwa kiwiliwili vyao kwa urahisi na wepesi zaidi, mahaba siku zote yanatimiza furaha.
Ama kumuingilia mwanamke bila ya kuwepo vitangulizi huwa ni jambo lisilofaa na la kinyama la kutosheleza mahitaji ya mwanamme, kisha haupiti muda mrefu kamaliza haja na kukaa mbali ya mwanamke hali ya kuhema!.
Mwanamke siku zote hupendelea mumewe ashirikiane nae katika hisia zake kwa upole na wema na acheze nae kwa muda unaotosha kupandisha hamu na nyege zake. Na hivi vitangulizi vya jimai husaidia kuwafikisha wanandoa wawili katika utulivu kamili na hivyo kufikia kilele cha raha ya tendo la ndoa.
Last edited by a moderator: