Wrevta
JF-Expert Member
- Jan 18, 2023
- 1,442
- 1,733
Kazi iendelee!
"Wrevta unashirikiana na wenzako kweli?" Kauli hii kutoka kwa mwalimu wangu nikiwa sekondari miaka hiyo inanikumbusha machungu mno.
Nikajibu "ndiyo", ila ukweli ni kwamba sikuwa na ushirikiano wa kuridhisha na wenzangu. Muda mwingi nilipenda kusoma mwenyewe, ila sikuwa mchoyo wa materials au majibu pindi nilipoulizwa swali.
Hata nyumbani nilikuwa mkimya mno na nisiyependa mikusanyiko, nilikuwa hivi toka utoto... utotoni napo nina historia mbaya, hali inayofanya nisifurahie kukumbuka utoto wangu.
Nilipojifunza kuongea nilikuwa napenda kumuambia mzee mmoja "mzee jua litakuangukia", niliongea haya huku natazama juu kuliangalia jua na kumuambia kuwa litamuangukia.
Nimeishi mno karibu na ndugu wa kuzaliwa tumbo moja, na wale wa karibu sana. Ila marafiki na jamaa sikuwapa attention sana toka utotoni.
Siwezi kuwa mcheshi wala kuigiza kuwa mcheshi, kila nikianza mahusiano na msichana, baada ya muda mfupi yanakufa tu automatically! Hali hii imezidi kunifanya niwe mpweke.
JF ndiyo rafiki na jamaa yangu, napitisha hata miezi bila kuwasiliana na rafiki wala jamaa. Nina namba zao zimejaa tu kwenye contact book yangu.
Sijui hali hii inanipeleka wapi...sijui wa kumuoa mpka dk hii, naumia zaidi kuona wenzangu wakiwa post 'to-be's' wao status na wakiwa vacations, mimi hata siku moja sijawahi kuwa na huyo wa kum post. Nasononeka mno!
Hivi kasoro yangu ni huu ukimya pekee? Mbona wengine ni wakimya na wana 'to-be's'? Mimi nina shida ipi? Au nimefungwa kimakusudi ili niwe hivi? Kwa maslahi gani huyo aliyenifunga anapata?
Wasichana wananichangamkia ila baada ya muda wanaanza kuniwekea vinyongo... najiuliza nakosea wapi? Au kwa kuwa siwatongozi? Au kwa kuwa nawachukulia kama marafiki tu in a positive way?
Kuna wakati napata kumbu kumbu za zamani hali inayoniumiza sana. Kwa nini maisha yapo hivi?
Hivi ni ushirikiano upi jamii na wasichana wanahitaji? Nataka nichague tu njia sahihi ya kuanza safari yangu ya mafanikio. Nafikiria nichague Islam au Christianity au Budhaism au nirudi kwenye imani za mababu!
Hii hali inaniumiza sana... mimi mbona ni kijana handsome nakosea wapi? Ugomvi wangu na wasichana wengi unaanzia wapi? Sina dharau, ni mtu safi tu.
Najua kuvaa vizuri na katika u smart! Je, wanani overrate? Wanakosa ujasiri kwangu? Mimi ni wa kawaida mno, why sijui uelekeo wangu kwenye maisha ya ndoa?
Sent from my SM-G800F using JamiiForums mobile app
"Wrevta unashirikiana na wenzako kweli?" Kauli hii kutoka kwa mwalimu wangu nikiwa sekondari miaka hiyo inanikumbusha machungu mno.
Nikajibu "ndiyo", ila ukweli ni kwamba sikuwa na ushirikiano wa kuridhisha na wenzangu. Muda mwingi nilipenda kusoma mwenyewe, ila sikuwa mchoyo wa materials au majibu pindi nilipoulizwa swali.
Hata nyumbani nilikuwa mkimya mno na nisiyependa mikusanyiko, nilikuwa hivi toka utoto... utotoni napo nina historia mbaya, hali inayofanya nisifurahie kukumbuka utoto wangu.
Nilipojifunza kuongea nilikuwa napenda kumuambia mzee mmoja "mzee jua litakuangukia", niliongea haya huku natazama juu kuliangalia jua na kumuambia kuwa litamuangukia.
Nimeishi mno karibu na ndugu wa kuzaliwa tumbo moja, na wale wa karibu sana. Ila marafiki na jamaa sikuwapa attention sana toka utotoni.
Siwezi kuwa mcheshi wala kuigiza kuwa mcheshi, kila nikianza mahusiano na msichana, baada ya muda mfupi yanakufa tu automatically! Hali hii imezidi kunifanya niwe mpweke.
JF ndiyo rafiki na jamaa yangu, napitisha hata miezi bila kuwasiliana na rafiki wala jamaa. Nina namba zao zimejaa tu kwenye contact book yangu.
Sijui hali hii inanipeleka wapi...sijui wa kumuoa mpka dk hii, naumia zaidi kuona wenzangu wakiwa post 'to-be's' wao status na wakiwa vacations, mimi hata siku moja sijawahi kuwa na huyo wa kum post. Nasononeka mno!
Hivi kasoro yangu ni huu ukimya pekee? Mbona wengine ni wakimya na wana 'to-be's'? Mimi nina shida ipi? Au nimefungwa kimakusudi ili niwe hivi? Kwa maslahi gani huyo aliyenifunga anapata?
Wasichana wananichangamkia ila baada ya muda wanaanza kuniwekea vinyongo... najiuliza nakosea wapi? Au kwa kuwa siwatongozi? Au kwa kuwa nawachukulia kama marafiki tu in a positive way?
Kuna wakati napata kumbu kumbu za zamani hali inayoniumiza sana. Kwa nini maisha yapo hivi?
Hivi ni ushirikiano upi jamii na wasichana wanahitaji? Nataka nichague tu njia sahihi ya kuanza safari yangu ya mafanikio. Nafikiria nichague Islam au Christianity au Budhaism au nirudi kwenye imani za mababu!
Hii hali inaniumiza sana... mimi mbona ni kijana handsome nakosea wapi? Ugomvi wangu na wasichana wengi unaanzia wapi? Sina dharau, ni mtu safi tu.
Najua kuvaa vizuri na katika u smart! Je, wanani overrate? Wanakosa ujasiri kwangu? Mimi ni wa kawaida mno, why sijui uelekeo wangu kwenye maisha ya ndoa?
Sent from my SM-G800F using JamiiForums mobile app