Nipo hapa Muhimbili National Hospital toka saa 6 hakuna umeme

Pi Network

JF-Expert Member
Mar 22, 2016
290
319
Kama kichwa cha habari kinavyojieleza, huduma zote zimesimama ikiwa ni pamoja na utoaji dawa kwa wagonjwa hali ambao imepelekea watu kukaa kusubiri umeme.

Kutokana na hali hiyo binafsi ikabidi nijipe jukumu la uandishi wa habari wa mda kwa kuzungumza na doctor mmoja ambae alikuwa karibu na eneo nililokuwepo ili kujua undani wake.

Kwa mujibu wa maelezo ya dokta huyo (jina kapuni), anasema tatizo la kukosekana kwa umeme hapa hospitalini si jambo lililo anza leo, anasema hili ni tatizo la mda mrefu na mara kwa mara wamekuwa wakililalamikia kwa mda mrefu bila mafanikio.

Swali la kipima joto kwa wote mliopo humu; inawezekanaje hospitali kubwa namna hii na inayotegemewa, Tanzania nzima kama sio (Africa Mashariki) kukosa umeme wa uhakika?
 
Hapo huwa kuna standby generator. Muulize huyo Daktari Jina Kapuni kama pesa ya mafuta ya generator wameacha kuitafuna!?
 
Umeme umekataa city centre maeneo mengi tu.... So Usijali tunafanya marekebsho unarudi Saiv
USIKANYAGE WALA KUSHIKA WAYA ULIOANGUKA CHINI.. TOA TAARIFA MAPEMA
 
Ukiwa kama unaenda MOI ukitokea pale Mortuary, ukipita tu jengo wanalofanyia ibada ya kuaga wapendwa waliotangulia, upande wa kulia kuna ofisi ya MKURUGENZI WA UFUNDI, Kyara. Ebu kachukue maelezo pale.....kwanini STANDBY GEN SET haifanyi kazi?
 
Kama kichwa cha habari kinavyojieleza, huduma zote zimesimama ikiwa ni pamoja na utoaji dawa kwa wagonjwa hali ambao imepelekea watu kukaa kusubiri umeme.

Kutokana na hali hiyo binafsi ikabidi nijipe jukumu la uandishi wa habari wa mda kwa kuzungumza na doctor mmoja ambae alikuwa karibu na eneo nililokuwepo ili kujua undani wake.

Kwa mujibu wa maelezo ya dokta huyo (jina kapuni), anasema tatizo la kukosekana kwa umeme hapa hospitalini si jambo lililo anza leo, anasema hili ni tatizo la mda mrefu na mara kwa mara wamekuwa wakililalamikia kwa mda mrefu bila mafanikio.

Swali la kipima joto kwa wote mliopo humu; inawezekanaje hospitali kubwa namna hii na inayotegemewa, Tanzania nzima kama sio (Africa Mashariki) kukosa umeme wa uhakika?
Mimi sijui
 
Hapo huwa kuna standby generator. Muulize huyo Daktari Jina Kapuni kama pesa ya mafuta ya generator wameacha kuitafuna!?
Zipo lkn zinakuwaga mbovu...
Uliza zina miaka mingapi...je hazifi..wamenunua mpya lini
 
Tuliambiwa gesi itatatua tatizo la umeme nchini kumbe sound tupu.

Bongo kila kitu kinaishia kwenye makaratasi tu.
 
Kama kichwa cha habari kinavyojieleza, huduma zote zimesimama ikiwa ni pamoja na utoaji dawa kwa wagonjwa hali ambao imepelekea watu kukaa kusubiri umeme.

Kutokana na hali hiyo binafsi ikabidi nijipe jukumu la uandishi wa habari wa mda kwa kuzungumza na doctor mmoja ambae alikuwa karibu na eneo nililokuwepo ili kujua undani wake.

Kwa mujibu wa maelezo ya dokta huyo (jina kapuni), anasema tatizo la kukosekana kwa umeme hapa hospitalini si jambo lililo anza leo, anasema hili ni tatizo la mda mrefu na mara kwa mara wamekuwa wakililalamikia kwa mda mrefu bila mafanikio.

Swali la kipima joto kwa wote mliopo humu; inawezekanaje hospitali kubwa namna hii na inayotegemewa, Tanzania nzima kama sio (Africa Mashariki) kukosa umeme wa uhakika?
Huenda standby generator haina mafuta au imeharibika
 
Back
Top Bottom