cocochanel
Platinum Member
- Oct 6, 2007
- 28,899
- 78,944
Maji ya baraka ni kutoka mto wa baraka mkuu..
Hayo ndio siamini kabisa. Kama Yesu hajanitosha basi sidhani kama kuna kibadala kingine.
Mimi nilikushauri utoe kabisa ili tuone inakuwaje ila tunasubir mrejesho mwenyez mungu akulinde.
Sasa hivi ndo nataka nilale na ndio nimevikagua viatu na kuhakikisha carpet yake ipo sawa japokuwa sio ndio nilivivaa leo wala jana. Nimefunga mlango na nishamshukuru Mungu kwa kunilinda katika siku.
Akili inakuambia hutshiki na ushirikina lkin kimsingi umeamini ushirikina.Niposa safarini nchi jirani kibiashara na nimeshukia nyumbani kwa rafiki yangu. Nimepewa chumba changu na ninalala humo peke yangu. Cha kunishangaza kama wiki tatu zilizopita nimeamka asubuhi nikakuta kiatu ninachovaa cha mguu wa kushoto ile carpet ya kukanyagia ndani ya kiatu imegeuzwa ndani nje. Nikajiuliza maswali mengi bila kupata jibu. Mimi ni mkristo nisiyetishika na mauza uza ya kishirikina nilikipiga kiatu damu ya Yesu na kuondoa shaka lolote. Wiki mbili baadae nimekivaa kiatu kile na hapakuwa na dhara lolote. Ninachoshangaa ni kwamba juzi usiku kuamkia jana nimeamka asubuhi na kukuta kiatu kile kile cha mguu wa kushoto carpet lake la ndani limegeuzwa ndani nje. Nimejiuliza maswali mengi na sikupata jibu ila mimi kama mkristo thabiti nimetupilia mbali dhana zote zinazoaminiwa ktk uchawi na uganga. Msingi huu nimeujenga juu ya uthabiti wangu kwamba sikuwahi kumwamini mchawi wala kumpa usikivu wa namna yeyote ile na pia sikuwahi hata kushika wala kuamini katika hirizi ya namna yeyote ile.
Hebu wanye hekima wa Jf tushirikiane katika hili ni nani au nini kinageuza carpet ya kiatu changu usiku? Nia na dhumuni ni nini? Niko fiti mentally na physically na sijaruhusu kwa namna yeyote kujiathiri kisaikolojia.
Kubwa zima bado linaenda kukaa kwa watu? Aibuuuu!! Kukaa kwa watu tena nchi ya ugenini, basi iwe siku 2 au 3 sasa lenyewe leo miezi liko kwa watu! Mfanyabiashara gani huyu ambaye hajajipanga huyu? Yaani unataka upate faida in the expense of others? Aibuuuuuuu!! Hama hapo kiongozi!!Mkuu umesema umeenda kibiashara, je kama huyo jamaa yako asingekuwepo ungekaa wapi siku zote hizo? Unapokuwa na mashaka sehemu siyo vizuri kuendelea kuishi hiyo sehemu.