kitalolo
JF-Expert Member
- Dec 4, 2006
- 1,827
- 707
Ikiwa tutauvunja muungano basi kizazi kijacho kitatuona kuwa tulikuwa wabinafsi na wapumbavu na kitaurejesha muungano, kwamfano watu za Tanzania Visiwani watakiona kisiwa chao ni kidogo sana kwa wakati huo haswa ikizingatia pia ongezeko la watu, hivyo basi watatamani kama bara na visiwani ingerudi kuwa moja ili wapate fursa za kujitanua kukabilia na wingi watu na kuwa na fursa zaidi juu ya mambo mbalimbali ikiwamo uongozi kwa wenye uchu wa uongozi kwani kutokana na udogo wa kisiwa na idadi ya watu kupata fursa kama za kiuongozi itawa adimu sana.
Tatizo litakuja wapi? Ni pale watakaposhindwa kuurejesha muungano huo ambao wengi wao watakuwa wanautamani, kutokana tu na tuliouvunja tuliuvanja kwa misingi na vigezo vya kutokuurejesha tena, na pia ikiwa visiwani wamevamiwa na mataifa yenye uchu wa onyajaji wa rasilimali za mataifa ya africa kutokana na au kupatikana kwa mafuta zanziba, au kutokana tu na jinsi Zanzibar ilivyo kwa sasa yaani wakaitamani tu kwa njisi ilivyo sasa kwamba panaweza pakawekezwa kwaajili ya shughuli za kiutalia na pakawa kama visiwa vingi duniani ambapo zinafanyika shughuli ya utalii, na hivyo mabwanyeye hayo yakaona kwamba kwa kuwapa fursa kwa sehemu hizi mbili kurudi katika muungano basi kuna maslahi yao yataguswa kwa namna yoyote na hivyo basi kupelekea kunyima fursa hiyo ya muungano na ilihali wananchi wanatamani kuwepo kwa muungano na mabwanyenye yanazuia. basi watanzania visiwani watajiona watumwa ndani ya nchi yao wenyewe.
Kwavile miongoni mwa faida za muungano ni usalama wa mipaka kwa nchi zote mbili, kuwa na nguvu kama za kiuchumi, hivyo basi Tujaribuni kuuenzi na kuudumisha muungano kwa kuondoa kero zote za muungano na hivyo kuuwezesha muungani kudumu na vizazi vijavyo vikauka na ikiwa vitaamua kuuvunja kwa wakati huo basi hiyo itakuwa ni shauri lao, labda pengine kwa wakati huo kutokana na hali ya dunia itakuwa imewalazimu kuuvunja basi na wauvunje lakini si sasa
Tatizo litakuja wapi? Ni pale watakaposhindwa kuurejesha muungano huo ambao wengi wao watakuwa wanautamani, kutokana tu na tuliouvunja tuliuvanja kwa misingi na vigezo vya kutokuurejesha tena, na pia ikiwa visiwani wamevamiwa na mataifa yenye uchu wa onyajaji wa rasilimali za mataifa ya africa kutokana na au kupatikana kwa mafuta zanziba, au kutokana tu na jinsi Zanzibar ilivyo kwa sasa yaani wakaitamani tu kwa njisi ilivyo sasa kwamba panaweza pakawekezwa kwaajili ya shughuli za kiutalia na pakawa kama visiwa vingi duniani ambapo zinafanyika shughuli ya utalii, na hivyo mabwanyeye hayo yakaona kwamba kwa kuwapa fursa kwa sehemu hizi mbili kurudi katika muungano basi kuna maslahi yao yataguswa kwa namna yoyote na hivyo basi kupelekea kunyima fursa hiyo ya muungano na ilihali wananchi wanatamani kuwepo kwa muungano na mabwanyenye yanazuia. basi watanzania visiwani watajiona watumwa ndani ya nchi yao wenyewe.
Kwavile miongoni mwa faida za muungano ni usalama wa mipaka kwa nchi zote mbili, kuwa na nguvu kama za kiuchumi, hivyo basi Tujaribuni kuuenzi na kuudumisha muungano kwa kuondoa kero zote za muungano na hivyo kuuwezesha muungani kudumu na vizazi vijavyo vikauka na ikiwa vitaamua kuuvunja kwa wakati huo basi hiyo itakuwa ni shauri lao, labda pengine kwa wakati huo kutokana na hali ya dunia itakuwa imewalazimu kuuvunja basi na wauvunje lakini si sasa