Nini tatizo

suranne

Senior Member
Aug 12, 2010
120
246
Hebu wana JF anayejua japo anijuze!
Tatizo hili la kugawa mikoa na wilaya ni kwa manufaa ya nani au ni ongezeko la watu ktk hayo maeneo kama ndivyo mbona DAR hizo mikoa hazina wakuu wa kila KANDA (hiyo mikoa mitatu)?Labda kuna watu walikosa nafasi za uongozi so wanatafutiwa?
Kwa fikira zangu naona tatizo ni hawa wateule(madc) na wengine kutokuwajibika vizuri hivyo kusababisha watu kukosa huduma zinazohitajika kwa jamii hivyo kuonesha kuwa kunahitajika kusogeza zaidi huduma kwa kuunda mikoa na wilaya?
Naomba kuwasilisha!



:washing:
 
Kwa uelewa wangu mdogo, Kuna sababu kadhaa nzuri na mbaya, zenye maslahi kwa taifa na ambazo hazina maslahi, za kugawa mikoa na wilaya. Ukweli ni kwamba sababu iliyo nzuri ni ile ya kuboresha au kurahisisha ufikishaji wa huduma kwa wananchi. Pia, si unajua kuwa JK anapenda kulipa fadhila kwa awapendao hata kama ni mafisadi; hiyo amegawa mikoa na wilaya ili hatimaye apate kazi ya kuwapa rafiki zake pindi akishinda uchaguzi (ingawaje mwaka huu kidogo hali kwake na wabunge wake si rahisi kama ilivyokuwa 2005). la mwisho, hii nimbinu ya kusababisha hata kuongeza majimbo ya uchaguzi ili kujaribu kuhakikisha kuwa nguvu ya CCM haipungui hata wakati viti vingi vitakuwa vimechukuliwa na chadema.

Kidumu chama ya Demokrasia na Maendeleo!
 
Back
Top Bottom