KENZY
JF-Expert Member
- Dec 27, 2015
- 26,200
- 56,826
Nikama vile naona mapichapicha yasiyoeleweka!,lkn hii ni dhahiri kuwa Hawa wenzetu wamegeuka mbogo!.kwanza ni Jambo linaloumiza kwani hata Kama ni kufukuzwa si kwa namna hiyo ya kuchomana na kurushiana mawe!
Hii si ile Afrika ya enzi za kina nyerere hasa wakati ule wa kupigania Uhuru ambapo adui yetu alikuwa mmoja!,ambae alitufanya tushikamane na kupambana nae.. hivi sasa mambo yamebadilika,baada ya kuwa huru sasa tumeanza kugeukiana sisi kwa sisi‼,hili tu linatosha kutukana nguvu walizojitoa wazee wetu ktk kupambana Uhuru wa viumbe ambao Leo hii twajizuru sisi kwa sisi hiyo ndio tafsiri yake.
Mbali na hapo yale tuliyoyaita mabeberu ndo kwanza yamekaa pembeni yakicheka kwa tuo kwa kuona watoto walioachiwa uhuru wakiutumia Uhuru huo kwa kujizuru wao!.Hivyo hili linatosha kutoa tafsiri ya udhaifu wetu mbele ya adui yetu.
Watu Kama gadafi na nyerere wao walikuwa na mtazamo wa tofauti kwani walihitaji Afrika kuwa moja‼,lkn kwa hili kikulacho ki nguoni mwako huko Afrika ya kusini kinatoa tafsiri ya kuwa Afrika kuwa moja kwa kuungana ni nadharia ambayo hata ndoto haipo!!.
Tukio Kama hili halijaanza Leo ni kidonda ambacho kimeshahamishia makazi yake eneo husika mpk kufikia hadhi ya kuitwa kidonda ndugu‼,hili pia linatafsiri kuwa viongozi wa eneo husika wameshindwa kutatua tatizo ambapo hata kushindwa kwao ni tatizo pia. Kama pia Afrika kwa ujumla tutashindwa kuchukua hatua dhidi ya Kile kinachoendelea napo pia itakuwa ni tatizo‼.Kama hatujui pia waafrika tumekosea wapi Basi hili pia ni tatizo na Kile kinachotupata ni matokeo ya matatizo.
Hii si ile Afrika ya enzi za kina nyerere hasa wakati ule wa kupigania Uhuru ambapo adui yetu alikuwa mmoja!,ambae alitufanya tushikamane na kupambana nae.. hivi sasa mambo yamebadilika,baada ya kuwa huru sasa tumeanza kugeukiana sisi kwa sisi‼,hili tu linatosha kutukana nguvu walizojitoa wazee wetu ktk kupambana Uhuru wa viumbe ambao Leo hii twajizuru sisi kwa sisi hiyo ndio tafsiri yake.
Mbali na hapo yale tuliyoyaita mabeberu ndo kwanza yamekaa pembeni yakicheka kwa tuo kwa kuona watoto walioachiwa uhuru wakiutumia Uhuru huo kwa kujizuru wao!.Hivyo hili linatosha kutoa tafsiri ya udhaifu wetu mbele ya adui yetu.
Watu Kama gadafi na nyerere wao walikuwa na mtazamo wa tofauti kwani walihitaji Afrika kuwa moja‼,lkn kwa hili kikulacho ki nguoni mwako huko Afrika ya kusini kinatoa tafsiri ya kuwa Afrika kuwa moja kwa kuungana ni nadharia ambayo hata ndoto haipo!!.
Tukio Kama hili halijaanza Leo ni kidonda ambacho kimeshahamishia makazi yake eneo husika mpk kufikia hadhi ya kuitwa kidonda ndugu‼,hili pia linatafsiri kuwa viongozi wa eneo husika wameshindwa kutatua tatizo ambapo hata kushindwa kwao ni tatizo pia. Kama pia Afrika kwa ujumla tutashindwa kuchukua hatua dhidi ya Kile kinachoendelea napo pia itakuwa ni tatizo‼.Kama hatujui pia waafrika tumekosea wapi Basi hili pia ni tatizo na Kile kinachotupata ni matokeo ya matatizo.