NewDawnTz
JF-Expert Member
- Nov 15, 2010
- 1,667
- 362
Hakuna kitu kinachonipa mashaka sasa ninapotafakari siasa za Tanzania zinapopeleka usalama wa nchi yetu kama swala la hivi vikundi vyao vya "askari" vinavyofanya kazi chini ya vyama vya siasa (Militia groups affiliated under Political parties). Hapa nazungumzia Green Guards ya CCM na Red Brigade (kama sijakosea jina - naweza kurekebishwa) ya CHADEMA.
Nimejiuliza maswali mengi sana hasa baada ya matukio ya hivi karibuni ambayo yanahusisha vikundi hivi kuhusika ikiwemo matukio kadha wa kadha huko Igunga pamoja na yaliyotokea jana huko Mwanza kama yalivyowasilishwa na baadhi ya members wa JF kuhusu Green Guard kupiga watu hadi kuwajeruhi huko Mwanza.
Naomba tujadili mwelekeo wa siasa ya Tanzania na kuwepo kwa vikundi hivi chini ya vyama kwa kuzingatia mambo yafuatayo.
ANGALIZO:
Hapa sizungumzii unstructured group kama vile kundi la watu ambalo halikuwa limejipanga kufanya kitu fulani ila imetokea ghafla wakajikuta kuwa na common interest na kujiunga kufanya jambo fulani.
Hapa nazungumzia kundi la watu ambalo limeandaliwa, limepewa jina, linafahamika na wanapatiwa hadi usafiri na nafasi ya kusimama mstari wa mbele au "kulinda usalama" huku wahusika wakiwa wanajua lipo kundi la namna hiyo na wakitolerate existence yavyo na utekelezaji wa "shughuli" zao.
Na pia tujadili kwa mustakabali wa maendeleo ya taifa na sio kwa "maslahi"ya vyama vyetu vya siasa nikikopa msemo wa Invisible "Tujadili kiuhalisia na sio kisiasa"
Naomba niwasilishe kwenu kwa mjadala zaidi......
UPDATE: April 2015 > IGP Mangu: Marufuku kuwa na Vikundi vya Ulinzi vya Vyama vya siasa kwani ni kinyume cha Katiba na Sheria ya nchi
Nimejiuliza maswali mengi sana hasa baada ya matukio ya hivi karibuni ambayo yanahusisha vikundi hivi kuhusika ikiwemo matukio kadha wa kadha huko Igunga pamoja na yaliyotokea jana huko Mwanza kama yalivyowasilishwa na baadhi ya members wa JF kuhusu Green Guard kupiga watu hadi kuwajeruhi huko Mwanza.
Naomba tujadili mwelekeo wa siasa ya Tanzania na kuwepo kwa vikundi hivi chini ya vyama kwa kuzingatia mambo yafuatayo.
- Hawa watu ni wakina nani? Je kuna sheria yoyote inayotoa uhalali wa kuwepo kwavyo?
- Je katiba za vyama vya siasa zinasehemu yoyote inayozungumzia kuwepo kwa vikundi hivi? Na kama ndiyo, je zimeanishaje majukumu ya vikundi hivi? Na je kuna uhalali wa kisheria unaotoa mwanya kwa vyama vya siasa kujianzishia vikundi kama hivi? Je inakubalika kuwepo kwa sheria ya namna hiyo?
- Je sheria ya vyama vya siasa inaruhusu kuwepo kwa vikundi hivi ndani ya vyama vya siasa? Kama sivyo je huu sio uvunjaji wa Sheria za Uanzishwaji wa Vyama vya siasa unaohitaji kuchukuliwa hatua? Au ndio tuseme "When the State is corrupt then the laws are most multiplied?"
- Je kuna wakati wowote ambao kuna kiongozi yoyote mwenye mamlaka ya usimamizi wa vyama vya siasa (Hapa namzungumzia Msajili wa Vyama vya Siasa ndugu John Tendwa) ametoa kauli ya kuzuia vikundi hivi? J e wale wenye mamlaka ya kusimamia usalama wa Taifa na Raia wake (Nazungumzia Jeshi la Polisi Tanzania na Jeshi la Wananchi wa Tanzania) wametoa kauli dhidi ya vikundi hivi ambavyo ni hatari kwa usalama wa Raia na Taifa kwa ujumla wake? Au ndio "Polisi Jamii" wenyewe?
- Je kuwepo kwa vikundi hivi ni ishara ya jeshi la polisi kushindwa kusimamia usalama wa shughuli za vyama vya siasa na ulinzi wa wanasiasa na kulazimisha kuanzishwa kwa vikundi hivi na vyama vya siasa ili kujihakikishia usalama?
- Je sisi kama Watanzania tunaona ni vema kwa vikundi hivi kuendelea kuwepo na kufanya kazi chini ya vyama vya siasa tena pasipo sheria halali wala majukumu yanayoeleweka? Viongozi wa vyama vya siasa mlioko hapa, bila kutafuna maneno, je mnadhani siasa yetu inahitaji sana vikundi hivi na wala sio polisi kusimamia yale ambayo vikundi hivi mmevianzishwa "kihunihuni"?
ANGALIZO:
Hapa sizungumzii unstructured group kama vile kundi la watu ambalo halikuwa limejipanga kufanya kitu fulani ila imetokea ghafla wakajikuta kuwa na common interest na kujiunga kufanya jambo fulani.
Hapa nazungumzia kundi la watu ambalo limeandaliwa, limepewa jina, linafahamika na wanapatiwa hadi usafiri na nafasi ya kusimama mstari wa mbele au "kulinda usalama" huku wahusika wakiwa wanajua lipo kundi la namna hiyo na wakitolerate existence yavyo na utekelezaji wa "shughuli" zao.
Na pia tujadili kwa mustakabali wa maendeleo ya taifa na sio kwa "maslahi"ya vyama vyetu vya siasa nikikopa msemo wa Invisible "Tujadili kiuhalisia na sio kisiasa"
Naomba niwasilishe kwenu kwa mjadala zaidi......
UPDATE: April 2015 > IGP Mangu: Marufuku kuwa na Vikundi vya Ulinzi vya Vyama vya siasa kwani ni kinyume cha Katiba na Sheria ya nchi