Nini matumizi ya Mabondo ya Samaki Sangara?

Nini matumizi ya Mabondo ya Samaki Sangara?

Mkuu nacho jua mimi hayaliwi bali ndio yanatengeneza nyuzi z kushona miili ye2 baada ya operation ndio mana kilo yake now inaweza kua juu ya elfu 10 au zaidi miaka 10 iliyopita ilikua 6000sh perkg palepale mwz
I think sio hizi nyuzi za hapa Tz. Ni Gundi ya ngozi au tissues. Maana hawa jamaa wanatechnologia ya kugundisha human tissues. So kama ngozi imechanika hawashoni bali wanagundiisha kutumia ayo mabondo. Hii ndyo inatumika hasa kwenye face surgery, na intestine surgery.
 
Thamani ya bondo inatokana na daraja la bondo. Kuhusu tumizi sijui ila nachojua bondo huhesabiwa thamani kutokana na uzito

Daraja la kwanza tsh 2300 kwa gram

Ila daraja la mwisho ni chini ya tsh 100 kwa gram. Hivyo yote yatajaa hapo kati
 
Hata kma ni kg 5 si ulipatakama milion 3
Hapana mkuu Lile Bondo lilikuwa na kilo sita na point kadhaa samaki mwenyewe hakuwa mpya!

So jamaa alitupa million 4 Lakini kwa mujibu wadau mshikaji inaonekana alitupiga Sana

Basi hatukuwa na namna ukizingatia samaki yenyewe tuliokota na Bado tulikuwa watatu TU!

Kilichofuata NI kupasuka na Kila mmoja kutafuta sehemu nzuri ya kuweka heshima
 
Thamani ya bondo inatokana na daraja la bondo. Kuhusu tumizi sijui ila nachojua bondo huhesabiwa thamani kutokana na uzito

Daraja la kwanza tsh 2300 kwa gram

Ila daraja la mwisho ni chini ya tsh 100 kwa gram. Hivyo yote yatajaa hapo kati
Mkuu hivi unajua unachoandika?
 
Mkuu hivi unajua unachoandika?
Mkuu kwenye mabondo Kuna madaraja manne

1 chips
2 small
3 big
4 large

Namba nne kama nimekosea naomba mnisahihishe

Lakini hapo Kila ukubwa unathamani yake!

Mfano kilo maja ya chipsi hailingani thamani na kilo maja ya small

Na small hailingani na big na big hailingani na (large) mtarekebisha hapo Sina hakika Kama napatia kuandika Hilo neno
 
Mimi nachojua huwa yanapelekwa China!

Na swala la kutengeneza nyuzi za kushonea waliofanyiwa upasuaji na lenyewe nilishalisikia ingawa Sina uhakika nalo!
Kama matumizi yake ni hayo, naanza kukubaliana na watoa hoja. Zaidi, kama ukweli ndiyo huu, basi hata bei ya TZS 400,000/= kwa kilo bado ni ndogo sana. Sana sana ilitakiwa iwe angalua TZS 800,000/= au million moja kwa kilo. Wewe umesema neno.

Tatizo jingine ambalo mimi bado ninalo mpaka leo, bado sijapata kujua matumizi hasa ya pembe za ndovu au meno ya tembo, yanayopelekea meno hayo kuyafanya yawe na thamani kubwa namna hiyo. Mimi sijui mpaka leo
 
Mkuu hivi unajua unachoandika?
Nakijua ndiyo. Unachotakiwa ni kutofautisha kati ya kilogram na gram. Mfano bondo moja la kilo moja thamani yake ni 2300 kwa gram na mabondo kumi ya kilo moja thamani yake ni tsh 320 kwa gram.

Kinachofanyika pale ni kulipima bondo moja na kuliona uzito wake kisha mnachukua mabondo yote ya daraja hilo kuyapima yote kujua uzito wake jumra kisha mnachukua bei ya daraja mara uzito wa jumla.

Mfano.

Bondo la gram 200 mpaka gram 350 bei yake ni tsh 220 kwa gram

Hivyo ukiwa na mabondo kumi ya saizi hizo yatakupa uzito wa kilo tatu.

Hivyo unachukua 1000gram×3kg×tsh220=660000tsh.
Watu wanadanganyika utadhani bei ya bondo ni almas.

Kwa bei nazoziona hum jf bas wavuvi wote wangekuwa wanaendesha v8
 
Mkuu kwenye mabondo Kuna madaraja manne

1 chips
2 small
3 big
4 large

Namba nne kama nimekosea naomba mnisahihishe

Lakini hapo Kila ukubwa unathamani yake!

Mfano kilo maja ya chipsi hailingani thamani na kilo maja ya small

Na small hailingani na big na big hailingani na (large) mtarekebisha hapo Sina hakika Kama napatia kuandika Hilo neno
Yaani kwenye mabondo kuna daraja zaidi hata ya 20. Yaani chips ina daraja kama nne. Small inadaraja kibao. Midium ndo idadi yake ni kibao japo yote ni midium na large hivyohivyo
 
Yatakuwa mali sana kwa maana wadosi wa NPFL huwa wanaya-escort hadi Airport yanakwea pipa wala hayaendi kwa meli kama minofu.
 
Nakijua ndiyo. Unachotakiwa ni kutofautisha kati ya kilogram na gram. Mfano bondo moja la kilo moja thamani yake ni 2300 kwa gram na mabondo kumi ya kilo moja thamani yake ni tsh 320 kwa gram.

Kinachofanyika pale ni kulipima bondo moja na kuliona uzito wake kisha mnachukua mabondo yote ya daraja hilo kuyapima yote kujua uzito wake jumra kisha mnachukua bei ya daraja mara uzito wa jumla.

Mfano.

Bondo la gram 200 mpaka gram 350 bei yake ni tsh 220 kwa gram

Hivyo ukiwa na mabondo kumi ya saizi hizo yatakupa uzito wa kilo tatu.

Hivyo unachukua 1000gram×3kg×tsh220=660000tsh.
Watu wanadanganyika utadhani bei ya bondo ni almas.

Kwa bei nazoziona hum jf bas wavuvi wote wangekuwa wanaendesha v8
Mkuu hata hiyo hela uliyotaja kwa kilo mbona ni 'ndefu' sana tu ikiwa mvuvi anavua kila siku?
 
Mkuu hata hiyo hela uliyotaja kwa kilo mbona ni 'ndefu' sana tu ikiwa mvuvi anavua kila siku?
Mfano samaki ambaye anatoa bondo la gram 300 moja huyo samaki atakuwa na kg 9 ama zaidi. Hivyo bas samaki wengi tunaovua sisi babondo yao ni kati ya gram 45 mpaka 99 ambayo ni midium ya kwanza chini. Bei yake ni tsh 150 kwa gram hivyo bas kilo nzima itakupa tsh 150000. Unaweza iona ni kubwa kweli hebu tuiangalie. Samaki ambaye atatoa bondo la gram 60 uzito wake uko kati ya kilo 2 hadi tatu. Hivyo bas unapaswa uwe na samaki 17 ili upate kilo1 ya mabondo wa aina ile. Na endapo utawapima katika mzani watakupa uzito wa kati ya kilo 40 mpaka 50. Kwa hiyo ukiwauza bila kutoa bondo kwa bei ya 5000 kila kilo utapata kati ya 160k mpaka 200k. Na ukiwatoa mabondo unayauza 150k kisha unawaingiza sokoni wakaliwe kama mboga. Nadhani umeshanielewa.

Hata tukisema tuwaangalie hawa ambao mabondo yao yanauzwa kwa tsh 220 kwa gram. Ambao bondo lake linaanzia gram 250 _350 kuwapata kwake unatumia nyavu za aina nyingine. Zenye matundu makubwa ambayo huwezi pata samaki 10 kwa siku. Narudia tena. Ni vigumu kupata samaki kumi kwa siku ambao watakuwa na uzito wa kuanzia kilo 9 na kuendelea kwa kila mmoja ili uipate ile 660000 kwa mabondo tu
 
Back
Top Bottom